Pamoja na kuwa leo ni siku ya Jumapili, watu wengi huwa wanapumzika, maproducer kadhaa wamejikusanya na kuhudhuria semina ya Hakimiliki iliyoendeshwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime. Semina hiyo iliyofanyika katika jengo la Sayansi na Teknolojia iliwawezesha Producers kufahamu nini maana ya Hakimiliki na vilevile kupata elimu ya awali kuhusu yaliyomo katika sheria ya Hakimiliki ya hapa nchini
Sunday, October 20, 2013
JULIUS NYAISANGAH.... UNCLE J.,,.SUPER TALL HATUNAE TENA
MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA UNATOA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KWA NDUGU , RAFIKI, NA WANAMUZIKI WALIOWAHI KUFANYA KAZI NA MTANGAZAJI MKONGWE JULIUS NYAISANGA, ALIYEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO 20 OKTOBA, 2013 KATIKA HOSPITALI YA MAZIMBU MOROGORO.
MUNGU AMLAZE PEMA JULIUS, KAZI YAKO ULIOIFANYA KATIKA TASNIA YA MUZIKI HAITAFUTIKA
MUNGU AMLAZE PEMA JULIUS, KAZI YAKO ULIOIFANYA KATIKA TASNIA YA MUZIKI HAITAFUTIKA
Wednesday, October 16, 2013
Je unapenda muziki wa Mashujaa Band?
Bendi ya Mashujaa imetengeneza ukurasa wao ambapo unaweza sasa kusikiliza nyimbo zao nyingi kutoka hapo. Je wewe au bendi yako mnanyimbo katika mtandao wa intanet, basi tutumie anwani au wimbo kupitia musicnettz@gmail.com ili tuuweke katika blog yetu.
Kwa kusikiliza nyimbo za Mashujaa ingia HAPA upate nyimbo zao
Kwa kusikiliza nyimbo za Mashujaa ingia HAPA upate nyimbo zao
Thursday, October 3, 2013
KIPINDI CHA MIKIKI MIKIKI YA MUZIKI KUANZA KURUKA JUMAMOSI HII SAA 12:30 JIONI TBC RADIO YA TAIFA
BAADA ya kupata ufadhili wa BEST AC kwa kupitia Tanzania Heritage Project, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TMN), utaanza kurusha vipindi vya radio kupitia Radio TBC Taifa. Vipindi hivyo ambavyo vitaendeshwa na mwanamuziki na mwenyekiti wa Mtandao John Kitime. Kipindi cha kwanza kitaanza na kuangalia biashara ya muziki kwa kutegemea viingilio ilivyo na kama kweli inalipa na kitashirikisha kwa kukusanya maoni kutoka kwa wasikilizaji. Kipindi hiki ni mwanzo wa vipindi vingi vya redio vitakavyohusu muziki kama utamaduni, taaluma na kama biashara. Karibuni tusikilize na tutoe maoni kupitia blog hii na ukurasa wa facebook https://www.facebook.com/wanamuzikiwa.tanzania Wanamuziki wa Tanzania tuna uwezo kama wanamuziki wengine duniani lakini tuna matatizo makubwa ya mpangilio katika tasnia yetu
Monday, September 30, 2013
WANAMUZIKI WAWILI WA TEMEKE WAFARIKI LEO
Msanii wa kundi la WATEULE, Malik Ahmed Moa maarufu kwa jina la Mack2B amefariki dunia leo. Msiba utakuwa Yombo kwa wazazi wake Mack 2B alikuwa producer na msanii wa raga, amefariki kutokana na ugonjwa wa figo uliokuwa unamsumbua muda mrefu
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMIN
**********************************************************
Mwanamuziki mpiga bezi wa siku nyingi Joseph Watuguru
amefariki mchana huu katika hospitali ya Amana. Watuguru amewahi kupigia bendi nyingi zikiwemo Bantu Group ya Hamza Kalala, Magoma Moto Sound, African Stars ile ya mwanzo kabisa Mchinga Sound, na katika siku zake za mwisho alikuwa bendi ya WK Sound ya Temeke. Watuguru aliwahi kushiriki katika bendi iliyotengenezwa na Producer kutoka Norway Sigbjorn Nedland iliyoitwa Mradi Group akiwa na akina Bob Rudala, Keppy Kiombile, John Saggati, Bizimana Ntavyu, Anania Ngoliga na wengine. Alikuwa mpiga bezi mzuri na pia fundi mitambo wa kutegemewa
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMIN
**********************************************************
Joseph akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wakati akiwa African Stars |
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA
Tuesday, September 17, 2013
MTANDAO KUANDAA SEMINA YA WANAMUZIKI KUHUSU UKUSANYAJI NA UGAWAJI WA MIRABAHA KATIKA KAZI ZA MUZIKI
Kamati ya kuratibu mradi unaoendelea wawa Utafiti wa hali halisi ya ukusanyaji na ulipaji wa mirabaha leo imekaa na kupanga kufanya semina ya awali kwa baadhi ya wanamuziki ili kuanza kuelimisha taratibu za ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Semina hiyo itafanyika katika muda wa wiki mbili. Semina itahusisha wanamuziki wa aina tofauti za muziki, dansi, taarab, bongoflava, hiphop, gospel muziki asili nakadhalika
