Monday, August 5, 2013

UJUE MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA, hali halisi sasa na malengo kwa muda mfupi ujao

TANZANIA MUSICIANS NETWORK ni mkusanyiko ya wadau wote wanaofanya kazi kwa njia moja au nyingine katika tasnia ya muziki. Muziki hapa ukiwa na maana ya mapana yake yote, muziki wa vikundi na ule wa watu mmoja mmoja, na bila kuwa na mipaka ya aina ya muziki na bila kujali kama ni muziki asili au muziki mapokeo, hivyo kila mtu anaefanya kazi ya muziki bila kujali umaarufu wake au aina ya muziki wake anakaribishwa. Chama pia kinakaribishwa watendaji wengine katika muziki kama vile mameneja , maproducer wa audio na video, mafundi mitambo wa studio na wale wa 'live', dancers maarufu kama stageshow, na wachezaji wa ngoma za asili. 
Wanachama wa Mtandao ni watu binafsi na si vikundi.
Mtandao una lengo la kuwakusanya wadau katika tasnia hii kuwa na sauti moja ili kuweza kurekibisha taratibu za utendaji katika tasnia hii na kuwawezesha wahusika wote kupata stahili zao kama inavyotakiwa. Mtandao ni mwanachama hai wa International Federation of Musician na hivyo moja ya malengo ya Shirikisho hilo ni kuhakikisha kazi ya muziki inatambuliwa kama ajira nyingine na hivyo kutungiwa sheria za kazi na taratibu za kazi kama kazi nyingine, na hivyo mtandao nao kulenga kufikisha hali hiyo kwa wanamuziki wa Tanzania. Kwa kipindi hiki cha awali ajenda nyingine kubwa ni kuweza kufanikisha kupatikana kwa Bima za Afya kwa wanamuziki wanachama mazungumzo yamekwisha anza na vyombo husika ili hili liwe limeanza kutekelezwa kabla ya mwisho wa mwaka.
Kwa wakati huu Mtandao uko chini ya uongozi wa muda 
Mwenyekiti:  John Kitime -Mwanamuziki Kilimanjaro Band
Katibu Mkuu: Abraham kapinga- Mwanamuziki Tanzanite band
Mweka Hazina: Asha Salvador- mwanamuziki Hisia Sound
Mpaka sasa kuna kamati mbili, zenye wanamuziki mchakanyiko vijana na wakongwe, ambazo ziko kazini
i. kamati ya utawala ambayo imewezesha kupatikana kwa ofisi na baadhi ya vifaa vyake na sasa inaanza taratibu za uandikishaji wa wanachama
ii. kamati ya fedha ambayo inaratibu mapato na matumizi ya fedha.
Kamati ya tatu itaanza kazi kabla ya tarehe 15 mwezi huu ambayo itashughulikia na utayarishaji wa ripoti ya hali halisi ya shughuli za Hakimiliki, jambo ambalo litahusisha researchers wa ndani na nje ya nchi, workshop kubwa ya wanamuziki mwezi wa tisa, na hatimae shughuli nzima kutoa ripoti ambayo itaweza kutumika na vyombo mbalimbali vinavyohusika na muziki na ripoti itasaidia sana Serikali kuanza kutoa maamuzi sahihi.

No comments:

Post a Comment