Tuesday, May 28, 2013

SOMA GAZETI LA INTERNATIONAL FEDERATION OF MUSICIANS HAPA

INGIA HAPA KUSOMA GAZETI LA INTERNATIONAL FEDERATION OF MUSICIAN BONYEZA

Tanzania Musicians Network chaanza upya kwa kishindo

-->
Tanzania Musicians Network au Mtandao wa  Wanamuziki Tanzania ni chombo kilichosajiliwa BASATA  2004, kilianza kwa nguvu mwaka 2006 na kufikia kuwa na wanachama 400, lakini  kilipata pigo mwaka 2007 kwa jengo ambalo lilikuwa ofisi ya chama hiki kuvunjwa na kulibadilishwa matumizi na mwenye mali, cham kikadorora.
Kutokana na umuhimu wa chombo hiki na kutokana na pengo la chombo chenye kukusanya wanamuziki wote na washiriki wengine kwenye muziki, wakiwemo, wanamuziki, wachezaji( stage show), sound engineers wa studio na wa muziki ‘live’, producers, managers na wadau wengine wa aina hiyo, imelazimika kukifufua tena chombo hiki muhimu.  Lengo kuu la mtandao huu ni kuwa chama cha wafanyakazi wanamuziki (Musicians Union). Chombo chenye kulea na kukuza shughuli hii kuwa yenye taratibu zinazompasa mfanya kazi wa kazi hizi, kama inavyokuwa katika ulimwengu sehemu nyingine.Chombo hiki ni mwanachama hai wa Shirikisho la Wanamuziki Duniani (FIM).
Kwa sasa ajenda iliyo mbele ni bima ya afya ya wanamuziki. Si siri kuwa tatizo la matunzo na huduma za wanamuziki na wafanyakazi wengine wa tasnia hii ni gumu pale afya zao zinapokuwa na matatizo, hivyo tayari viongozi wameshakuwa na mazungumzo ya awali na moja ya vyombo vya bima ya afya na kinachosubiriwa ni wanamuziki kujiunga na chombo hiki ili kuweza kuanzisha taratibu hizi.
Pamoja na malengo haya Mtandao huu utaendesha semina na warsha kwa ajili ya wanamuziki wanachama katika Nyanja mbalimbali za mambo ya muziki. Katika kipindi hiki hiki tayari mtandao umewezesha wafadhili kufadhili utafiti kuhusu matatizo yaliyomo katika biashara ya muziki jambo ambalo litawezesha wafadhili kufadhili miradi itakayobuniwa katika kurekibisha hali hiyo ngumu.
Tunakaribisha maombi ya uwanachama, unaweza kuonyesha nia kwa kutuma jina na anwani yako katika inbox ya ukurasa facebook Wanamuziki wa Tanzania au kupitia anwani ya musicnettz@yahoo.com na utaweza kuwapewa maelezo ya ziada. Tuma jina lao, jinsia, mahala uliko, namba ya simu, anwani ya email na taaluma unayoshiriki, …. UMOJA NI NGUVU