Monday, September 21, 2015

DOUBLE M YAANZA KUTIKISA MSUMBIJI

KUNDI  la Double M chini ya Muumin Mwinyjuma, limealikwa Msumbiji kwa mwezi mzima, na katika wakati huo kundi litashiriki katika sherehe za miaka 51 ya Vita vya Ukombozi wa nchi hiyo. Wanamuziki hawa ambao ni wanachama wa Mtandao wa Wanamuziki walipitisha barua yao ya taarifa ya kwenda huko na hivyo Mtandao ukatoa taarifa Baraza la sanaa La Taifa kama inavyostahili. Waliomo katika msafara huo ni pamoja na kiongozi wa kundi Muumin Mwinyjuma,  maarufu kwa jina la KOCHA, na wanamuziki wengine 16.
1.     Mwinjuma Muumin Buguza- Kiongozi wa Bendi-Muimbaji
2.     Omary Kisila- Kinanda
3.     Hamza S Waninga- Drums
4.     Imma Keffa –Bass Guitar
5.     Emmanuel Namwinga- Rhythm guitar
6.     Amina R Juma –Muimbaji
7.     Veronica D Buzeri –Dansa
8.     Neema Kawambwa-Dansa
9.     Stamili  Hamis –Dansa
10. Greyson Semsekwa – Rapper
11. Sharey Aboubakar-Muimbaji
12. Revina Mzinja -Dansa
13.  Salma Shaaban –Dansa
14. Afande Muhamada-Fundi Mitambo
15. Omary Maulid –Fundi Mitambo
16. Saleh Kupaza-Muimbaji
17. Dogo Rama-Muimbaji











Habari toka TAMUNET- Mtandano wa Wanamuziki Tanzania

Monday, September 14, 2015

MWANAMUZIKI KUIBURUZA KAMAPUNI YA SIMU MAHAKAMANI


MWANAMUZIKI wa Abuja, nchini Nigeria Omenuwoma Okson Dovie, aka Baba 2010, ameamua kuipeleka mahakamani kampuni ya simu ya  MTN kwa kukiuka haki zake za hakimiliki katika nyimbo zake nne, zikiwemo "Gentleman "Ometena", "Twisted" and "Unity Song."
Dovie anaituhumu kampuni hiyo kwa kubadili nyimbo hizo kuwa caller tunes/ring tones, na kuziuza bila ruksa yake kwa miaka mitatu mfululizo. Nyimbo hizo ziko kwenye album yake aliyoitoa 2005 ikiwa na jina
 "Twisted”.
Barua ya mwanasheria wake Rockson Igelige, imeitaka  MTN kumlipa mteja  wake naira milioni 500 (Tshs 5,455,000,000), kwa matumizi ambayo hayakuruhusiwa na yenye kupunguza thamani ya nyimbo zake. Na pia alitoa siku 14 ambazo MTN lazima iwe imekamilisha malipo au kujibu hoja.
Mshauri wa sheria wa MTN amekubali kuwa kapokea barua na kuwa kampuni hiyo inaliangalia swala hilo. Wakati huohuo Igelige amesema wameishauri Kamisheni ya Hakimiliki ya Nigeria kuwafungulia mashtaka MTN, wakati nao wakifungua mashtaka kwa upande wa mwanamuziki.

Wednesday, September 2, 2015

WANAMUZIKI WACHANGAMKIA KUPATA BIMA YA AFYA

Hamis Mnyupe wa Msondo akijaza fomu za Bima ya Afya

Kinuka, mpiga bezi wa kujitegemea na producer akijaza fomu za Bima ya Afya

Goddy Mkude mpiga gitaa wa B Band akijaza fomu za Bima ya Afya




Geophrey Kumburu mpiga kinanda na producer akiwa na kadi yake ya Bima aliyoipata karibuni


Simon Mwamkinga mpiga kinanda na kiongozi  wa Rungwe Band akiwa na kadi yake ya Bima ya Afya aliyoipata karibuni

