Saturday, November 26, 2016

CDEA WAZINDUA MRADI WA ATAMISHI YA KAZI ZA SANAA ‘IIDEA’ KUSAIDIA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Culture and Development East Africa (CDEA) leo limezindua rasmi mradi wa Atamishi ya kazi za sanaa (IIDEA) ambapo utakuwa nguzo muhimu kwa nchi za Umoja Wa Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania na Uganda.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa Bw.Habibu Msammy aliyemwakilisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye, ameeleza kuwa sanaa ni ajira hivyo mpango huo utasaidia kuinua ajira kwa wasanii watakaofikiwa na kukuza soko la Afrika Mashariki kupitia Sanaa zao.
“Sanaa ni kazi ya kujikimu na kazi ni hutu hivyo ni wajibu wa kila msanii kujiheshimu na kufuata taratibu ili kuwa njia kwa jamii na kuheshimika zaidi hasa katika sanaa yake. Nawapongeza sana CDEA kwa mpango huu kwani utaendelea kudumisha umoja wa Afrika Mashariki, utasaidia Wasanii wetu kupanua mawazo yao zaidi na kujiongezea maarifa ya juu katika taaluma yao ya Sanaa.” Alieleza Bw. Habibu Msammy.
Pia alisisitiza kuwa mafunzo watakayoyapata wayatumie kujiimalisha kiuchumi huku akisisitiza kuwa bado wanayo nafasi ya kujifunza zaidi katika kuweza kubuni vazi la Taifa.
“Kwa kuwa mradi huu unagusa sanaa za Ubunifu wa mavazi, Urembo na filamu. Wabunifu wa Tanzania ni wasaha wa kuendelea kubuni vazi la Taifa, Wasanii wanaangaliwa na wengi hivyo kuanzia mavazi na mawazo yao ya ubunifu na tunawategemea pia katika kubuni vazi letu la Taifa” alieleza Habibu Msammy.
Mradi huo wa mwaka mmoja unatarajia kuanza kutoa mafunzo kwa wabunifu wa mavazi na urembo, Wanamuziki na wasanii wa filamu.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CDEA, Bi. Ayeta Anne Wangusa amebainisha kuwa, baada ya mwezi mmoja kuanzia sasa wataanza mchakato wa kupata washiriki ambapo wahusika watatakiwa kutuma maombi ya ushiriki baada ya kuona matangazo mbalimbali yatakayotolewa na CDEA kupitia mitandao ya kijamii na sehemu zingine za Utamaduni.
Katika uzinduzi huo, watu mbalimbali wameshiriki wakiwemo wasanii wa filamu, maigizo, wabunifu wa mavazi, wanahabari, wanamuziki na wasanii wa kazi za sanaa ikiwemo za mikono na ubunifu.
dsc_1296
Afisa wa Mradi wa IIDEA, Bi. Angela Kilusungu wa CDEA, akisoma taarifa fupi juu ya mradi huo mpya wa utakaosaidia sanaa kwa Afrika Mashariki
dsc_1306
Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya CDEA, wakiwa katika mkutano huo
dsc_1316 dsc_1333
Allen Enjewele wa CDEA akifanya mahojiano katika tukio hilo
dsc_1354
Msanii Remigius Sostenes wa CDEA akitoa burudani katika tukio hilo
dsc_1337
Mwenyekiti wa Bodi wa CDEA, Mzee Madaraka Nyerere akijadiliana jambo na Mjumbe wa bodi hiyo ambaye anatokea Burundi, Bw. Gilbert Hagabimana wakati wa uzinduzo huo.
dsc_1341
Baadhi ya wadau wa Sanaa nchini wakijadiliana katika uzinduzi huo
dsc_1342 dsc_1346
Mkurugenzi Mtendaji wa CDEA, Bi. Ayeta Anne Wangusa (kushoto) akijadiliana jambo na wadau wa sanaa
dsc_1348 dsc_1357
Msanii Nick wa Pili akielezea namna sanaa inavyohitaji ubunifu wakati wa tukio hilo
dsc_1369
Baadhi ya wadau wa sanaa na wanahabari wakipata kujadiliana jambo
dsc_1406
Wadau wa sanaa wakifuatilia makala fupi ya CDEA iliyokuwa maalum wakati wa uzinduzi huo
dsc_1408
Uzinduzi huo ukiendelea
dsc_1427
Mkurugenzi Mtendaji wa CDEA, Bi. Ayeta Anne Wangusa akielezea jambo katika tukio hilo
dsc_1433
Mwenyekiti wa Bodi wa CDEA, Mzee Madaraka Nyerere akitoa neno na kumkaribisha mgeni rasmi
dsc_1440
Mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa Bw.Habibu Msammy aliyemwakilisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akizindua rasmi mradi huo
dsc_1434
Mzee Kitime mmoja wa wadau wa Sanaa nchini akifuatilia kwa makini tukio hilo la uzinduzi
dsc_1438
Wadau wa kifuatilia uzinduzi huo
dsc_1455 dsc_1461
dsc_1471
cdea
Wajumbe wa Bodi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi mara baada ya uzinduzi wa mradi huo wa IIDEA, mapema leo Novemba 25.2016.
PICHA ZOTE NA ANDREW CHALE

