Friday, December 13, 2013

GURUMO 53 - TAMASHA LA KUSTAAFU MUZIKI MUHIDIN MAALI GURUMO

Wanamuziki kadhaa wenye heshima katika muziki wa dansi watakuweko katika Tamasha la Gurumo 53, ambalo ni tamasha la kustaafu muziki  mwanamuziki mkongwe Muhidin Maalim Gurumo. Kati ya wanamuziki watakao panda jukwaani ni  Komandoo Hamza Kalala, Mzee Makassy, wanamuziki nyota waliowahi kutamba na bendi ya DDC Mlimani Park , Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe, Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa, Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande. Pia wapulizaji wakongwe Majengo na King Maluu watakuweko na wote kwa pamoja wataporomosha show kubwa Jumamosi hii ndani ya TCC Club Chang’ombe. Wakali hao  jana Alhamisi walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano watakazopiga katika tamasha hilo. Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo zilizofanyiwa mazoezi ni  pamoja na “Selina” utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa). Tamasha la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi kustaafu muziki. Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia, Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga. Burudani zingine zitakazokuwepo siku hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga Pepeta.

Wednesday, November 20, 2013

MWENYEKITI WA MTANDAO ATOA MADA YA UTAFITI WA MALIPO YA MIRABAHA

Katika Jukwaa la Sanaa ambalo huweko kila Jumatatu katika ukumbi wa BASATA , wiki hii Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime alichambua utafiti uliokamilika karibuni uliofanywa na mtafiti Martin Cuff kwa niaba ya Mtandao kwa ufadhili wa BEST AC. Utafiti huo ambao umo kwenye kitabu chenye kurasa 84 unachambua hali halisi ya Hakimiliki Tanzania, na mapungufu yake na kisha kutoa mapendekezo ya kuboresha hali hiyo kwa manufaa ya wenye Hakimiliki na tasnia ya muziki kwa ujumla. Kitabu cha utafiti huo kitapatikana baada ya muda si mrefu.




















Thursday, November 7, 2013

UBALOZI WA MAREKANI WAKABIDHI VITABU 800 KWA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA


Ubalozi wa marekani nchini Tanzania, leo hii 7/11/2013 umemkabidhi  vitabu vya Hakimiliki zaidi ya 800 Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network, John F Kitime katika hafla iliyofanyika katika maktaba ya Ubalozi huo uliopo jijini Dar es Salaam. Kitabu hicho chenye lugha mbili Kiswahili na Kiingereza kimetungwa na  Alex Perullo ambaye ni Associate Professor wa Anthropology na African Studieskatika chuo cha Bryant Marekani. Hiki ni kitabu cha pili cha aina hii kutungwa na Profesa huyu, cha kwanza alikisambaza kupitia Ubalozi huu huu miaka kumi iliyopita. Kwa vile kina lugha mbili kitabu hiki kina majina mawili kinaitwa Artistic Rights na Haki za Kisanii. Ni kitabu cha kurasa 98 ambacho kimejaa maelezo mengi kuhusu haki za wasanii, wasanii watakao kisoma watafaidika sana.
Mtandao wa Muziki Tanzania, utakisambaza kitabu hiki katika taasisi mbalimbali muhimu na pia utawapa bure wanachama wake nakala za kitabu hiki muhimu. Dibaji ya kitabu hiki imeandikwa na John Kitime.




Wednesday, October 30, 2013

WANAMUZIKI WA TANZANIA WAFANYA WARSHA KUBWA







Martin Cuff

 Warsha kubwa ya siku moja ya wanamuziki wa tanzania yafanyika pale Nyumbani Lounge. Wanamuziki kutoka kila aina ya muziki walikuweko. katika warsha hii iliyoomgozwa na mtafiti Martin Cuff ilikuwa ni kutoa report ya utafiti wake kuhusu hali halisi ya utekelezaji wa Ukusanyaji na ugawaji wa Mirabaha. Wanamuziki walipata nafasi ya kuchangia  na kutoa mapendekezo. Ripoti nzima kutoka katika wiki mbili zijazo. Utafiti ulifanywa na Martin Cuff na kuongozwa na Tanzania Musicians Network kwa ufadhili wa BEST AC.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ndie aliyefunga warsha hii kwa kusifu jitihada hii ya wanamuziki kufanya utafiti. Katika kukutana huku na Naibu Katibu mkuu wanamuziki walioingia mkataba na kampuni mojawapoya ringtones walilalamika kuwa waliingia mkataba wa miaka kumi na kampuni hiyo na baada ya hapo kampuni hiyo haikutaka hata kujibu barua zao, Naibu Katibu Mkuu aliwaita wahsanii hao ofisini kwake ili kuona cha kufanya, pia alimtaka Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network John Kitime amuone ili waongelee tatizo la TBC kutokulipa mirabaha na kuatafuta suluhu.


















