Wednesday, March 29, 2017

UNATAKA KUSHIRIKI TAMASHA LA SANAA UGANDA?


JE,  unataka kushiriki katika tamasha la Bayimba International Festival, ambalo litafanyika tarehe 15-17 September 2017  Kampala, Uganda?

Tamasha la mwaka huu litakuwa ni la kumi. Ni tamasha ambalo linajumuisha muziki, dansa, maonyesho jukwaani, filamu, vichekesho, mashahiri, na sanaa za maonyesho. Wanaohitaji kushiriki ni muhimu kuwa wameshajaza fomu zao na kutuma ifikapo April 30. Katika tamasha la mwaka jana walikuweko wasanii wa Hiphop kama  Akua Naru kutoka Ghana, Tribute ‘Birdie’ Mboweni toka Afrika ya kusini, bibie wa Kiganda ambae ni mpiga saxaphone wa mahadhi ya soul Mo Roots, kundi la Reggae toka Kenya Gravittii Band, na wengine wengi. Kutakuwepo na malipo kidogo kwa washiriki toka nje ya Uganda, japo washiriki wanashauriwa kutafuta njia za kulipia gharama za usafiri, viza na bima mbalimbali. Barua ya utambulisho itatolewa mara utakapokubaliwa kushiriki ili ikusaidie kutafuta ufadhili. Wanaotaka kushiriki wanatakiwa watoe taarifa zifuatazo,

·     Fomu ya ushiriki na kupitia bayimbafestival.com

·     Maelezo mafupi ya wasanii yasiyozidi maneno 800 na picha ya karibuni 

·     Nakala ya kazi yako, kama ni muziki au filamu kazi moja au mbili kwenye CD, DVD or mp3.

·     Mahitaji yako ya vifaa (technical rider/data sheet)

Watayarishaji watawajibu mapema waliofanikiwa.Fomu za maombi zinapatikana pia  HAPA