Tuesday, November 22, 2016

Mkataba wa Kumkodi Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji Kwa ajili ya kurekodi

Ni jambo la kawaida kabisa kuona makubaliano makubwa katika tasnia ya muziki Tanzania yanafanywa bila mikataba bali kwa makubaliano ya mdomo. Hili ni tatizo ambalo lazima lirekebishwe, kwani linaleta hasara kubwa kwa wasanii kutokupata haki zao stahili na mara nyingine kudhulumiwa kabisa. Hivyo basi kwa kuwa mikataba ya muziki huwa na lugha ngumu ifuatayo ni mikataba mabayo imerahisishwa na UNESCO ili wanamuziki waweze kuitumia kwa marekibisho kidogo kutegemeana na hali halisi. Hii ni mifano ya mikataba ambayo hutumika dunia nzima. Usikubali kuanza kazi bila mkataba wa maandishi…. JE UNATAKIWA KUFANYA KAZI YA MUZIKI KWENYE ALBUM YA MTU MWINGINE? MKATABA HUU HAPA  
 
 Mkataba wa kumkodi Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji Kwa ajili ya kurekodi Santuri 

 Mkataba unaeleza masharti ya kumkodi mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji kwa ajili ya kurekodi santuri moja au zaidi zitakazotayarishwa kibiashara. Mkataba unaainisha wajibu wa mtayarishaji na vilevile ule wa wanamuziki na waimbaji.