TAMUNET YAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA BIMA YA AFYA


Mwaka 2004, John Kitime ambaye kwa sasa ndie Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (Tanzania Musicians Network-TAMUNET) alihudhuria Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Muziki Duniani –International Federation of Musician (FIM). Katika mkutano huo moja ya maazimio ya mkutano ule ilikuwa kila nchi ihakikishe inaanzisha utaratibu wa Bima ya Afya kwa wanamuziki wake. 
Mara baada ya kurudi Tanzania, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa TAMUNET, Kitime alianza kufuatilia uwezekano wa kupata huduma ya Bima hiyo kwa wanamuziki. Kwa bahati mbaya hakukuwa na njia yenye gharama nafuu ya malipo ya BIma hiyo ambayo mwanamuziki wa kawaida angeweza kuyamudu. Kulikuweko na kampuni ambayo iliweza kutoa huduma hiyo kwa gharama ya dola 300 kwa mwaka kwa mwanamuziki mmoja. Kampuni nyingine za Bima zilizotembelewa hazikuonyesha ushirikiano katika jambo hilo. TAMUNET iliwasiliana pia na mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa katika kipindi hico mfuko ulikuwa hauna mamlaka ya kuhudumia watu waliokuwa nje ya ajira ya serikali na mashirika ya umma. TAMUNET iliwasiliana na Mganga Mkuu wa Serikali, ambaye alishauri TAMUNET kuwasiliana na NGO moja ambayo ilikuwa na makao yake makuu Sinza, na kweli NGO hiyo ilikubali kuwa ingeweza kutoa huduma ya Bima ya Afya kwa wanamuziki kwa gharama ya shilingi 3000/- tu kwa mwezi, lakini huduma hii ilikuwa ni kwa hospitali kadhaa tu jijini Dar es Salaam. Hilo nalo lilionekana ni bora kuliko kukosa kabisa, lakini muda mfupi baadae NGO hiyo ilisema haishughuliki tena na huduma hiyo bali imeelekeza nguvu zake kwa watoto wa mtaani. Hapo ilifuatia miaka kadhaa ambayo hakukuweko na njia yoyote iliyowezekana ya kupata huduma hiyo. TAMUNET ilijaribu pia kuwasiliana na mifuko mingine, lakini kila mara iligonga ukuta aidha kwa ahadi ambazo zilikuwa zikipigwa kalenda bila kutekelezwa.
Mwaka 2015 hatimae ndipo mlango umefunguka, Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa NHIF, uliitarifu TAMUNET kuwa umeanzishwa mpango wa Bima kwa Kikoa ambao ungewawezesha wanamuziki nao kupata Bima ya Afya kwa gharama nafuu. TAMUNET iliuchangamkia mpango huo kwa kuwa imekuwa ajenda ya chama hiki kwa miaka zaidi ya kumi.
Wanamuziki wanachama wa TAMUNET tayari wameanza kufaidi huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka mzima, hii ni baada ya kulipia shilingi 76,800/-. Mpango huu utaondoa aibu ya wanamuziki kuchangiwa fedha za matibabu kila wanapougua, kwani itakuwa busara kwa wapenzi na washabiki wa muziki kuchangia mwanamuziki wanaempenda apatiwe Bima ya Afya kuliko kumchangia fedha za matibabu ya muda mfupi. Baadhi ya wanamuziki ambao tayari wana bima za afya chini ya mpango huu ni Louiza Nyoni, Abdul Salvador, Rashid pembe, na wengine wengi wamekwisha anza taratibu za kupata huduma hii.
Wasanii katika semina kuhusu BIma Ya Afya iliyofanyika BASATA karibuni

Muwezeshaji Catherine kutoka Mfuko wa Taifa wa BIma ya Afya akitoa maada katika semina ya wasanii kuhusu Bima ya Afya

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makond aliyekuwa mgeni rasmi katika semina ya Bima ya Afya kwa wasanii

Mwenyekiti wa TAMUNET akipokea kadi za kwanza za Bima ya Afya za wanamuziki, katika ofisi za Mfuko wa BIma ya Afya wa Taifa.

