Sunday, August 4, 2013

MASHUJAA BAND YATAMBULISHA NYIMBO ZAKE ITAKAZO REKODI


Jana Jumamosi  tarehe 3 Agosti, bendi ya Mashujaa ilifanya jambo ambalo ni nadra kufanyika katika bendi siku hizi. Bendi hii ilialika wadau na wapenzi wa bendi ili waweze kuzisikiliza nyimbo ambazo bendi hii inatarajia kuzirekodi. Bendi ilipiga mfululizo wa nyimbo  tano, zilizokuwa katika miondoko mbalimbali . Kwa ujumla bendi ina waimbaji wazuri sana kadri ya mazingira ya uimbaji wa siku hizi. Nyimbo zilikuwa nzuri japo zingeweza kuwa bora zaidi kwa kuongeza effects katika magitaa, na urekibishaji wa sauti  kwa ujumla(maarufu kama setting) , japo ungeboreshwa zaidi. Tatizo la setting ya vyombo kwa ujumla limekuwa sugu kwa bendi nyingi, kiasi kuwa kama ni kawaida kukuta sauti zikitoka kwa kikwaruzo na mara nyingine kutosikia waimbaji wanatamka nini katika wimbo.
Album hii itakuwa na mvuto kwa wapenzi wa muziki wa sebene, na pia ni album ya kwanza baada ya bendi hii kubeba tuzo tano katika Kili Music Awards karibuni.
Kati ya wadau waliokuweko katika shughuli hii ni wakali kama deo mwanatanga, William kaijage, Mafumu Bilali, Khalid Chokoraa, Khamis Dacota, John Kitime na wengine wengi walitoa mawazo yao kila baada ya wimbo kwisha ni jambo zuri kama litaendelezwa na pia kama litachukuliwa kwa uzito unaostahili na wanamuziki kwa upande wao.






No comments:

Post a Comment