 MWANAMUZIKI AU MWIMBAJI MSINDIKIZAJI MTAYARISHAJI WA SANTURI 
 KIFUNGU CHA 1 – Madhumuni.  
Mtayarishaji anamkodi mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji katika nafasi yake ya kitaalamu kurekodi santuri moja au kadhaa. Santuri zitatumiwa mojamoja au kama sehemu ya Albamu. Mkataba lazima ujazwe kikamilifu pale inapobidi, kwa kuzigatia masharti ya sheria za kazi za nchi ambazo mkataba unasainiwa. 
 KIFUNGU CHA 2 – uidhinishaji wa Matumizi. MWANAMUZIKi au MWIMBAJI MSINDIKIZAJI anaidhinisha upangiliaji wa maonesho yake na kurudufu santuri zilizoainishwa kwenye kifungu cha 1 na vile vile kufanya biashara ya santuri hizo kwa umma. Hivyo mtayarishaji atakuwa na haki ya kuzalisha, kuchapisha, kusambaza itakuvyokuwa kuuza kwenye kibebeo cha aina yoyote ( K7, CD, DVD ya sauti au muundo wowote wa siku zijazo nk ) au kwa mawasiliano ya mtandao (Intaneti na mingineyo), kutangaza katika muundo wowote, chini ya kichwa cha habari, nembo au alama ya chaguo lake na duniani kote, santuri zilizoanishwa katika kifungu cha 1. Unufaikaji wowote zaidi ya matumizi yaliyoelezwa hapo juu, yakiwamo matumizi kwa ajili ya matangazo ya biashara, matumizi ya kielimu, matumizi katika sinema au onesho, na matumizi kwenye bidhaa maalumu, yatahitaji kwanza kupata idhini ya asasi ya usimamizi wa pamoja inayosimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji. Ili kuruhusu matumizi sahihi ya haki. Mtayarishaji anawajibika kuhakikisha mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji anasaini karatasi ya kurekodi kipindi kulingana na taratibu za kitaalamu, na kuwasilisha nakala ya karatasi hii ya kurekodi kipindi kwenye asasi ya usimamizi wa pamoja ambayo inasimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji katika nchi zilizotarishwa santuri. Zaidi ya hayo msanii anaridhia matumizi ya jina na picha yake, kama vitahitajika, kuhusiana na matumizi ya santuri hizo. 
 KIFUNGU CHA 3 – Wajibu wa mtayarishaji. MTAYARISHAJI anajukumu la kuheshimu wajibu wote uliowekwa na sheria za kijamii kuhusiana na kumkodi MWANAMUZIKI au MWIMBAJI MSINDIKIZAJI. Mtayarishaji anawajibika kumlipa mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji kiasi cha _____________________ kwa kila kipindi cha kurekodi, ili kufidia kushiriki kwake katika kurekodi santuri, na vilevile kwa ajili ya uchapishaji na mauzo ya miziki kwenye aina yoyote ya kibebeo (K7, CD, DVD ya sauti n.k) au katika mawasiliano ya mitandao (Intaneti au mingineyo). Upigaji wa santuri katika utangazaji utatakiwa kuliipiwa moja kwa moja na mashirika ya utangazaji kwenye asasi ya usimamizi wa pamoja ambayo inasimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji katika nchi matangazo yanamotolewa. 
 KIFUNGU CHA 4 – wajibu wa Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji. 
Mwanamuziki kutoka nje au mwimbaji msindikizaji kutoka nje ya nchi anahakikisha kuwa amepewa kibali cha kufanya kazi kwenye nchi santuri zinapotayarishwa na kuwasilisha uthibitisho wa jambo hilo. Mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji anawajibika kuwepo kuanzia ___________________ hadi
___________________katika sehemu ifuatayo _____________________ kushiliki katika vipindi vya kurekodi ambavyo vitafanyika kulingana na ratiba zifuatazo:- ______________________________________________________________________________ Kifungu cha 5 – mambo mbalimbali  
Mkataba huu unaongozwa na sheria ya nchi unamofanyika utayarishaji. 
Umesainiwa (mji)…………………………………….. Tarehe ……………….. Katika ……………… nakala halisi. 
 MWANAMUZIKI AU MWIMBAJI MSINDIKIZAJI ________________________________________________________________________   MTAYARISHAJI ________________________________________________________________________  

Tuesday, November 8, 2016

PUMZIKA KWA AMANI SAMWEL JOHN SITTA

Mzee Samwel John Sitta alikuwa rafiki mkubwa wa wasanii na jambo ambalo wengi hawalijui ni kuwa pia alikuwa msanii mpiga gitaa. Mwalimu wa Mzee Sitta ambaye nae ni marehemu Mzee Brown Swebe aliwahi kusema kuwa alimfundisha gitaa Mzee Samweli Sitta wakati yuko shule ya sekondari Tabora, na alifanya hivyo kwa malipo ya kulima matuta kadhaa ya viazi. Wakati wote alikuwa kigusia umuhimu wa Hakimiliki na hata wakati akiwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba aliwezesha wasanii kukutana na wajumbe wengi wa Bunge la katiba kuweza kujielezea kuhusu umuhimu wa ulinzi wa mali isiyoshikika kutajwa katika katiba.





