Tuesday, September 17, 2013

MTANDAO KUANDAA SEMINA YA WANAMUZIKI KUHUSU UKUSANYAJI NA UGAWAJI WA MIRABAHA KATIKA KAZI ZA MUZIKI

Kamati ya kuratibu mradi unaoendelea wawa Utafiti wa hali halisi ya ukusanyaji na ulipaji wa mirabaha leo imekaa na kupanga kufanya semina ya awali kwa baadhi ya wanamuziki ili kuanza kuelimisha taratibu za ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Semina hiyo itafanyika katika muda wa wiki mbili. Semina itahusisha wanamuziki wa aina tofauti za muziki, dansi, taarab, bongoflava, hiphop, gospel muziki asili nakadhalika

Sunday, September 15, 2013

MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA UFADHILI WA BEST AC


MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA umepata ufadhili kutoka Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) ili kuweza kufanya utafiti wa kina kupata ukweli wa hali halisi ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha ya muziki unaofanywa na COSOTA, na baada ya hapo kutoa ushauri wa nini kifanyike ili kuboresha hali iliyopo. Madhumuni ya mradi huu ni kuwezesha kufanya mabadiliko katika tasnia ya muziki ambayo yatatengeneza nafasi za ajira zenye tija ili kuwezesha tasnia kutoa mchango wake katika pato la Taifa, na kukuza sifa ya nchi kutokana na wasanii wengi wenye sifa waliomo hapa nchini.

Mradi utaangalia sheria zilizopo zinazohusu ugawaji wa mirabaha ya wanamuziki na mambo mengine yote yanayohusiana na shughuli ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha na kupendekeza taratibu za kuboresha hali.

Kamati za fedha na utawala zitaanza kazi wiki hii ili kuweza kufanikisha zoezi hili ambalo linatakiwa likamilike katika muda wa mwezi mmoja. Wanamuziki watashirikishwa katika semina ambayo itafanyika katika wiki chache zijazo.  Mtafiti kutoka Afrika ya Kusini amekwisha ingia mkataba na Mtandao ili kufanya kazi hiyo.

TANZANIA MUSICIANS NETWORK SECURES A GRANT FROM BEST AC



TMN has secured a grant from Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) to conduct a study to assess the existing arrangement under COSOTA in collection of music royalties and use the findings to provide clear and precise recommendations for appropriate interventions to advocate for change in collection system for the music industry growth of Tanzania.
The objective of the project is to initiate appropriate interventions that will support the Tanzania music industry to create the much needed jobs, subsequently taxes flowing back to government and enhancing the image of country built up from the talented artistes from institutionalized support for the industry.
The Project will specifically carry out a study to assess the legal framework regulating the distribution of royalties to musicians and other owners of copyright in works and all matters connected thereto and provide a report with recommendations.  The report will be used to engage with government to address the inefficiencies established with a purpose to strengthen the musicians' bargaining power in controlling the usage of their copyright.
The project is aims to examine the music industry landscape and the struggle on copyright protection, combating piracy, legislative instruments to implement copyright and managing music rights; mandate, transparency, fairness in collection and timely payment of royalties to artists.  The purpose is to seek government’s support to have clear distinguished roles of the Copyright Society of Tanzania (COSOTA) as a Government copyright office from that of collecting organization. The project should identify the important stake holders in the industry such as Publishers, Distributors, Manufacturers of musical works, lyrists, arrangers, producers, executive producers and such others and their roles in the Royalties payment chain.

Tuesday, September 3, 2013

MWENYEKITI WA MTANDAO WA WANAMUZIKI JOHN KITIME, ATEULIWA MJUMBE WA BASATA


Profesa Penina Mlama
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Penina Mlama kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari - MAELEZO leo, Uteuzi huo wa Profesa Mlama unaanzia mwaka 2013 na unatarajia kumalizika mwaka 2016.
Prof. Mlama ni Profesa wa Sanaa na Sanaa za Maonyesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla watu 12 kuwa wajumbe wa BASATA kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu.
Walioteuliwa ni pamoja na wawakilishi wa Vyama na Asasi mbalimbali wa Baraza hilo ambao ni Dkt. Vincensia Shule, John Kitime , Angela Ngowi, Dkt. Herbert Makoye, Erick Shigongo na Alex Msama.
John Kitime

