Thursday, December 10, 2015

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AUNDA WIZARA MPYA

Nape
Mhe Nape M Nnauye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo

 Rais John Pombe Magufuli ameunda Wizara mpya itakayoshughulikia pia wasanii. Katika kutangaza baraza jipya la mawaziri ambalo hakika litakuwa dogo kama alivyoahidi wakati wa kampeni, pia Ria amekuja na Wizara mpya. Wizara ya Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo. Waziri aliyeteuliwa ni Mheshimiwa Nape Moses Nnauye. Kwa wengine tuliomo katika Wizara hii hakika tunaona tunahitaji mabadiliko mengi, yakiwemo uongozi wenye uzalendo wa kupenda utamaduni wa Kitanzania, pia uongozi utakaotengeneza na kuheshimu mtiririko wa uongozi wa kiserikali wa shughuli za Utamaduni. Pia tungependa uongozi ambao unakubali kusikiliza pande zote za wadau wa tasnia ya sanaa. Uongozi ambao utaelewa tofauti kati ya Utamaduni, sanaa na burudani. Uongozi ambao utakuwa wa kwanza kuhakikisha sheria na taratibu zihusuzo sanaa zinafuatwa. Tuna uhakika Mheshimiwa Nape atayaweza haya na zaidi, hivyo kuweza kuweka kumbukumbu ya uwepo wake katika historia ya sanaa ya nchi hii. Bado jina la Wizara linaleta chemsha bongo katika kipengele cha wasanii, je Wizara itahusika na wasanii au Sanaa? Najua inawezekana likaonekana ni swali la ajabu lakini ukukikumbuka tu kuwa kuna wizara ya kilimo sio ya wakulima, au wizara ya biashara na si ya wafanyabiashara, kuna wizara ya uvuvi si ya wavuvi, ni mifano michache ya kuonyesha changamoto hii.

Monday, November 23, 2015

JE WEWE NI MSANII WA BONGOFLEVA? USIKOSE HII


JOHN KITIME ATOA ELIMU YA HAKIMILIKI KWA VIONGOZI WA VYAMA NA VIKUNDI VYA SANAA

MWENYEKITI  wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, John Kitime, siku ya tarehe 19 Novemba 2015, alitoa semina ya Hakimiliki kwa zaidi ya wasanii 50 waliokuwa katika warsha iliyoandaliwa na Baraza la Sanaa La Taifa (BASATA). Katika semina hiyo iliyotambulika kama Capacity Buildingfor Art Association and Group Leaders in Tanzania ilifanyika Ilala Shariff Shamba zilipo ofisi za BASATA. Kitime aliweza kuwafahamisha washiriki nini maana ya Hakimiliki, matumizi yake mipaka yake na kugusia sheria ya Hakimiliki ya Tanzania inavyofanya kazi. John Kitime ambaye amekwisha fanya semina za aina hii katika nchi mbalimbali Afrika zikiwemo Ghana, Malawi, Senegal amekwisha karibishwa Kenya kufanya semina za aina hiyo.

WASHIRIKI MBALIMBALI WAKIKABIDHIWA VYETU VYA USHIRIKI


STELLAH JOEL





RAY

BRAITON


KAKA GANO





Tuesday, November 17, 2015

TAMASHA LA KUMSHUKURU MUNGU SASA KUFANYIKA DESEMBA 25 DIAMOND JUBILEE

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akifafanua jambo kwa umakini mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki kuhusu maandalizi ya tamasha la kumshukuru Mungu kwa amani na utulivu wakati wa Uchaguzi Mkuu litakalofanyika Desemba 25.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki kuhusu maandalizi ya tamasha la kumshukuru Mungu kwa amani na utulivu wakati wa Uchaguzi Mkuu litakalofanyika Desemba 25.

KAMPUNI ya Msama Promotions imeamua kuandaa Tamasha la muziki wa Injili litakalofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumshukuru Mungu nchi kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama, alisema wameamua kuua ndege wawili kwa jiwe moja, kwani sasa litafanyika Desemba 25, likibeba Sikukuu ya Krismasi na shukrani hiyo ya kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu.