John Kitime akiwa na kadi yake ya BIma ya Afya aliyoipata karibuni

Kadi za Bima ya Afya za wanamuziki mbalimbali



Louiza Nyoni akionyesha kadi yake mpya ya Bima ya Afya
Ushirikiano wa Mfuko wa Biam ya Afya na TAMUNET unaweka uwezekano wa mwanamuziki kuanza kuchanga hata fedha kidogokidogo ili kuweza kufikisha kiasi kinachotakiwa. Wanamuziki wanaweza kupiga simu au kutuma ujumbe kwenue simu na 0763722557 ili kupata maelezo ya namna ya kujiunga na huduma hii. Ukiwa mwanamuziki wa Hiphop, taarab, muziki asili, dansi bongofleva, huduma hii ni kwa ajili yako kumbuka WAJANJA HUJIWEKEA BIMA YA AFYA- NA WEWE NI MMOJA WA WAJANJA

Thursday, May 21, 2015

VANESSA MDEE AFIWA NA DADAKE MKUBWA

Muimbaji mahiri Vanessa Mdee amefiwa na dada yake mkubwa Anna Mdee, ambaye amefariki katika hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam,  jana Jumatano alfajiri. Anna ambaye alikuwa mfanya kazi wa kampuni ya sigara ya TCC na alikuwa katika kituo cha Dodoma kwa muda mrefu alikuwa India akipatiwa matibabu.
Anna na Vanessa ni watoto wa marehemu Sammy Mdee, aliyekuwa mwandishi mkongwe aliyewahi kuongoza gazeti la Daily News, Katibu wa Mwalimu Nyerere na pia mkurugenzi wa kituo cha AICC. Mazishi ya Anna yatakuwa Same Jumamosi mchan saa 8.
Mungu Amlaze Pema Anna Mdee

Wednesday, April 29, 2015

MTANDAO WA WANAMUZIKI WAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA HUDUMA YA BIMA YA AFYA

Wanamuziki wanachama wa Tanzania Musicians Network -TAMUNET_ sasa wanaweza kujiunga na mpango nafuu wa Bima ya Afya baada ya chama chao kuingia katika makubaliano na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF.
WAnamuziki walikuwa ni kundi mojawapo ambalo limekuwa na tatizo kubwa la kupata matibabu bora kutokana na kukosa taratibu za bima ya afya, jambo ambalo ni njia ya kisasa na ya uhakika wa kupata matibabu bora kwa kila binadamu.
Katika kikao cha viongozi wa chama hicho leo kamati maalumu imeundwa kuratibu mpango huu ambapo kamati hii itakuwa ikiandikisha wanachama wote wanaohitaji kupata huduma hii muhimu. Kamati itakuwepo kila Jumatano kuanzaia saa nne mpaka saa tisa katika ofisi za Mtandao zilizopo katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa jirani na hospitali ya Mvungi katika barabara ya kuelekea mahakama ya Kinondoni, chumba namba 148. Pia unaweza kuwasiliana na Mweka hazina Asha Salvador kupitia simu namba 0687378797 kwa maelezo ya ziada

Friday, August 29, 2014

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI YA WASANII KATIKA BUNGE LA KATIBA...........