Monday, October 28, 2013

MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA WAFANYA WARSHA YA SIKU MOJA


 
WANAMUZIKI takriban 70 leo wameshinda siku nzima wakijadili ripoti ya utekelezaji wa Hakimiliki katika kipengele cha kukusanya na kugawa mirabaha. Wanamuziki wakiongozwa na mtafiti kutoka Afrika ya Kusin martin Cuff leo walifanya warsha hiyo katika ukumbi wa Nyumbani Lounge. Warsha ilifungwa na Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya habari, Utamaduni na Michezo aliyesifu jitihada za wanamuziki kuweza kufanya kikao kama hiki.

Sunday, October 20, 2013

PRODUCERS WAHUDHURIA SEMINA YA HAKIMILIKI

Pamoja na kuwa leo ni siku ya Jumapili, watu wengi huwa wanapumzika, maproducer kadhaa wamejikusanya na kuhudhuria semina ya Hakimiliki iliyoendeshwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime. Semina hiyo iliyofanyika katika jengo la Sayansi na Teknolojia iliwawezesha Producers kufahamu nini maana ya Hakimiliki na vilevile kupata elimu ya awali kuhusu yaliyomo katika sheria ya Hakimiliki ya hapa nchini

JULIUS NYAISANGAH.... UNCLE J.,,.SUPER TALL HATUNAE TENA

MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA UNATOA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KWA NDUGU , RAFIKI, NA WANAMUZIKI WALIOWAHI KUFANYA KAZI NA MTANGAZAJI MKONGWE JULIUS NYAISANGA, ALIYEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO 20 OKTOBA, 2013 KATIKA HOSPITALI YA MAZIMBU MOROGORO.
MUNGU AMLAZE PEMA JULIUS, KAZI YAKO ULIOIFANYA KATIKA TASNIA YA MUZIKI HAITAFUTIKA

Wednesday, October 16, 2013

Je unapenda muziki wa Mashujaa Band?

Bendi ya Mashujaa imetengeneza ukurasa wao ambapo unaweza sasa kusikiliza nyimbo zao nyingi kutoka hapo. Je wewe au bendi yako mnanyimbo katika mtandao wa intanet, basi tutumie anwani au wimbo kupitia musicnettz@gmail.com ili tuuweke katika blog yetu.
Kwa kusikiliza nyimbo za Mashujaa ingia HAPA upate nyimbo zao

Thursday, October 3, 2013

KIPINDI CHA MIKIKI MIKIKI YA MUZIKI KUANZA KURUKA JUMAMOSI HII SAA 12:30 JIONI TBC RADIO YA TAIFA

BAADA ya kupata ufadhili wa BEST AC kwa kupitia Tanzania Heritage Project, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TMN), utaanza kurusha vipindi vya radio kupitia Radio TBC Taifa. Vipindi hivyo ambavyo vitaendeshwa na mwanamuziki na mwenyekiti wa Mtandao John Kitime. Kipindi cha kwanza kitaanza na kuangalia biashara ya muziki kwa kutegemea viingilio ilivyo na kama kweli inalipa na kitashirikisha kwa kukusanya maoni kutoka kwa wasikilizaji. Kipindi hiki ni mwanzo wa vipindi vingi vya redio vitakavyohusu muziki kama utamaduni, taaluma na kama biashara. Karibuni tusikilize na tutoe maoni kupitia blog hii na ukurasa wa facebook  https://www.facebook.com/wanamuzikiwa.tanzania Wanamuziki wa Tanzania tuna uwezo kama wanamuziki wengine duniani lakini tuna matatizo makubwa ya mpangilio katika tasnia yetu

Monday, September 30, 2013

WANAMUZIKI WAWILI WA TEMEKE WAFARIKI LEO

Msanii wa kundi la WATEULE, Malik Ahmed Moa maarufu kwa jina la Mack2B amefariki dunia leo. Msiba utakuwa Yombo kwa wazazi wake Mack 2B alikuwa producer na msanii wa raga, amefariki kutokana na ugonjwa wa figo uliokuwa unamsumbua muda mrefu
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMIN

