Saturday, August 16, 2014

UMUHIMU WA MILIKIBUNIFU KUTAJWA KATIKA KATIBA MPYA

Katika Rasimu ya Katiba kumetajwa ulinzi wa mali, lakini ni wazi mali hizi ni zile zililzozoeleka katika akili za watu mali zinazohamishika na zisizohamishika. Kuna aina ya tatu ya mali ni ile inayotokana na ubunifu, na kwa sasa ndio mali inayolindwa zaidi na mataifa mengi, kwani ndio inayoleta ugunduzi wa madawa, mitambo, teknolojia, sanaa, na maendeleo ya kila aina. Hii huitwa Milikibunifu. Ni muhimu kutajwa kama zilivyofanya nchi nyingine ambazo zimefaidika sana na kulinda milikibunifu za wananchi wake.....
Milikibunifu au Intellectual Property Rights ni haki anazopewa mbunifu ili kulinda hali za mali yake ambayo haishikiki. Mali hii iyokanayo na ubunifu ni muhimu kuilinda kwani matokeo ya mali hii huwa faida kubwa kwa jamii. Milikibunifu ndizo haki ambazo huwalinda wagunduzi wa maendeleo katika teknolojia, madawa ya binadamu mifugo na kilimo, njia mbalimbali za kuongeza ubora na ufanisi wa teknolojia. Milikibunifu imegawanywa katika makundi mbalimbali ya ulinzi;
i.                Patent – (Hataza) hii ni njia ya kulinda na kusajili uvumbuzi mbalimbali wa kiteknolojia. Mfano vifaa vya kuvunia mazao kwa haraka zaidi, au kulima kwa haraka zaidi, vifaa vya uvuvi wa haraka, vifaa vya mawasiliano na vifaa vyovyote ambavyo vitaongeza thamani ya maisha yetu. Katika nchi kama Korea ya Kusini ulinzi wa Milikibunifu uliwekwa katika Katiba kuanzia baada ya vita ya pili ya dunia kwa kufusts mfumo wa  Katiba ya Marekani na ulinzi huo umeifanya wananchi wake ambao ni wabunifu kuweza kuja naubunifu ambao unatikisa dunia vifaa kama Samsung, Daewoo, KIA, LG ni matokeo ya ulinzi wa kikatiba wa wa Milikibunifu
ii.              Trademarks – (Alama za Biashara ) Alama za biashara huweza kufikia hatua ambapo zikawa na thamani kubwa kwani huweza kuaminika. Ili kulinda zisitumiwe hovyo au hata kuibiwa na wenye uwezo zaidi hulindwa na sheria za kulinda alama hizi. Kwa mfano Cocacola, Vodacom, Dell, na hapa kwetu Azam, ni majina ya bidhaa ambazo zina aminika, na hivyo kuwa na dhamani kubwa japo hazishikiki, nazo ni sehemu ya mali  ambazo hazishikiki lakini zina thamani kubwa
iii.             Industrial designs – Hizi ni haki wanazopewa wale wenye ubunifu wa kuweza kufanya usanii wenye kuboresha muonekano wa kitu ambacho tayari kimeshagunduliwa. Kwa mfano kila mtu ana simu ya mkononi lakini muonekano wa simu mbalimbali shape nap engine hali ya kuwa ni ya ku slide au kufungua au kupokea moja kwa moja ni matokeo ya design, pia vitu kama design za nguo, viatu , kiti ulichokalia makochi magari, vyote hivyo ndivyo matokeo ya industrial designs. Kazi za ubunifu huo ni muhimu kulindwa kwani huwa na thamani kubwa sana, kwa mbunifu na kwa mchango wake kwa nchi.  
iv.             Geographical Indication – Huu ni utambulisho wa wapi chanzo cha mali husika. Kwa mfano mvinyo kutoka Dodoma, Dodoma Wine ni mzuri na hivyo huitwa Dodoma Wine bila kulinda hili, watu watachukua mvinyo huu na kuupa hata jina jingine ukaitwa South African wine na hivyo kuiba haki wanazostaili kupata wakulima wa Dodoma, kutambuliwa kwa jina hili kutasababisha kutakiwa zaidi kwa wine hii duniani na hivyo kuweza kufanya hata Dodoma kuwa Wine City jambo ambalo linawezekana lakini nchi haijatambua umuhimu huu. Pia kuna mchele wa Kyela, Dagaa wa Kigoma na vitu kama hivi ambavyo havipatikani popote duniani kasoro sehemu iliyotajwa.  