Wednesday, February 19, 2014

HARAKATI ZA WASANII KUPATA NAFASI KATIKA KATIBA MPYA—3


Kamati ilipata mapokezi ya heshima kubwa kutoka kwa wabunge wa CHADEMA, ambapo Wabunge  sita wa CHADEMA walikaa na kuwasikiliza wawakilishi hawa wa wasanii wakieleza mapendekezo yao katika Katiba kuhusiana na wasanii. Wasanii wana ajenda mbili,




 1. Kundi la wasanii kutajwa katika Katiba kuwa ni kundi rasmi kutokana na ukubwa wa kundi hili nchini, kama yalivyotajwa makundi ya wakulima, wafugaji, wavuvi na kadhalika, pia mchango wake katika ajira ya vijana na ukubwa wa pato linalotokana na kundi hili, ambalo kutokana na kutokutambuliwa linapotea katika mifuko ya watu na kukosesha wasanii na Taifa pato kubwa. 
2. Wasanii walitaka ubunifu ulindwe kwanza kwa ulinzi wa Milikibunifu kutajwa rasmi katika katiba na hivyo kuwezesha sheria bora kutungwa na pia utekelezaji wa ulinzi wa kazi zao uweko kama ilivyo katika mali nyingine za wananchi wengine. Kikao cha saa moja na nusu kilikuwa cha mafanikio na kuwa na faida kwa pande zote mbili.
Wasanii hawakulala mapema kwani walimalizia siku na kuhamia  eneo jingine ambapo walikuwa na kikao na Mheshimiwa Mbunge wa Donge ambae pia ni Mwenyekiti wa Ummoja wa Vijana wa CCM Taifa Mheshimiwa Sadifa, ambapo kikao hicho kiliisha saa saba ya usiku.

No comments:

Post a Comment