MTANDAO WA MUZIKI WASHIRIKI SAFARI YA KUTEMBELEA BUNGE LA KATIBA DODOMA




Hii ndio PRESS RELEASE  iliyosomwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki siku ya  27 August 2014 kwa waandishi wa habari jijini Dodoma. Ndugu waandishi wa habari, katika mfumo wa sanaa wa nchi yetu wasanii wamegawanyika katika makundi makuu manne, ambayo yanaendeshwa na Mashirikisho ya vyama mbalimbali vya sanaa. Mashirikisho hayo ni;
i.                Shirikisho la Filamu TAFF
ii.              Shirikisho la Sanaa za Maonyesho
iii.             Shirikisho la Sanaa za Ufundi
iv.             Shirikisho la Muziki
 Tuliopo mbele yenu ni viongozi na wasanii kutoka vyama na Mashirikisho ya sanaa yaliyotajwa hapo juu. Kundi hili limekuwepo hapa Dodoma kwa siku mbili kukutana na wajumbe wa Bunge la katiba ili kufuatilia maslahi ya wasanii katika katika mchakato wa  Katiba mpya ya nchi yetu Tanzania.  Hii si mara ya kwanza kwa kundi hili kukutana na Wabunge wa Bunge hili la Katiba, bali hii ni mara ya tatu kundi hili limefika hapa Dodoma. Mchakato uliotufikisha leo hapa ulianza kwa Mashirikisho kukutana na kutengeneza Baraza la katiba ambapo mashirikisho yalitoa mapendekezo kadhaa yaliyofikishwa kwenye Tume ya Katiba. Lakini hakukuweko jambo lolote lililotokana na mawazo hayo ambalo lilichukuliwa na kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba. Mashirikisho yalituma majina 36, (tisa kutoka kila shirikisho)  katika kupendekeza wawakilishi katika Bunge la Katiba. Katika hili mjumbe mmoja, Paulynus Raymond Mtenda aliteuliwa na hivyo kubeba uwakilish wa kundi zima la wasanii Tanzania. Siku ya Ijumaa 14/2/2014 Mashirikisho yote ya sanaa yalikutana BASATA na kumkabidhi rasmi mapendekezo yao Mbunge huyu, ili ahakikishe kundi hili haliachwi katika mchakato wa Katiba.
Muda mfupi baada ya hapo kundi hili lilikuja Dodoma, na kukutana na Wabunge mbalimbali wa Bunge hili la Katiba, tulikutana na Wabunge wa kambi zote na kufanya nao mikutano mingi, ambayo mingine ilifika mpaka saa nane za usiku. Wabunge wa kambi zote walionekana kuunga mkono hoja za wasanii na tulianza mawasiliano mbalimbali na Wabunge yakiwemo ya ana kwa ana, simu na email, Wabunge wakihitaji documentation mbalimbali kuhusiana na mapendekezo yetu katika Katiba mpya.  Katika kipindi hiki tulikuja wakati hata Mwenyekiti wa Bunde la Katiba hajachaguliwa. Ujumbe huu ulikuja tena …. Na hii ni mara ya tatu.
Ujumbe huu toka awali ulikuwa na maombi mawili tu.
i.                Wasanii kutambuliwa kama kundi maalumu kama yalivyotambuliwa makundi ya wakulima wafugaji, wavuvi. Sababu za kutaka kutambuliwa huku, ni kuwa kundi hili ni kubwa kuliko hata makundi mengine yaliyotajwa hapo juu. Takwimu za Baraza la Sanaa la Taifa za mwaka 2006 zinaonyesha kuwa wasanii nchini walikuwa kiasi cha milioni 6. Leo ni mika minane imepita na si siri kuwa kundi hili limekuwa na hivyo kukaribia robo ya Watanzania, si haki kutolitambua.
ii.              Milikibunifu (Intellectual Property) itajwa rasmi kama moja ya aina za mali zinazohitaji kulindwa katika katika Katiba
Tumekuja pia na mapendekezo ya namna ya kuingiza hoja zetu hizi zilizosahauliwa, hatujaja na  Ibara mpya kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyoonekana kutuhumu katika magazeti ya juzi. Mapendekezo yetu ni kuwa katika Ibara ya 30 iongezwe  aya moja tu ya. Na ibara ya 37 inayoongelea Haki ya ulinzi wa mali, itambue kuwa pamoja na mali zinazohamishika na zisizohamishika, pia kuna mali isiyoshikika.
Tumepata faraja kubwa kupokelewa na Bunge hili,  Na kuweza kuzunguka kwenye kamati 9 kwa hizi siku mbili kukumbusha mapendekezo yetu haya, ambayo hayabebi tu wasanii bali pia wavumbuzi wa kiteknolojia, kibailojia, wasomi watafiti, na wananchi wote kwa ujumla. Pendekezo letu la pili ni muhimu katika kulinda na kuendeleza uchumi wa Tanzania. Na sisi kama Watanzania tumeona ni muhimu kutumia nafasi hii adimu kuhakikisha tunatoa mawazo yetu katika Bunge hili kwani tusipotumia nafasi hii tutakuwa hatukujitendea haki wala kuvitendea haki vizazi vijavyo vya Tanzania.


