Wednesday, June 21, 2017

MTANDAO WA MUZIKI TAMUNET WAJIPANGA UPYA

Katika kuadhimisha Siku ya Muziki Duniani ambayo husherehekewa kila tarehe 21 June, wajumbe wa Mtandao wa Muziki, Tanzania Musicians Network, leo wamesherehekea kwa kufanya kikao kilichojenga kamati ya uongozi ya mud, viongozi hawa watakuwa katika uongozi kwa mwaka mmoja kisha kutayarisha Mkutano Mkuu wa kuchagua viongozi wa kudumu.  Katika kikao cha leo kilichotumia masaa matatu safu ya uongozi mpya ni kama ifuatayo;
1.  Mwenyekiti - John F Kitime
2.  Makamu Mwenyekiti - Rashid Pembe
3.  Katibu Mkuu - Innocent Nganyagwa
4.  Katibu Mkuu Msaidizi - Geophrey Kumburu
5.  Mweka Hazina - Asha Warsama
6.  Wajumbe - David Ng'asi, Abdul Salvador
TAMUNET ni chama ambacho malengo yake ni kutetea haki za wanachama wake kama wafanyakazi katika tasnia, na kuwa chama rasmi cha wafanyakazi waliomo katika tasnia ya muziki (Musicians Union). Uongozi uliopo unajipanga kuhakikisha chama kinafanya kazi yake ambayo imo katika katiba yake. 
Picha za uongozi mpya wakiwa katika kikao




No comments:

Post a Comment