Alisema kutokana na tamasha hilo kubeba ajenda hizo mbili kwa pamoja, kamati yake imelipa uzito mkubwa kwa upande wa suala la  maandalizi ambapo wameanza kuzungumza na waimbaji nguli wa kitaifa na kimataifa.

Msama alisema baada ya tamasha hilo kufanyika Desemba 25 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, litahamia katika mikoa mbalimbali itakayoteuliwa na kamati yake kwa kuzingatia kigezo cha wingi wa maombi na uwezo wao kifedha.

“Naomba ifahamike, tamasha hili la kumshukuru Mungu kuiwezesha nchi kuvuka salama katika mtihani mgumu wa Uchaguzi Mkuu uliokuwa na ushindani mkubwa, litafanyika Desemba 25 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee,” alisema Msama na kuongeza:

“Unaweza kuona ni tamasha ambalo safari hii litakuwa na uzito mkubwa, kwani litakuwa limebeba uzito wa Krismasi itakayoambatana na shukrani maalumu kwa Mungu kutokana na kuijalia nchi kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu,” alisisitiza Msama.

Kuhusu waimbaji, Msama alisema kamati yake itajitahidi kuwaleta wenye uzito na mvuto kulingana  na uzito wa tamasha hilo, akiamini litakuwa na mvuto wa tofauti na yaliyotangulia na kuwasihi wapenzi na mashabiki wa muziki wa Injili kukakaa mkao wa kupokea baraka za Mungu.

Msama kupitia Kampuni yake ya Msama Promotions, amechangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa muziki wa Injili nchini kupitia ubunifu wake wa kuratibu matukio ya muziki huo kuanzia tamasha la Pasaka, Krismasi na uzinduzi wa kazi za waimbaji mbalimbali.

Juhudi hizo za Msama ndizo zimeufanya muziki wa Injili kupata umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kiasi cha kuwa moja ya ajira kwa vijana wenye vipaji na karama ya kumtumikia Mungu kwa njia hiyo ya uimbaji.

Thursday, November 12, 2015

KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO ATEMBELEA BASATA


IMG_20151112_131420 Prof Elisante akiongea na akina mama wanaofanya sanaa ya kutengeneza Batik katika maeneo ya BASATAIMG_20151112_211008 Toka kushoto Godfrey Mngereza, Katibu Mtendaji BASATA, Prof Elisante Ole Gabriel, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, John Kitime Mjumbe wa Bodi BASATA, Kaimu Mkurugenzi wa Utamaduni 
KATIBU mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Vijana na Michezo Prof Elisante Ole Gabrielleo ametembelea Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA). Katibu MKuu baada ya kuzunguka na kuangalia maeneo yote ya Baraza, hatimae alikuwa na mkutano na wafanya kazi wa Baraza. Katika mkutano huo Katibu Mkuu alisema ametembelea Baraza ili kufahamiana,na pia kufafanua kauli mbiu ya Rais ya HAPA KAZI TU.
Katibu Mkuu alisifia Baraza kwa kusimamia sheria na taratibu zilizounda Baraza hilo. Profesa alilitaka Baraza kuhakikisha kuwa linakuwa na ufanisi zaidi na pia kuwezesha kutafuta masoko ya uhakika ya kazi za sanaa. Tanzania ina kazi nyingi sana za sanaa hivyo alilitaka Baraza kuhakikisha zinafahamika zinatangazwa, na zinasambazwa, ili kuleta manufaa kwa wasanii na kuchangia pato la nchi kwa kodi. Katibu Mkuu aliagiza kuwa viongozi wa Baraza wawe mfano katika utendaji wa kazi, heshima kwa watumishi wote na pia wawe waadilifu katika kazi zao. Katibu Mkuu aliwaasa watumishi wa Baraza kuipenda kazi yao kuwa wazalendo na kuwajibika ipasavyo, kuheshimu viongozi na kuwasiliana kwa staha pale kunapokuwa na tatizo. Aliwakumbusha wafanya kazi kuwahi kazini lakini pia alikumbusha uongozi kutokuwaweka wafanya kazi masaa ya ziada bila ya sababu za msingi, kwani wanahtaji kupumzika baada ya kazi za siku nzima. Aliwaonya watumishi kuhusu ‘majungu’ na kuwataka waepuka jambo hilo kwani ni chanzo cha kuharibu kazi. Kabla ya hotuba hii Katibu Mtendaji alimueleza Katibu Mkuu kuhusu changamoto za Baraza na baadhi ya njia ambazo zingefanywa kutatua changamoto hizo. Katibu Mkuu alisema kuwa yeye haridhiki na hali ya uchumi ya wasanii na alitaka Baraza lifanye kazi kubadili hali hii. Na mwisho alisisitika kuwa kauli ya Hapa Kazi tu ni ya ukweli na kila mtu aishi kwa kauli mbiu hiyo.
Kabla ya maelezo haya Katibu Mtendaji wa Basata alitoa baadhi ya changamoto za uendeshaji wa BASATA. Kati ya changamoto hizo alizitaja kuwa ni ukosefu wa sera za sanaa, kupitwa na wakati kwa sheria iliyounda Baraza. Mtawanyiko wa asasi zinazotawala wasanii. Ukosefu wa masoko ya sanaa, kutokukamilika kwa ukumbi wa BASATA, tatizo la siasa kujikita katika sanaa, na pia uhamasishaji wa Bima ya Afya kwa wasanii.
Katibu Mtendaji alimkabidhi Katibu Mkuu, nyaraka zote zilizotayarishwa kuhusu changamoto hizo