SIMON MWAKIFWAMBA-SHIRIKISHOLA FILAMU TANZANIA (TAFF)


JOHN KITIME….MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA (TAMUNET)

Saturday, August 16, 2014

UMUHIMU WA MILIKIBUNIFU KUTAJWA KATIKA KATIBA MPYA

Katika Rasimu ya Katiba kumetajwa ulinzi wa mali, lakini ni wazi mali hizi ni zile zililzozoeleka katika akili za watu mali zinazohamishika na zisizohamishika. Kuna aina ya tatu ya mali ni ile inayotokana na ubunifu, na kwa sasa ndio mali inayolindwa zaidi na mataifa mengi, kwani ndio inayoleta ugunduzi wa madawa, mitambo, teknolojia, sanaa, na maendeleo ya kila aina. Hii huitwa Milikibunifu. Ni muhimu kutajwa kama zilivyofanya nchi nyingine ambazo zimefaidika sana na kulinda milikibunifu za wananchi wake.....
Milikibunifu au Intellectual Property Rights ni haki anazopewa mbunifu ili kulinda hali za mali yake ambayo haishikiki. Mali hii iyokanayo na ubunifu ni muhimu kuilinda kwani matokeo ya mali hii huwa faida kubwa kwa jamii. Milikibunifu ndizo haki ambazo huwalinda wagunduzi wa maendeleo katika teknolojia, madawa ya binadamu mifugo na kilimo, njia mbalimbali za kuongeza ubora na ufanisi wa teknolojia. Milikibunifu imegawanywa katika makundi mbalimbali ya ulinzi;
i.                Patent – (Hataza) hii ni njia ya kulinda na kusajili uvumbuzi mbalimbali wa kiteknolojia. Mfano vifaa vya kuvunia mazao kwa haraka zaidi, au kulima kwa haraka zaidi, vifaa vya uvuvi wa haraka, vifaa vya mawasiliano na vifaa vyovyote ambavyo vitaongeza thamani ya maisha yetu. Katika nchi kama Korea ya Kusini ulinzi wa Milikibunifu uliwekwa katika Katiba kuanzia baada ya vita ya pili ya dunia kwa kufusts mfumo wa  Katiba ya Marekani na ulinzi huo umeifanya wananchi wake ambao ni wabunifu kuweza kuja naubunifu ambao unatikisa dunia vifaa kama Samsung, Daewoo, KIA, LG ni matokeo ya ulinzi wa kikatiba wa wa Milikibunifu
ii.              Trademarks – (Alama za Biashara ) Alama za biashara huweza kufikia hatua ambapo zikawa na thamani kubwa kwani huweza kuaminika. Ili kulinda zisitumiwe hovyo au hata kuibiwa na wenye uwezo zaidi hulindwa na sheria za kulinda alama hizi. Kwa mfano Cocacola, Vodacom, Dell, na hapa kwetu Azam, ni majina ya bidhaa ambazo zina aminika, na hivyo kuwa na dhamani kubwa japo hazishikiki, nazo ni sehemu ya mali  ambazo hazishikiki lakini zina thamani kubwa
iii.             Industrial designs – Hizi ni haki wanazopewa wale wenye ubunifu wa kuweza kufanya usanii wenye kuboresha muonekano wa kitu ambacho tayari kimeshagunduliwa. Kwa mfano kila mtu ana simu ya mkononi lakini muonekano wa simu mbalimbali shape nap engine hali ya kuwa ni ya ku slide au kufungua au kupokea moja kwa moja ni matokeo ya design, pia vitu kama design za nguo, viatu , kiti ulichokalia makochi magari, vyote hivyo ndivyo matokeo ya industrial designs. Kazi za ubunifu huo ni muhimu kulindwa kwani huwa na thamani kubwa sana, kwa mbunifu na kwa mchango wake kwa nchi.  
