Monday, September 14, 2015

MWANAMUZIKI KUIBURUZA KAMAPUNI YA SIMU MAHAKAMANI


MWANAMUZIKI wa Abuja, nchini Nigeria Omenuwoma Okson Dovie, aka Baba 2010, ameamua kuipeleka mahakamani kampuni ya simu ya  MTN kwa kukiuka haki zake za hakimiliki katika nyimbo zake nne, zikiwemo "Gentleman "Ometena", "Twisted" and "Unity Song."
Dovie anaituhumu kampuni hiyo kwa kubadili nyimbo hizo kuwa caller tunes/ring tones, na kuziuza bila ruksa yake kwa miaka mitatu mfululizo. Nyimbo hizo ziko kwenye album yake aliyoitoa 2005 ikiwa na jina
 "Twisted”.
Barua ya mwanasheria wake Rockson Igelige, imeitaka  MTN kumlipa mteja  wake naira milioni 500 (Tshs 5,455,000,000), kwa matumizi ambayo hayakuruhusiwa na yenye kupunguza thamani ya nyimbo zake. Na pia alitoa siku 14 ambazo MTN lazima iwe imekamilisha malipo au kujibu hoja.
Mshauri wa sheria wa MTN amekubali kuwa kapokea barua na kuwa kampuni hiyo inaliangalia swala hilo. Wakati huohuo Igelige amesema wameishauri Kamisheni ya Hakimiliki ya Nigeria kuwafungulia mashtaka MTN, wakati nao wakifungua mashtaka kwa upande wa mwanamuziki.

No comments:

Post a Comment