Thursday, October 29, 2015

KATIBU MTENDAJI WA BASATA AMKABIDHI MZEE MAPILI KADI YAKE YA BIMA YA AFYA

Katibu Mtendaji wa BASATA Bwana Ngereza, Mzee Mapili na Mama Shalua mmoja wa maafisa wa BASATA
KUPITIA mpango unaoratibiwa na TAMUNET, ambapo Mtandao huu umeingia makubaliano na Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa HHIF, mwanamuziki mkongwe wa siku ntingi ameweza leo kukabidhiwa kadi ya Bima ya Afya. Akikabidhiwa kadi hiyo Mzee Mapili alishukuru Mtandao wa Wanamuziki, na kusema kuwa mpango huu utamsaidia sana kwani ana matatizo ya moyo na figo na anahitaji matibabu na dawa za mara kwa mara. Katibu Mtendaji wa BASATA aliwashauri wanamuziki na wasanii wengine kujiunga na Bima ya Afya

Monday, October 26, 2015

DIAMOND ATWAA TUZO YA MTVEMA


HAKIKA Diamond kiboko yao. TAMUNET inatoa hongera kwa  Diamond Platnumz kwa kushinda MTV European Music Awards (MTVEMA), katika tukio lililofanyika Milan  Jumapili hii tarehe  25 October wakati Tanzania ikipiga kura kutafuta viongozi wake wa miaka mitano ijayo. Tuzo hili hufanyika katika miji mbalimbali ya Ulaya kila mwaka, na washindi huchaguliwa kwa kura za wapenzi kutoka dunia nzima. Mcheza filamu kutoka India na ambae pia alikuwa Miss  World mwaka 2000 Priyanka Chopra pia alishiriki akiwa kundi moja na Diamond, katika ‘ category ‘ ya  Worldwide Act : "Africa/ India". Pamoja na uwingi wa watu wa India , Diamond Platnumz ameweza kupata kura nyingi zaidi na kuongeza sifa wake mwenyewe binafsi na kwa Taifa. Hongera tena Diamond
Priyanka Chopra

Saturday, October 24, 2015

Profesa Elisante Ole Gabriel ateuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete usiku wa Ijumaa, Oktoba 23, 2015, amewateua Makatibu Wakuu wanne wapya wa wizara mbali mbali. Kati Makatibu Wakuu hao Rais amemteua aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel, kuwa Katibu Mkuu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Sihaba Nkinga kuhamishiwa Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Habari. Hakika hii ni habari nzuri kwa wasanii katika kipindi hiki tunapongojea matokeo ya uchaguzi Mkuu. Profesa ni mchapa kazi wa ukweli, ni kati ya mambo mazuri makubwa yaliyotokea katika Wizara hii kwa muda mrefu