Wawakilishi wengine ni pamoja na Juma Adam Bakari, Daniel Ndagala, Michael Kadinde na Joyce Fisoo.
Wanaoingia kwa mujibu wa nyadhifa zao ni Prof. Hermas Mwansoko na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Katika hatua nyingine Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amemteua Bwana Ghonche Materego kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
Kabla ya uteuzi huo Materego alikuwa amemaliza muda wake kama Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa.
Wajumbe wa Bodi hiyo walioteuliwa na Waziri Mukangara ni Dkt. Herbert Makoye, Prof. Emanuel Mbogo, Dkt. Lucy Mboma, Prof. Hermas Mwansoko pamoja na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla ya watu 21 kuwa wajumbe wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.
Wajumbe hao ni Dkt. Shani Omari, Prof. Yohana Msangila, Ester Riwa, Dkt. Issa Zidi, Khadija Juma na Dkt. Martha Qorro.
Wengine ni Mmanga Mjawiri, Razia Yahaya, Richard Mbaruku, Selina Lyimo, Keneth Konga, Amour Khamis, John Kiango, na Shani Kitogo.
Wajumbe wengine ni Ally Kasinge, Ahmed Mzee, Rose Lukindo, Shabani Kisu pamoja na Edwin Mgendera.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo la BAKITA atachaguliwa na wajumbe watakapokutana kwenye kikao chao cha kwanza.

Thursday, August 22, 2013

Mwenyekiti na Mweka Hazina katika mafunzo ya siku tatu

Mwenyekiti wa Mtandao John Kitime na Mweka hazina wa Mtandao Bi Asha Salvador, wamo katika mafunzo ya siku tatu ya Public Policy Advocacy, mafunzo yanayoendelea UDSM

Friday, August 16, 2013

KICHEKESHO..MWANAMUZIKI NA NJAA ZAKE

Mwanamuziki mmoja alikuwa na tabia ya kukuta mkewe kampikia chakula kila alipotoka kazini usiku. Siku moja mkewe akawa anaumwa hakupika hivyo jamaa aliporudi hakukuta chakula akalazimika kulala njaa. Katika usingizi akaota ankula ugali  wa nguvu. Asubuhi alipoamka akakuta katafuna kona nzima ya godoro

Wednesday, August 14, 2013

Sikiliza SIUMWI SIKU YA MSHAHARA ya Soggy The Hunter

Msanii Anselm Soggy The Hunter ametuma kazi yake hii na haya ndio maelezo ya kazi hiyo.......
Ndugu zangu baada ya kuufanyia mixing upya sasa naachia rasmi ngoma yangu mpya SIUMWI SIKU YA MSHAHARA nikiwa na WATENGWA na imetengenezwa ARUSHA chini ya DAZ NALEDGE naombeni msaada wenu.Ni aina ya Hip-hop ngumu ambayo sijawahi kufanya miaka yangu yote miaka 18 kwenye muziki

Wanamuziki wakutana na kusafisha ofisi yao mpya.

 Katika kuonyesha kuwa wako katika nia ya ujio mpya wanamuziki kadhaa walikutanika na kufanya usafi wa ofisi yao asubuhi ya leo. Samani za ofisi zinategemewa kuingizwa siku ya  Alhamisi na baada ya hapo Katibu Mkuu Abraham Kapinga mwanamuziki mpiga gitaa wa Tanzanite Band atatoa ratiba ya matumizi ya ofisi.