**********************************************************
Joseph akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wakati akiwa African Stars
Mwanamuziki mpiga bezi wa siku nyingi Joseph Watuguru
amefariki mchana huu katika hospitali ya Amana. Watuguru amewahi kupigia bendi nyingi zikiwemo Bantu Group ya Hamza Kalala, Magoma Moto Sound, African Stars ile ya mwanzo kabisa Mchinga Sound, na katika siku zake za mwisho alikuwa bendi ya WK Sound ya Temeke. Watuguru aliwahi kushiriki katika bendi iliyotengenezwa na Producer kutoka Norway Sigbjorn Nedland iliyoitwa Mradi Group akiwa na akina Bob Rudala, Keppy Kiombile, John Saggati, Bizimana Ntavyu, Anania Ngoliga na wengine. Alikuwa mpiga bezi mzuri na pia fundi mitambo wa kutegemewa
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA

Tuesday, September 17, 2013

MTANDAO KUANDAA SEMINA YA WANAMUZIKI KUHUSU UKUSANYAJI NA UGAWAJI WA MIRABAHA KATIKA KAZI ZA MUZIKI

Kamati ya kuratibu mradi unaoendelea wawa Utafiti wa hali halisi ya ukusanyaji na ulipaji wa mirabaha leo imekaa na kupanga kufanya semina ya awali kwa baadhi ya wanamuziki ili kuanza kuelimisha taratibu za ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Semina hiyo itafanyika katika muda wa wiki mbili. Semina itahusisha wanamuziki wa aina tofauti za muziki, dansi, taarab, bongoflava, hiphop, gospel muziki asili nakadhalika

Sunday, September 15, 2013

MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA UFADHILI WA BEST AC


MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA umepata ufadhili kutoka Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) ili kuweza kufanya utafiti wa kina kupata ukweli wa hali halisi ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha ya muziki unaofanywa na COSOTA, na baada ya hapo kutoa ushauri wa nini kifanyike ili kuboresha hali iliyopo. Madhumuni ya mradi huu ni kuwezesha kufanya mabadiliko katika tasnia ya muziki ambayo yatatengeneza nafasi za ajira zenye tija ili kuwezesha tasnia kutoa mchango wake katika pato la Taifa, na kukuza sifa ya nchi kutokana na wasanii wengi wenye sifa waliomo hapa nchini.

Mradi utaangalia sheria zilizopo zinazohusu ugawaji wa mirabaha ya wanamuziki na mambo mengine yote yanayohusiana na shughuli ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha na kupendekeza taratibu za kuboresha hali.

Kamati za fedha na utawala zitaanza kazi wiki hii ili kuweza kufanikisha zoezi hili ambalo linatakiwa likamilike katika muda wa mwezi mmoja. Wanamuziki watashirikishwa katika semina ambayo itafanyika katika wiki chache zijazo.  Mtafiti kutoka Afrika ya Kusini amekwisha ingia mkataba na Mtandao ili kufanya kazi hiyo.

TANZANIA MUSICIANS NETWORK SECURES A GRANT FROM BEST AC



TMN has secured a grant from Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) to conduct a study to assess the existing arrangement under COSOTA in collection of music royalties and use the findings to provide clear and precise recommendations for appropriate interventions to advocate for change in collection system for the music industry growth of Tanzania.
The objective of the project is to initiate appropriate interventions that will support the Tanzania music industry to create the much needed jobs, subsequently taxes flowing back to government and enhancing the image of country built up from the talented artistes from institutionalized support for the industry.
The Project will specifically carry out a study to assess the legal framework regulating the distribution of royalties to musicians and other owners of copyright in works and all matters connected thereto and provide a report with recommendations.  The report will be used to engage with government to address the inefficiencies established with a purpose to strengthen the musicians' bargaining power in controlling the usage of their copyright.
The project is aims to examine the music industry landscape and the struggle on copyright protection, combating piracy, legislative instruments to implement copyright and managing music rights; mandate, transparency, fairness in collection and timely payment of royalties to artists.  The purpose is to seek government’s support to have clear distinguished roles of the Copyright Society of Tanzania (COSOTA) as a Government copyright office from that of collecting organization. The project should identify the important stake holders in the industry such as Publishers, Distributors, Manufacturers of musical works, lyrists, arrangers, producers, executive producers and such others and their roles in the Royalties payment chain.