Wednesday, October 21, 2015

DOUBLE M WAKO MSUMBIJI KWA MARA YA PILI



Baada ya kazi nzuri ya awali Double M Sound chini ya Muumin Mwinyjuma imealikwa tena Msumbiji. Kwa maneno yake mwenyewe kiongozi huyu wa kundi hilo alituma ujumbe huu, “Nipo  njiani na vijana wangu tunaenda Msumbiji, tumepata mualiko  mwingine, safari hii tumealikwa na serikali kupitia Manispaa ya Mkoa Wa PEMBA, baada ya kufurahishwa na kazi yetu ya mwezi uliopita. Kuna sherehe ya Kitaifa ambayo hua inazunguka kila Mkoa na mwezi huu inafanyika ktk Mkoa Wa Mpemba, kutakua na burudani za aina nyingi  tofauti. Safari Hii tumetakiwa kuwa na idadi ya watu 14 tofauti na safari ya kwanza tulikwenda 19.
Kwenye msafara wetu tupo watu 13 na mwenzetu mmoja fundi mitambo na mpiga tumba Omar Zagalo alibaki kule na vyombo toka tulipoenda mara ya kwanza. Tulio kwenye msafara huu ni mimi Muumin Mwinyjuma, Rashid Sumuni-solo, Pascal Kinuka-bass, Issa Ramadhani-kinanda, H Waninga-drums, Amina Juma, Salehe Kupaza na  Dogo Rama waimbaji, madansa ni Verosa,Regina, Salma, Titi na Star. Tunasafiri kwa njia ya bus tukishavuka Boda saa 10 Jioni tutachukuliwa na gari lililoandaliwa na wenyeji wetu, ambayo itatumia saa 1-30 kutufikisha mji wa Msimbwe na hapo tutapanda ndege maalum itakayotupeleka Pemba. Tuombeeni Mungu tufanye vizuri zaidi kwani Show hii ni muhimu sana kujitangaza na kuutangaza muziki wa Bendi za TZ."

Tuesday, October 20, 2015

MSONDO NGOMA WAKUBALIANA KUPATA BIMA YA AFYA.

KATIKA  mkutano uliofanyika leo kwenye makao makuu ya MSONDO, wanamuziki waliweza kupata taarifa ya namna BIMA YA AFYA inavyofanya kazi. Maelezo hayo yaliyotolewa kwao na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki, (TAMUNET) John Kitime. Baada ya mkutano huo wanamuziki hao walikubaliana kuanza kuhakikisha kila mmoja wao ana Bima ya Afya mara moja


Sunday, October 11, 2015

DIAMOND AZOA TUZO TATU AFRIMMA AWARDS


diaDiamond Vannessa Mdee na Ommy Dimpoz wameweka historia kwa maisha yao, nay a muziki wa Tanzania kwa kushinda Tuzo katika Afrimma Awards 2015, zilizofanyika Dallas Marekani leo. Diamond akiwa ameshinda tuzo 3 zikiwemo Best Dance Video- Nana, Best Male Artists East Africa, na Artiste of the Year Vannesa Mdee akachukua Tuzo ya Best Female Artists East Africa. Ommy Dimpoz akishinda tuzo ya Best Newcomer> Diamond amkuwa katika tuzo jingine kutokana na wimbo alioshirikiana na Mnaijeria Tiwa Savege, hivyo kupata tuzo ya Best Inspiration Song Hongera kwa wote Best Male – East Africa
  • Eddy Kenzo (Uganda)
  • Jaguar (Kenya)
  • Diamond Platnumz (Tanzania)
  • Bebe Cool (Uganda)
  • Jackie Gosse (Ethiopia)
  • Ali Kiba (Tanzania)
  • Dynamq (Sudan)
Best Female – East Africa
  • Khadija Kopa (Tanzania)
  • Aster Aweke (Ethiopia)
  • Victoria Kimani (Kenya)
  • Vanessa Mdee (Tanzania)
  • Juliana Kanyamozi (Uganda)
  • STL (Kenya)
  • Irene Ntale (Uganda)
vannessa

