Thursday, June 19, 2014

WASANII WAKUTANA NA KUTOA MCHANGO KATIKA UTAYARISHAJI WA SERA YA MILIKIBUNIFU YA TANZANIA



Wasanii kadhaa wakiwemo viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa yote yaliyopo,wiki iliyopita walikutana katika ukumbi wa Chichi Hotel Kinondoni kutoa mchango wao katika utengenezaji wa Sera ya Taifa ya Milikibunifu (National Intellectual Property Policy). Katika mradi huu wa pamoja wa Tanzania Musicians Network (TAMUNET) na Tanzania Film Federation (TAFF), ambao umefadhiliwa na BEST AC, wasanii hawa walipata nafasi kuchangia mambo mbalimbali kuhusu kipengele cha Hakimiliki katika sera ya Milikibunifu. Washiriki wakiongozwa na mtaalamu Ernest Omalla na John Kitime , Mwenyekiti wa TAMUNET na wataalamu kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, mambo mengi yalipendekezwa yawemo katika sera hiyo.Bado zinatafutwa taratibu za kuweza kuwapata wadau wengine wa Hakimiliki ili waweze kuongeza ubora wa sera hii.












No comments:

Post a Comment