Wednesday, October 21, 2015

DOUBLE M WAKO MSUMBIJI KWA MARA YA PILI



Baada ya kazi nzuri ya awali Double M Sound chini ya Muumin Mwinyjuma imealikwa tena Msumbiji. Kwa maneno yake mwenyewe kiongozi huyu wa kundi hilo alituma ujumbe huu, “Nipo  njiani na vijana wangu tunaenda Msumbiji, tumepata mualiko  mwingine, safari hii tumealikwa na serikali kupitia Manispaa ya Mkoa Wa PEMBA, baada ya kufurahishwa na kazi yetu ya mwezi uliopita. Kuna sherehe ya Kitaifa ambayo hua inazunguka kila Mkoa na mwezi huu inafanyika ktk Mkoa Wa Mpemba, kutakua na burudani za aina nyingi  tofauti. Safari Hii tumetakiwa kuwa na idadi ya watu 14 tofauti na safari ya kwanza tulikwenda 19.
Kwenye msafara wetu tupo watu 13 na mwenzetu mmoja fundi mitambo na mpiga tumba Omar Zagalo alibaki kule na vyombo toka tulipoenda mara ya kwanza. Tulio kwenye msafara huu ni mimi Muumin Mwinyjuma, Rashid Sumuni-solo, Pascal Kinuka-bass, Issa Ramadhani-kinanda, H Waninga-drums, Amina Juma, Salehe Kupaza na  Dogo Rama waimbaji, madansa ni Verosa,Regina, Salma, Titi na Star. Tunasafiri kwa njia ya bus tukishavuka Boda saa 10 Jioni tutachukuliwa na gari lililoandaliwa na wenyeji wetu, ambayo itatumia saa 1-30 kutufikisha mji wa Msimbwe na hapo tutapanda ndege maalum itakayotupeleka Pemba. Tuombeeni Mungu tufanye vizuri zaidi kwani Show hii ni muhimu sana kujitangaza na kuutangaza muziki wa Bendi za TZ."

No comments:

Post a Comment