 Best Newcomer
  • Kiss Daniel (Nigeria)
  • Pappy Kojo (Ghana)
  • Korede Bello (Nigeria)
  • Lil Kesh (Nigeria)
  • Mz Vee (Ghana)
  • Fabregas (Congo)
  • Ommy Dimpoz (Tanzania)
  • Bebi Philip (Ivory Coast)
  • mpata Wapi’ (Tanzania)
  • Sauti Sol – ‘Sura Yako’ (Kenya)
  • Cassper Nyovest – ‘Doc Shabaleza’ (South Africa)
  • ommy
Artist of the Year
  • Flavour (Nigeria)
  • Diamond Platnumz (Tanzania)
  • Sarkodie (Ghana)
  • Cassper Nyovest (South Africa)
  • Davido (Nigeria)
  • Fally Ipupa (Congo)
  • Eddy Kenzo (Uganda)
  • Wizkid (Nigeria)
  • Yemi Alade (Nigeria)
  • Bucie (South Africa)
Inspirational Song
  • Bracket ft. Diamond & Tiwa Savage – ‘Alive’ (Nigeria & Tanzania)
  • Irene Ntale – ‘Woman’ (Uganda)
  • Sarkodie ft. Castro – ‘Adonai’ (Ghana)
  • Jose Chameleon – ‘Bwerere’ (Uganda)
  • Psquare ft. Dave Scott – ‘Bring it On’ (Nigeria)
  • Eddy Kenzo – ‘Be Happy’ (Uganda)
 

Thursday, October 8, 2015

TAMUNET YAFANYA MKUTANO

Wa kwanza kushoto, Abraham Kapinga (Tanzanite Band) Katibu Mkuu wa Mtandao

Toka kushoto-Innocent Nganyagwa, Ally Jamwaka(Sikinde), Rashid Pembe(Mark Band), Davidi Ng'asi(Mwalimu wa muziki)

Abdul Salvador
Wanamuziki kadhaa walikusanyika jana kwenye ofisi za TAMUNET, Tanzania Musicians Network kujadili mambo kadhaa yanayohusu wanachama wa Mtandao huo. Baadhi ya mambo yalitojadiliwa ni tathmini ya wanamuziki kujiunga na Bima ya Afya, Tamasha la sanaa litakalokuweko March 2016 huko Ivory Coast, ushiriki wa Mtandao katika uboreshaji wa elimu ya muziki, na pia kuangalia nafasi ya maendeleo ya muziki katika serikali ijayo.
Ilionekana kuwa kasi ya kujiunga na bima ya afya bado ni ndogo, na moja ya sababu ni ukosefu wa uelewa kuhusu umuhimu wa Bima na namna ya utendaji wa Bima. Mikakati ilipangwa kukabili hali hiyo.
Taaarifa ya Tamasha ilikwisha anza kusambazwa kutumia mitandao ya Facebook, vikundi vya Whatsapp Blog hii na taarifa za mdomo. Tayari wasanii kadhaa walionyesha nia ya kushiriki. Mtandao uangalie namna ya kwezesha wanamuziki hawa kufanikiwa katika ushiriki wa tamasha hili.
Ilikuablika kuwa katika wiki mbili zijazo kufanyike kikao cha kuangalia utekelezaji wa kushiriki katika kuboresha elimu ya muziki. Mwanamuziki na Mwalimu wa Muziki David Ng'asi alipewa jukumu la kuja na andiko la awali la mkakati huo.