Tutakukumbuka daima Mzee Samwel  John Sitta

Friday, October 21, 2016

MZEE KUNGUBAYA AZIKWA NA WENGI

MWANAMUZIKI mkongwe ambaye alipata umaarufu kutokana na wimbo wake Salam za Wagonjwa amezikwa leo katika makaburi ya kifamilia Njeteni Kwembe. Msiba huo ulihudhuria na watu wengi wakiwemo majirani, ndugu, wanamuziki na wapenzi wa muziki wa Mzee Kungubaya.Tatu itakuwa siku ya Jumamosi 22/10/2016.
Jeneza likiwa nje ya nyumba ya marehemu

Mwanamuziki Mjusi Shemboza akiongea na mmoja wa watoto wa marehemu Mzee Kungubaya




Mjusi Shemboza akiwa na Mtendaji Mkuu wa COSOTA wa zamani Mzee Mtetewaunga

Msafara wa kuelekea makaburini



Mazishi ya Mzee Kungubaya

Thursday, October 20, 2016

MZEE OMARI KUNGUBAYA HATUNAE TENA

kungubaya
Mzee Omari Kungubaya akipiga gitaa siku ya mkesha wa msiba wa Dr. Remmy Ongala
MZEE Omari Kungubaya ambaye atakumbukwa kwa wimbo wake Salam za wagonjwa, wimbo uliokuwa ukiashiria kuanza na kuisha kwa kipindi cha salamu za wagonjwa kupitia Radio Tanzania kwa miaka mingi amefariki leo mchana baada ya afya yake kuwa si nzuri kwa muda mrefu. Msiba wake uko nyumbani kwake Njeteni, Mbezi ya Kimara Habari zaidi tutawaleteeni Mungu amlaze pema peponi

Thursday, October 13, 2016

NGUZA VIKING, PAPII KOCHA NA TWANGA PEPETA JUKWAA LA TAMASHA LA WAFUNGWA


Bendi ya African Stars, maarufu kwa jina la Twanga Pepeta kesho itashiriki katika Tamasha la Wafungwa ambalo litaanza saa 2 asubuhi. Katika mambo ambayo yatakuwa makubwa kimuziki ni kushiriki kwa mwanamuziki mkongwe  Nguza Viking na mwanae Papii Kocha ambao kwa sasa wanatumikia kifungo cha maish katika gereza la Ukonga. Pia katika tamasha hilo atakuweko msanii nyita wa muziki wa Singeli Msaga Sumu. Lengo la tamasha hilo ni kuwatia moyo wafungwa na kuwaonyesha kuwa wapo pamoja na Watanzania wenzao walio nje ya magereza. Eric Shigongo Mkurugenzi mkuu wa Global Publishersambao ndio walioandaa tamasha amesema hii ni mara ya pili kuandaa tamasha la namna hii, ambalo lengo ni kunyanyua ari ya wafungwa. Wafungwa waliohudhuria tamasha lililopita ambao walikwisha maliza kifungo wamesifu na kusema tamasha lililopita liliwapa faraja sana. Mratibu wa tamasha hilo Juma Mbizo, amesema mbali na burudani kali kutoka kwa Twanga, kutakuwepo na michezo mbalimbali kama ya mpira wa miguu, kuvuta kamba na mingineyo ambapo zawadi mbalimbali zitatolewa kwa washindi.  Pamoja na maneno mazuri ya kutia moyo yatakayotolewa na Eric Shigongo, Mkuu wa Gereza la Ukonga, ACP Stephen Mwaisabila naye anatarajiwa kutoa neno katika tamasha hilo sanjari na viongozi wengine wa Jeshi la Magereza.

