Thursday, June 19, 2014

COSOTA KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA


Rob Hooijer
CHAMA cha Hakimiliki cha Tanzania kimekuwa katika wiki moja na nusu ya warsha, na mikutano ya kukiboresha ambayo inaendeshwa na mtaalamu Robert Hooijer kutoka Afrika ya Kusini. Kazi kubwa iliyokuwa inafanyika ni kuiwezesha COSOTA kufanya kazi katika mifumo ya kisasa ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Mr Hooijer ni mtu mwenye uzoefu wa miaka mingi katika shughuli za Hakimiliki, aliwahi kuwa CEO wa CISAC, ambacho ndicho muungano wa vyama vyote vya ukusanyaji mirabaha duniani na pia alikuwa CEO wa South African Musicians Rights Organisation (SAMRO) ambayo ndicho chama kikubwa kuliko vyote cha ukusanyaji wa mirabaha Afrika. Kwa kipindi hiki amekuwa Kenya akisaidia shughuli kama hii na mafanikio makubwa yamewezekana huko.









No comments:

Post a Comment