Monday, October 5, 2015

MWALIKO WA KUSHIRIKI TAMASHA LA 9 LA MASA -IVORY COAST

WANACHAMA  wa Tanzania Musicians Network (TAMUNET) mnakaribishwa kushiriki katika tamasha la 9 la MASA litakalokuwa Abidjan Ivory Coast kati ya tarehe 5-12 March 2016. Kwa maelezo zaidi wasiliana uongozi kupitia 0713274747 au 0763722557. Au wasiliana kupitia musicnettz@gmail.com

Tuesday, September 29, 2015

MWANAMUZIKI WA DOUBLE M SOUND AVAMIWA NA VIBAKA MSUMBIJI


Taarifa zimetufikia kwenye ofisi ya Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, kutoka kwa Muumin Mwinjuma 'Kocha' zikieleza kuwa mmoja wanamuziki wake aliokuwa nao katika safari ya Msumbiji amepata mkasa wa kuibiwa na kuumizwa muda mfupi kabla ya onyesho kumalizika rasmi. Kwa kadri ya maelezo ya Muumini, bendi ilipiga katika kitongoji cha Nanyupu, ambapo show hiyo ilikuwa ni ya pili katika mahala hapo baada ya bendi kufanya show ya kwanza siku ya Jumapili tarehe 20 Septemba. Kitongoji hiki ni makazi ya wachimbaji wa madini ya Ruby ambapo wengi wao ni Watanzania, pia kuna wenyeji ambao ni Wamsumbiji, Wasenegali na Wanaijeria kadhaa. Kwa kuwa Watanzania ni wengi, mara baada ya show ya kwanza, wakazi walimuomba aliyeipeleka bendi wakapige show nyingine, nae hakukataa kwani alikuwa katengeneza pesa vizuri, hivyo bendi ilikwenda kupiga tena siku ya Alhamisi tarehe 24 Septemba, siku ya Idd. Wakati wa kupiga wimbo wa mwisho, muimbaji Amina hakuwa na kazi hivyo alishauriana na madansa watangulie kwenye gari. Madansa waliondoka kwa pamoja na kuelekea kwenye gari lakini Amina ambaye pia ni katibu wa bendi alipanda kwanza jukwaani kumuaga Muumini. Aliposhuka kwenye jukwaa kuelekea kwenye gari kundi la vijana wakaanza kumsemesha Kiswahili nae akawa anajisikia kama yuko na ndugu zake. Vijana wale ghafla wakamvamia na kuanza kumpiga makofi na kumburula na kumpora mkoba wake uliokuwa na passport yake na ya mpiga drum na fedha za Msumbiji zenye thamani ya 150,000/-. Wenzie walipofika kumsaidia tayari vibaka wale walikuwa wameshaingia gizani.  Na mara moja dansi lilivunjwa ili kumpeleka mji wa Pemba kwa matibabu.
Bendi ilifanya maonyesho mengine mawili katika mji wa Pemba na kuona kuna haja ya kurudi kwanza nyumbani ili Amina apone vizuri, wakati wanamuziki wengine wanategemea kurudi nchini wakati wowote, Amina ataendelea kuwa Msumbiji kwa wiki moja zaidi ili apate matibabu zaidi. Pia bendi inakuja  kujipanga kwa safari ndefu zaidi inayotegemewa muda si mrefu.
Amina akiwa na mwanamuziki mwenzie Kupaza


Monday, September 21, 2015

DAVID NG'ASI MWANACHAMA WA MTANDAO WA WANAMUZIKI AFIWA NA BABA YAKE

MWANACHAMA WA MTANDAO WA WANAMUZIKI ambaye ni mpiga piano na mwalimu wa piano amefiwa na baba yake mzazi Mzee Aloysi Ng'asi nae alikuwa mwalimu wa muziki aliyeheshika sana katika nyanja hiyo.Mzee Ng'asi aliyezaliwa huko Iringa amezikwa Kinondoni
David akisimika msalaba kwenye kaburi la baba yake