Saturday, October 8, 2016

RATIBA YA MSIBA WA MAREHEMU SALOME KIWAYA


Taarifa ya ratiba ya msiba wa marehemu Salome Kiwaya aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma na mwanamuziki, aliyefariki jana 07/10/2016, kwa ajali ya gari maeneo ya Kilimo Kwanza Dodoma Mjini. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Image, Kata ya Kilimani, Wilaya ya Dodoma Mjini. RATIBA:
 1.Tarehe 08/10/2016 - maombolezo  yanaendelea nyumbani Image Kilimani Dodoma.
2.Tarehe 09/10/2016 kuanzia saa 2:00 asubuhi - mwili wa marehemu utaletwa nyumbani kutoka  chumba cha maiti cha General Hospital Dodoma.
3. Tarehe 09/10/2016 saa kuanzia 6:00 mchana -salamu mbalimbali za Viongozi na Makundi Maalumu zitaanza kutolewa.
Saa 8: 00 mchana- mwili wa marehemu utatolewa nyumbani, na kuelekea Kanisa Kuu Roman Catholic. Baada ya Misa, msafara wa mwili wa marehemu utaelekea Kijiji cha Mtila, Kata ya Matola Mkoa wa Njombe kwa ajili ya maziko tarehe 10/10/2016 siku ya Jumatatu.


Friday, October 7, 2016

RIP SALOME KIWAYA


Picha iliyopigwa Uingereza wakati Salome alipoenda huko na Shikamoo Jazz Band. Toka Kushoto Marehemu Salome Kiwaya, Marehemu Papa Wemba, na Marehemu Bi Kidude Mungu awalaze pema.
Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa za msiba wa Mama Salome Kiwaya, mwanamuziki mkongwe. Taarifa zilinifikia kuwa Salome amefariki katika ajali ya gari iliyotokea Dodoma sehemu za Meriwa. Nilimfahamu Salome kwa mara ya kwanza mwaka 1987, wakati nikiwa bendi ya Tancut Almasi Orchestra, tulipopiga kambi Dodoma Hotel kwa muda wa miezi mitatu, tukitoa burudani kwanza kwa wajumbe wa mkutano wa Kizota, kisha wenyeji wa mji wa Dodoma. Katika kufahamiana  kipindi hicho, tuliweza hata  kupiga wimbo wake mmoja ulioitwa Tuhina, uliokuwa ukiimbwa na Kasaloo Kyanga na Kyanga Songa, ambao nao ni marehemu. Siku moja nilipita mtaani Dodoma na kununua kanda za muziki wa Salome, nilizipenda sana nyimbo zake na nikamuahidi kuwa ningejitahidi kuzipeleka kwa watu wenye uwezo wa kuendeleza kazi zile. Nilizipeleka kanda kwa Ronnie Graham, Mscotch mmoja mwenye upenzi na uelewa mkubwa wa muziki wa Kiafrika na hasa rumba, na huyu Mscotch ndie aliyewezesha kuanzishwa kwa bendi ya Shikamoo Jazz Band. Baada ya kuzisikia nyimbo zile akaamua kuwa Salome asindikizane na bendi ya Shikamoo kwenye ziara yao ya Uingereza kama muimbaji wa kike. Salome alienda Uingereza na aliporudi ndipo alipoanza kununa vyombo na kuunda kundi la Saki Stars, ikiwa ni kifupi cha Salome Kiwaya Stars. Mume wake Mzee Kiwaya nae ni msanii maarufu aliyekuwa kiongozi wa kikundi cha Utamaduni cha CDA miaka hiyo ya 80. Kuanzia hapo nimekuwa karibu sana na Salome, miaka ya 90 wakati nikiwa Mwenyekiti wa CHAMUDATA, Salome ndie alikuwa mwenyekiti wa chama hicho katika mkoa wa Dodoma baada ya mkutano mkubwa wa wanamuziki uliofanyika mwezi June 1998, kule Bagamoyo, ambapo wanamuziki 265 waliweza kukusanyika pamoja na kukaa siku nne katika mji wa Bagamoyo wakifanya warsha za fani mbalimbali za muziki. Katika miaka ya karibuni Salome alishughulika na sanaa ya urembo akiwa wakala wa Miss Tanzania kwa kanda ya Kati na kuweza kutoa MIss Tanzania mmoja, baadae aliingia katika siasa na kufikia kuwa Mwenyekiti wa UWT wa Mkoa wa Dodoma, lakini aliendelea na muziki katika maisha yake yote.