Tuesday, August 13, 2013

MKUTANO WA WANAMUZIKI WAFANA


Ule mkutano ulioitishwa na Tanzania Musicians network (TMN) au Mtandao wa Wanamuziki  Tanzania umekuwa wa mafanikio makubwa. Kwanza kwa mahudhurio ya wasanii mbalimbali wakiwemo wanamuziki wa muziki asili, taarab, dansi, bongoflava na gospel, pia kulikuweko na mameneja wa wanamuziki na mabendi mbalimbali, producers. Hii ilikuwa ni mafanikio makubwa kwani ilionyesha maana halisi ya mtandao.
Pamoja na maelezo ya madhumuni ya kutengeneza mtandao, mwenyekiti wa Mtandao John Kitime alieleza kuwa wanamuziki wa Tanzania lazima wafanye kazi ya ziada ili kuwakamata kimaendeleo wenzao wa nchi nyingine Afrika. Wanamuziki walielezwa umuhimu wa kutumia teknolojia ya internet kwa kuhakikisha kuwa kila mwanamuziki ana anwani ya barua pepe na kujitahidi kuingia kwenye mitandao ya kijamii kama Facebook na kuitumia vizuri kwa kutangaza kazi zao. Wanamuziki walikaribishwa kutumia blog yao ya www.tanzaniamusicians.blogspot.com kwa kupeleka matangazo, picha za matukio mbalimbali hata ya shughuli binafsi kama birthday, harusi na  kadhalika na pia kutuma hata nyimbo zao ili ziweze kutundikwa katika mtandao huo bure bila malipo. Wanamuziki walielekezwa kutuma kazi zao kupitia anwani ya musicnettz@gmail.com.
Katibu Mkuu wa mtandao Abraham Kapinga, alitoa maelezo kuhusu hali ya ofisi, ambapo wanamuziki walielezwa kuwa ofisi iko Kinondoni karibu na American Chips, mtaa wa CHADEMA, na kwa vile ndio tumekabidhiwa ofisi, wanamuziki waliafikiana kukutana hapo na kuifanyia ofisi usafi, jambo ambalo nalo lilionyesha nia ya wanamuziki kulea chama chao. Mwanamuziki Hussein Jumbe alijitolea viti 4 kwa ajili ya ofisi, jambo ambalo kwa kila hali ni la kutia moyo kuhusu mwanzo huu wa mtandao.
Mweka hazina wa Mtandao Asha Salvador alitoa taarifa ya vifaa vya ofisi vilivyonunuliwa vikiwemo viti, meza feni, na stationary.
Maelezo mengine muhimu yaliyotolewa ni kuhusu wanamuziki kujiunga na chama, na kulipia ada ili kuweza kuendesha ofisi. Fomu za wanachama ni shilingi 1000/- ada ya mwaka 5,000/- na kiingilio ni shilingi 20,000/-.
Wajumbe walipata muda wa kutoa mawazo na mapendekezo. Mjumbe mmoja alitoa mapendekezo ya mtandao kuwezesha wanamuziki kutoa maoni yao kuhusu Rasimu ya  Katiba ya nchi na  mjumbe mmoja alijitolea kufuatilia taratibu za kuhakikisha wanamuziki wanashiriki katika jambo hilo muhimu.  Mjumbe mwingine alitaka Mtandao uandae program za elimu ya Management ya Band na hata elimu kwa wanamuziki kujitambua na hivyo sio kufika mahala kuporomoka baada ya muda mfupi, pia itolewe elimu kuhusu haki mbalimbali za wanamuziki. Mmoja wa wajumbe alieleza kuwa ametoka nje ya nchi karibuni alikopata elimu ya vocal training, na hivyo Mtandao uandae taratibu ili elimu hii iwafikie wanamuziki waimbaji.
Mjumbe mmoja alitoa taadhari kuhusu hali inayoelekea sasa ambayo inafanya kuweko na uhasama kati ya wanamuziki wa kizazi kipya na wale wa zamani, badala ya wote kutambuana kuwa ni wanamuziki wanaoweza kufanya kazi pamoja na kupata mafanikio makubwa zaidi, Mtandao uliombwa uwe chombo cha kuunganisha wanamuziki wote bila kujali aina ya muziki wa rika.
Swala la vyombo vya utangazaji liliongelewa hasa kuhusu rushwa iliyokithiri katika vyombo hivi ikawekwa hadharani. Mjumbe mmoja alieleza kuwa imefikia kuwa inahitajika shilingi milioni moja kuwezesha wimbo kupigwa katika radio, kwani kuna mgao wa kuanzia mtu anaweka nyimbo kwenye playlist hadi watangazaji wa vipindi mbalimbali kwa ajili ya kupiga muziki na interviews. Ilionekana tatizo hilo lipo hata kwenye radio zinazopiga muziki wa Gospel ambako tofauti ni bei tu. Ambapo bei ya kupigwa wimbo ni kati ya shilingi alfu 80 hadi laki moja. Mtandao ulitakiwa ufuatilie utekelezaji wa sheria ya kulipia matumizi ya muziki katika vyombo vya utangazaji, ambayo ilikuwa ianze kutumika toka 2003.
Wanamuziki walimaliza siku kwa kutumia muda kujaza fomu za uanachama.