DOUBLE M YAANZA KUTIKISA MSUMBIJI

KUNDI  la Double M chini ya Muumin Mwinyjuma, limealikwa Msumbiji kwa mwezi mzima, na katika wakati huo kundi litashiriki katika sherehe za miaka 51 ya Vita vya Ukombozi wa nchi hiyo. Wanamuziki hawa ambao ni wanachama wa Mtandao wa Wanamuziki walipitisha barua yao ya taarifa ya kwenda huko na hivyo Mtandao ukatoa taarifa Baraza la sanaa La Taifa kama inavyostahili. Waliomo katika msafara huo ni pamoja na kiongozi wa kundi Muumin Mwinyjuma,  maarufu kwa jina la KOCHA, na wanamuziki wengine 16.
1.     Mwinjuma Muumin Buguza- Kiongozi wa Bendi-Muimbaji
2.     Omary Kisila- Kinanda
3.     Hamza S Waninga- Drums
4.     Imma Keffa –Bass Guitar
5.     Emmanuel Namwinga- Rhythm guitar
6.     Amina R Juma –Muimbaji
7.     Veronica D Buzeri –Dansa
8.     Neema Kawambwa-Dansa
9.     Stamili  Hamis –Dansa
10. Greyson Semsekwa – Rapper
11. Sharey Aboubakar-Muimbaji
12. Revina Mzinja -Dansa
13.  Salma Shaaban –Dansa
14. Afande Muhamada-Fundi Mitambo
15. Omary Maulid –Fundi Mitambo
16. Saleh Kupaza-Muimbaji
17. Dogo Rama-Muimbaji











Habari toka TAMUNET- Mtandano wa Wanamuziki Tanzania

Monday, September 14, 2015

MWANAMUZIKI KUIBURUZA KAMAPUNI YA SIMU MAHAKAMANI


MWANAMUZIKI wa Abuja, nchini Nigeria Omenuwoma Okson Dovie, aka Baba 2010, ameamua kuipeleka mahakamani kampuni ya simu ya  MTN kwa kukiuka haki zake za hakimiliki katika nyimbo zake nne, zikiwemo "Gentleman "Ometena", "Twisted" and "Unity Song."
Dovie anaituhumu kampuni hiyo kwa kubadili nyimbo hizo kuwa caller tunes/ring tones, na kuziuza bila ruksa yake kwa miaka mitatu mfululizo. Nyimbo hizo ziko kwenye album yake aliyoitoa 2005 ikiwa na jina
 "Twisted”.
Barua ya mwanasheria wake Rockson Igelige, imeitaka  MTN kumlipa mteja  wake naira milioni 500 (Tshs 5,455,000,000), kwa matumizi ambayo hayakuruhusiwa na yenye kupunguza thamani ya nyimbo zake. Na pia alitoa siku 14 ambazo MTN lazima iwe imekamilisha malipo au kujibu hoja.
Mshauri wa sheria wa MTN amekubali kuwa kapokea barua na kuwa kampuni hiyo inaliangalia swala hilo. Wakati huohuo Igelige amesema wameishauri Kamisheni ya Hakimiliki ya Nigeria kuwafungulia mashtaka MTN, wakati nao wakifungua mashtaka kwa upande wa mwanamuziki.

Wednesday, September 2, 2015

WANAMUZIKI WACHANGAMKIA KUPATA BIMA YA AFYA

Hamis Mnyupe wa Msondo akijaza fomu za Bima ya Afya

Kinuka, mpiga bezi wa kujitegemea na producer akijaza fomu za Bima ya Afya

Goddy Mkude mpiga gitaa wa B Band akijaza fomu za Bima ya Afya




Geophrey Kumburu mpiga kinanda na producer akiwa na kadi yake ya Bima aliyoipata karibuni


Simon Mwamkinga mpiga kinanda na kiongozi  wa Rungwe Band akiwa na kadi yake ya Bima ya Afya aliyoipata karibuni