Nchi kama Uswiss imejenga jina miaka mingi ya utengenezaji wa saa bora hivyo saa ikiandikwa Swiss made huwa inajulikana ni bora na huwa gharama zaidi, Sigara kutoka Cuba, Cuban Cigars ni bei kubwa kwani hazipatikani popote kasoro Cuba, au mvinyo maarufu kama Champagne, ambao hutoka jimbo la Champagne Ufaransa, umejijengea sifa kubwa duniani na kuwa na bei kubwa sana kiasi cha kwamba si rahisi kwa mtu wa kipato cha kawaida kununua. Harusi zetu hutumia Sparkling Wine na kuiita Shampeni.
v.              Hakimiliki na Hakishiriki – Hizi ni haki zinazolinda kazi za kisayansi na kisanii. Computer Programs, Data, Utunzi wa vitabu, miswaada, hotuba, uchoraji, muziki, kazi za usonara, picha za mnato na filamu, uchongaji na kadhalika. Kazi hizi zimekuwa ni chanzo cha utajiri mkubwa kwa watu binafsi na Mataifa. Katika nchi ya Marekani kazi za Hakimiliki na Hakishiriki ni za pili katika uchangiaji wa pato la Taifa. Ripoti ya WIPO ya 2010 ilionyesha kuwa katika nchi ya Tanzania kazi za hakimiliki na Hakishiriki zilichangia asilimia 4.3 ya pato la taifa, karibu mara mbili ya mchango wa Madini!. Katika mwaka 2009 kazi za hakimiliki zilitengenza aslimia 5.63 ya ajira nchini, ikiwa juu ya mchango wa Afya (4.23), Biashara na mambo ya Fedha Real estate, &Business Service(2.37), Ujenzi (1.38),Usafirishaji na Mawasiliano (0.92), Umeme, Gas na maji (0.91), Madini (0.89)
Pamoja na umuhimu huu, Katiba inataja mali zinazoshikika tu-Zinazohamishika na zisizohamishika, hivyo mali hizi ambazo zimeonyesha kuleta maendeleo makubwa kwa nchi ambazo wakati wa Uhuru tulikuwa sawa kwa mfano Thailand, India, Malasia, Korea kusini ambazo zote zimetuacha mbali ni kwa ajili ya ulinzi wa mali hizi zisizoshikika ambazo ndizo pia zinawezesha mazingira ya kuingiza fedha nyingi za uwekezaji kutoka kwa wenye pesa na kuanzisha viwanda vyenye mali ya asili ya hapa. Nchi zote zinazoendelea ambazo ziliwahi kuona umuhimu wa kuweka kipengele cha miliki bunifu katika Katiba yake mapema, zimeweza kupata maendeleo ya haraka kama nilivyotaja hapo juu.

 Mifano ya nchi nyingine….
Marikani ni nchi moja wapo ambapo ulinzi wa Milikibunifu umewezesha maendeleo makubwa katika sanaa na teknolojia,
·      U.S. Constitution. Article I, Section 8 provides: "The Congress shall have Power … To promote the Progress of Science and useful Arts, by securing for limited Times to Authors and Inventors the exclusive Right to their respective Writings and Discoveries."
·      The Constitution of Malaysia, which is the supreme law of Malaysia, was adopted on 31 August 1957. Since then, the Constitution has been amended many times, most recently in 2009.
The Constitution contains provisions on intellectual property.
In the Legislative Lists (List I-Federal List) of the Ninth Schedule, the Constitution gives the federal government the power to enact laws relating to patents, designs, inventions, trade marks and mercantile marks, copyrights (Section 8 (e)).
·      Article 22 ya Katiba ya South Korea inasema (1) All citizens shall enjoy freedom of learning and the arts. (2) The rights of authors, inventors, scientists, engineers, and artists shall be protected by Act

No comments:

Post a Comment