Thursday, November 12, 2015

KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO ATEMBELEA BASATA


IMG_20151112_131420 Prof Elisante akiongea na akina mama wanaofanya sanaa ya kutengeneza Batik katika maeneo ya BASATAIMG_20151112_211008 Toka kushoto Godfrey Mngereza, Katibu Mtendaji BASATA, Prof Elisante Ole Gabriel, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, John Kitime Mjumbe wa Bodi BASATA, Kaimu Mkurugenzi wa Utamaduni 
KATIBU mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Vijana na Michezo Prof Elisante Ole Gabrielleo ametembelea Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA). Katibu MKuu baada ya kuzunguka na kuangalia maeneo yote ya Baraza, hatimae alikuwa na mkutano na wafanya kazi wa Baraza. Katika mkutano huo Katibu Mkuu alisema ametembelea Baraza ili kufahamiana,na pia kufafanua kauli mbiu ya Rais ya HAPA KAZI TU.
Katibu Mkuu alisifia Baraza kwa kusimamia sheria na taratibu zilizounda Baraza hilo. Profesa alilitaka Baraza kuhakikisha kuwa linakuwa na ufanisi zaidi na pia kuwezesha kutafuta masoko ya uhakika ya kazi za sanaa. Tanzania ina kazi nyingi sana za sanaa hivyo alilitaka Baraza kuhakikisha zinafahamika zinatangazwa, na zinasambazwa, ili kuleta manufaa kwa wasanii na kuchangia pato la nchi kwa kodi. Katibu Mkuu aliagiza kuwa viongozi wa Baraza wawe mfano katika utendaji wa kazi, heshima kwa watumishi wote na pia wawe waadilifu katika kazi zao. Katibu Mkuu aliwaasa watumishi wa Baraza kuipenda kazi yao kuwa wazalendo na kuwajibika ipasavyo, kuheshimu viongozi na kuwasiliana kwa staha pale kunapokuwa na tatizo. Aliwakumbusha wafanya kazi kuwahi kazini lakini pia alikumbusha uongozi kutokuwaweka wafanya kazi masaa ya ziada bila ya sababu za msingi, kwani wanahtaji kupumzika baada ya kazi za siku nzima. Aliwaonya watumishi kuhusu ‘majungu’ na kuwataka waepuka jambo hilo kwani ni chanzo cha kuharibu kazi. Kabla ya hotuba hii Katibu Mtendaji alimueleza Katibu Mkuu kuhusu changamoto za Baraza na baadhi ya njia ambazo zingefanywa kutatua changamoto hizo. Katibu Mkuu alisema kuwa yeye haridhiki na hali ya uchumi ya wasanii na alitaka Baraza lifanye kazi kubadili hali hii. Na mwisho alisisitika kuwa kauli ya Hapa Kazi tu ni ya ukweli na kila mtu aishi kwa kauli mbiu hiyo.
Kabla ya maelezo haya Katibu Mtendaji wa Basata alitoa baadhi ya changamoto za uendeshaji wa BASATA. Kati ya changamoto hizo alizitaja kuwa ni ukosefu wa sera za sanaa, kupitwa na wakati kwa sheria iliyounda Baraza. Mtawanyiko wa asasi zinazotawala wasanii. Ukosefu wa masoko ya sanaa, kutokukamilika kwa ukumbi wa BASATA, tatizo la siasa kujikita katika sanaa, na pia uhamasishaji wa Bima ya Afya kwa wasanii.
Katibu Mtendaji alimkabidhi Katibu Mkuu, nyaraka zote zilizotayarishwa kuhusu changamoto hizo

No comments:

Post a Comment