TAMUNET YAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA BIMA YA AFYA


Mwaka 2004, John Kitime ambaye kwa sasa ndie Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (Tanzania Musicians Network-TAMUNET) alihudhuria Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Muziki Duniani –International Federation of Musician (FIM). Katika mkutano huo moja ya maazimio ya mkutano ule ilikuwa kila nchi ihakikishe inaanzisha utaratibu wa Bima ya Afya kwa wanamuziki wake. 
Mara baada ya kurudi Tanzania, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa TAMUNET, Kitime alianza kufuatilia uwezekano wa kupata huduma ya Bima hiyo kwa wanamuziki. Kwa bahati mbaya hakukuwa na njia yenye gharama nafuu ya malipo ya BIma hiyo ambayo mwanamuziki wa kawaida angeweza kuyamudu. Kulikuweko na kampuni ambayo iliweza kutoa huduma hiyo kwa gharama ya dola 300 kwa mwaka kwa mwanamuziki mmoja. Kampuni nyingine za Bima zilizotembelewa hazikuonyesha ushirikiano katika jambo hilo. TAMUNET iliwasiliana pia na mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa katika kipindi hico mfuko ulikuwa hauna mamlaka ya kuhudumia watu waliokuwa nje ya ajira ya serikali na mashirika ya umma. TAMUNET iliwasiliana na Mganga Mkuu wa Serikali, ambaye alishauri TAMUNET kuwasiliana na NGO moja ambayo ilikuwa na makao yake makuu Sinza, na kweli NGO hiyo ilikubali kuwa ingeweza kutoa huduma ya Bima ya Afya kwa wanamuziki kwa gharama ya shilingi 3000/- tu kwa mwezi, lakini huduma hii ilikuwa ni kwa hospitali kadhaa tu jijini Dar es Salaam. Hilo nalo lilionekana ni bora kuliko kukosa kabisa, lakini muda mfupi baadae NGO hiyo ilisema haishughuliki tena na huduma hiyo bali imeelekeza nguvu zake kwa watoto wa mtaani. Hapo ilifuatia miaka kadhaa ambayo hakukuweko na njia yoyote iliyowezekana ya kupata huduma hiyo. TAMUNET ilijaribu pia kuwasiliana na mifuko mingine, lakini kila mara iligonga ukuta aidha kwa ahadi ambazo zilikuwa zikipigwa kalenda bila kutekelezwa.
Mwaka 2015 hatimae ndipo mlango umefunguka, Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa NHIF, uliitarifu TAMUNET kuwa umeanzishwa mpango wa Bima kwa Kikoa ambao ungewawezesha wanamuziki nao kupata Bima ya Afya kwa gharama nafuu. TAMUNET iliuchangamkia mpango huo kwa kuwa imekuwa ajenda ya chama hiki kwa miaka zaidi ya kumi.
Wanamuziki wanachama wa TAMUNET tayari wameanza kufaidi huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka mzima, hii ni baada ya kulipia shilingi 76,800/-. Mpango huu utaondoa aibu ya wanamuziki kuchangiwa fedha za matibabu kila wanapougua, kwani itakuwa busara kwa wapenzi na washabiki wa muziki kuchangia mwanamuziki wanaempenda apatiwe Bima ya Afya kuliko kumchangia fedha za matibabu ya muda mfupi. Baadhi ya wanamuziki ambao tayari wana bima za afya chini ya mpango huu ni Louiza Nyoni, Abdul Salvador, Rashid pembe, na wengine wengi wamekwisha anza taratibu za kupata huduma hii.
Wasanii katika semina kuhusu BIma Ya Afya iliyofanyika BASATA karibuni

Muwezeshaji Catherine kutoka Mfuko wa Taifa wa BIma ya Afya akitoa maada katika semina ya wasanii kuhusu Bima ya Afya

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makond aliyekuwa mgeni rasmi katika semina ya Bima ya Afya kwa wasanii

Mwenyekiti wa TAMUNET akipokea kadi za kwanza za Bima ya Afya za wanamuziki, katika ofisi za Mfuko wa BIma ya Afya wa Taifa.

John Kitime akiwa na kadi yake ya BIma ya Afya aliyoipata karibuni

Kadi za Bima ya Afya za wanamuziki mbalimbali



Louiza Nyoni akionyesha kadi yake mpya ya Bima ya Afya
Ushirikiano wa Mfuko wa Biam ya Afya na TAMUNET unaweka uwezekano wa mwanamuziki kuanza kuchanga hata fedha kidogokidogo ili kuweza kufikisha kiasi kinachotakiwa. Wanamuziki wanaweza kupiga simu au kutuma ujumbe kwenue simu na 0763722557 ili kupata maelezo ya namna ya kujiunga na huduma hii. Ukiwa mwanamuziki wa Hiphop, taarab, muziki asili, dansi bongofleva, huduma hii ni kwa ajili yako kumbuka WAJANJA HUJIWEKEA BIMA YA AFYA- NA WEWE NI MMOJA WA WAJANJA