iv.             Geographical Indication – Huu ni utambulisho wa wapi chanzo cha mali husika. Kwa mfano mvinyo kutoka Dodoma, Dodoma Wine ni mzuri na hivyo huitwa Dodoma Wine bila kulinda hili, watu watachukua mvinyo huu na kuupa hata jina jingine ukaitwa South African wine na hivyo kuiba haki wanazostaili kupata wakulima wa Dodoma, kutambuliwa kwa jina hili kutasababisha kutakiwa zaidi kwa wine hii duniani na hivyo kuweza kufanya hata Dodoma kuwa Wine City jambo ambalo linawezekana lakini nchi haijatambua umuhimu huu. Pia kuna mchele wa Kyela, Dagaa wa Kigoma na vitu kama hivi ambavyo havipatikani popote duniani kasoro sehemu iliyotajwa.  Nchi kama Uswiss imejenga jina miaka mingi ya utengenezaji wa saa bora hivyo saa ikiandikwa Swiss made huwa inajulikana ni bora na huwa gharama zaidi, Sigara kutoka Cuba, Cuban Cigars ni bei kubwa kwani hazipatikani popote kasoro Cuba, au mvinyo maarufu kama Champagne, ambao hutoka jimbo la Champagne Ufaransa, umejijengea sifa kubwa duniani na kuwa na bei kubwa sana kiasi cha kwamba si rahisi kwa mtu wa kipato cha kawaida kununua. Harusi zetu hutumia Sparkling Wine na kuiita Shampeni.
v.              Hakimiliki na Hakishiriki – Hizi ni haki zinazolinda kazi za kisayansi na kisanii. Computer Programs, Data, Utunzi wa vitabu, miswaada, hotuba, uchoraji, muziki, kazi za usonara, picha za mnato na filamu, uchongaji na kadhalika. Kazi hizi zimekuwa ni chanzo cha utajiri mkubwa kwa watu binafsi na Mataifa. Katika nchi ya Marekani kazi za Hakimiliki na Hakishiriki ni za pili katika uchangiaji wa pato la Taifa. Ripoti ya WIPO ya 2010 ilionyesha kuwa katika nchi ya Tanzania kazi za hakimiliki na Hakishiriki zilichangia asilimia 4.3 ya pato la taifa, karibu mara mbili ya mchango wa Madini!. Katika mwaka 2009 kazi za hakimiliki zilitengenza aslimia 5.63 ya ajira nchini, ikiwa juu ya mchango wa Afya (4.23), Biashara na mambo ya Fedha Real estate, &Business Service(2.37), Ujenzi (1.38),Usafirishaji na Mawasiliano (0.92), Umeme, Gas na maji (0.91), Madini (0.89)
Pamoja na umuhimu huu, Katiba inataja mali zinazoshikika tu-Zinazohamishika na zisizohamishika, hivyo mali hizi ambazo zimeonyesha kuleta maendeleo makubwa kwa nchi ambazo wakati wa Uhuru tulikuwa sawa kwa mfano Thailand, India, Malasia, Korea kusini ambazo zote zimetuacha mbali ni kwa ajili ya ulinzi wa mali hizi zisizoshikika ambazo ndizo pia zinawezesha mazingira ya kuingiza fedha nyingi za uwekezaji kutoka kwa wenye pesa na kuanzisha viwanda vyenye mali ya asili ya hapa. Nchi zote zinazoendelea ambazo ziliwahi kuona umuhimu wa kuweka kipengele cha miliki bunifu katika Katiba yake mapema, zimeweza kupata maendeleo ya haraka kama nilivyotaja hapo juu.

 Mifano ya nchi nyingine….
Marikani ni nchi moja wapo ambapo ulinzi wa Milikibunifu umewezesha maendeleo makubwa katika sanaa na teknolojia,
·      U.S. Constitution. Article I, Section 8 provides: "The Congress shall have Power … To promote the Progress of Science and useful Arts, by securing for limited Times to Authors and Inventors the exclusive Right to their respective Writings and Discoveries."
·      The Constitution of Malaysia, which is the supreme law of Malaysia, was adopted on 31 August 1957. Since then, the Constitution has been amended many times, most recently in 2009.
The Constitution contains provisions on intellectual property.
In the Legislative Lists (List I-Federal List) of the Ninth Schedule, the Constitution gives the federal government the power to enact laws relating to patents, designs, inventions, trade marks and mercantile marks, copyrights (Section 8 (e)).
·      Article 22 ya Katiba ya South Korea inasema (1) All citizens shall enjoy freedom of learning and the arts. (2) The rights of authors, inventors, scientists, engineers, and artists shall be protected by Act