Mungu Amlaze Pema Salome Kwaya. Ucheshi wako hatutausahau. 
JOHN KITIME

Saturday, March 19, 2016

DKT AYUB RIOBA CHACHA MKURUGENZI MKUU MPYA TBC

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AMEMTEUA DKT AYUB RIOBA CHACHA KUWA MKURUGENZI MPYA WA TBC. DKT RIOBA ANACHUKUA NAFASI YA CLEMENT MSHANA ALIYESTAAFU.

WAZIRI NAPE NNAUYE KUKUTANA NA WANAMUZIKI JUMATATU 21 MARCH 2016

12347733_1139421576075747_4085232307530687920_nKATIKA hatua ya kujua mafanikio na changamoto za muziki wa dansi na hatimae kupanga yajayo, Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo atakutana na wanamuziki wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni siku ya Jumatatu kuanzia saa nne asubuhi. Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka mingi kwa Waziri wa Utamaduni kufanya mkutano wa namna hii na wanamuziki.

Sunday, February 21, 2016

LEO NDIO SIKU YA MAZISHI YA RAFIKI YETU NA NDUGU YETU FRED CAMILLIUS MOSHA



FRED
RIP FRED MOSHA
  LEO NDIO SIKU YA MAZISHI YA RAFIKI YETU NA NDUGU YETU FRED CAMILLIUS MOSHA. FRED ALIKUWA MTANGAZAJI ALIYEKUWA NA MAPENZI MAKUBWA NA MUZIKI WA DANSI. MAPENZI YAKE YALIANZA TOKA AKIWA MDOGO KWANI NAMKUMBUKA AKIJA NA MAMA YAKE KATIKA MADANSI YA MCHANA AMBAYO BENDI YETU YA TANCUT ALMASI ILIKUWA IKIPIGA KWENYE UKUMBI WA OMAX KEKO. UPENZI HUU ULIFIKIA MPAKA KIPINDI ALITAKA KUACHA SHULE NA KUJIUNGA NA BENDI YA DDC MLIMANI PARK, BAHATI NZURI MAMA YAKE ALIIKAMATA BARUA YA MAOMBI YAKE YA KAZI, NA KUZUIA MPANGO HUO WA KUACHA SHULE. FRED HAKIKA ALIKUWA MTANGAZAJI BORA WA HABARI ZA WANAMUZIKI WA MUZIKI WA ZAMANI WA DANSI.
RATIBA YA MAZISHI NI KAMA IFUATAYO;
  • SAA 4-5 MWILI UTAPELEKWA NYUMBANI KWAKE CHAMAZI UKITOKEA MUHIMBILI
  • SAA 7 MWILI KUPELEKWA KANISA LA RC CHANG'OMBE KWA MISA YA MAZISHI
  • BAADA YA HAPO SAFARI ITAANZA YA KUELEKEA MAKABURI YA KINONDONI KWENYE MAKAZI YAKE YA MILELE
  • MUNGU MALAZE PEMA PEPONI FRED MOSHA

Tuesday, January 19, 2016

SIZONJE -KIBAO KIPYA CHA MRISHO MPOTO AKISHIRIKIANA NA BANANA ZOLLO

Mrisho Mpoto- mjomba amekuja na kibao kipya kabisa Sizonje, kibao ambacho kamshirikisha mwanamuziki Banana Zollo, kisikie hapa