Sunday, July 16, 2017

RATIBA YA MSIBA WA MKE WA WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI NA MICHEZO

Mke wa mheshimiwa Waziri wa habari Utamaduni na Michezo, Dr Harrison Mwakyembe, Bi Linah Mwakyembe amefariki usiku wa kuamkia jana Jumapili, katika hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam alikokuwa anatibiwa. Ratiba ya msiba ni kama ifuatavyo:
Jumanne 18/7/2017 asubuhi mwili wa marehemu utawasili nyumbani kwa Mhe. Dr Mwakyembe Kunduchi Beach, kisha taratibu za Ibada na kuaga zitafuata na hatimae mwili kusafirishwa kwenda Kyela zitafanyika siku hiyohiyo. Mazishi yatakuwa Kyela siku ya Jumatano
Mungu Amlaze Pema Linnah Mwakyembe