Wednesday, October 30, 2013

WANAMUZIKI WA TANZANIA WAFANYA WARSHA KUBWA







Martin Cuff

 Warsha kubwa ya siku moja ya wanamuziki wa tanzania yafanyika pale Nyumbani Lounge. Wanamuziki kutoka kila aina ya muziki walikuweko. katika warsha hii iliyoomgozwa na mtafiti Martin Cuff ilikuwa ni kutoa report ya utafiti wake kuhusu hali halisi ya utekelezaji wa Ukusanyaji na ugawaji wa Mirabaha. Wanamuziki walipata nafasi ya kuchangia  na kutoa mapendekezo. Ripoti nzima kutoka katika wiki mbili zijazo. Utafiti ulifanywa na Martin Cuff na kuongozwa na Tanzania Musicians Network kwa ufadhili wa BEST AC.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ndie aliyefunga warsha hii kwa kusifu jitihada hii ya wanamuziki kufanya utafiti. Katika kukutana huku na Naibu Katibu mkuu wanamuziki walioingia mkataba na kampuni mojawapoya ringtones walilalamika kuwa waliingia mkataba wa miaka kumi na kampuni hiyo na baada ya hapo kampuni hiyo haikutaka hata kujibu barua zao, Naibu Katibu Mkuu aliwaita wahsanii hao ofisini kwake ili kuona cha kufanya, pia alimtaka Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network John Kitime amuone ili waongelee tatizo la TBC kutokulipa mirabaha na kuatafuta suluhu.


















No comments:

Post a Comment