Sunday, September 15, 2013
MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA UFADHILI WA BEST AC
MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA umepata ufadhili kutoka
Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) ili kuweza kufanya
utafiti wa kina kupata ukweli wa hali halisi ya ukusanyaji na ugawaji wa
mirabaha ya muziki unaofanywa na COSOTA, na baada ya hapo kutoa ushauri wa nini
kifanyike ili kuboresha hali iliyopo. Madhumuni ya mradi huu ni kuwezesha
kufanya mabadiliko katika tasnia ya muziki ambayo yatatengeneza nafasi za ajira
zenye tija ili kuwezesha tasnia kutoa mchango wake katika pato la Taifa, na
kukuza sifa ya nchi kutokana na wasanii wengi wenye sifa waliomo hapa nchini.
Mradi utaangalia sheria zilizopo zinazohusu ugawaji wa
mirabaha ya wanamuziki na mambo mengine yote yanayohusiana na shughuli ya
ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha na kupendekeza taratibu za kuboresha hali.
Kamati za fedha na utawala zitaanza kazi wiki hii ili
kuweza kufanikisha zoezi hili ambalo linatakiwa likamilike katika muda wa mwezi
mmoja. Wanamuziki watashirikishwa katika semina ambayo itafanyika katika wiki chache zijazo. Mtafiti kutoka Afrika ya Kusini amekwisha ingia mkataba na Mtandao ili
kufanya kazi hiyo.
TANZANIA MUSICIANS NETWORK SECURES A GRANT FROM BEST AC
TMN has secured a grant from Business Environment
Strengthening of Tanzania (BEST – AC) to conduct a study to assess the existing
arrangement under COSOTA in collection of music royalties and use the findings
to provide clear and precise recommendations for appropriate interventions to advocate
for change in collection system for the music industry growth of Tanzania.
The objective of the project is to
initiate appropriate interventions that will support the Tanzania music
industry to create the much needed jobs, subsequently taxes flowing back to
government and enhancing the image of country built up from the talented
artistes from institutionalized support for the industry.
The Project will specifically carry
out a study to assess the legal framework regulating the distribution of
royalties to musicians and other owners of copyright in works and all matters
connected thereto and provide a report with recommendations. The report will be used to engage with
government to address the inefficiencies established with a purpose to strengthen
the musicians' bargaining power in controlling the usage of their copyright.
The project is aims to examine the music industry landscape
and the struggle on copyright protection, combating piracy, legislative
instruments to implement copyright and managing music rights; mandate,
transparency, fairness in collection and timely payment of royalties to
artists. The purpose is to seek
government’s support to have clear distinguished roles of the Copyright Society
of Tanzania (COSOTA) as a Government copyright office from that of collecting
organization. The project should identify the important stake holders in the
industry such as Publishers, Distributors, Manufacturers of musical works,
lyrists, arrangers, producers, executive producers and such others and their
roles in the Royalties payment chain.
Sunday, September 8, 2013
Tuesday, September 3, 2013
MWENYEKITI WA MTANDAO WA WANAMUZIKI JOHN KITIME, ATEULIWA MJUMBE WA BASATA
Profesa Penina Mlama |
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari - MAELEZO leo, Uteuzi huo wa Profesa Mlama unaanzia mwaka 2013 na unatarajia kumalizika mwaka 2016.
Prof. Mlama ni Profesa wa Sanaa na Sanaa za Maonyesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla watu 12 kuwa wajumbe wa BASATA kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu.
Walioteuliwa ni pamoja na wawakilishi wa Vyama na Asasi mbalimbali wa Baraza hilo ambao ni Dkt. Vincensia Shule, John Kitime , Angela Ngowi, Dkt. Herbert Makoye, Erick Shigongo na Alex Msama.
John Kitime |
Wawakilishi wengine ni pamoja na Juma Adam Bakari, Daniel Ndagala, Michael Kadinde na Joyce Fisoo.
Wanaoingia kwa mujibu wa nyadhifa zao ni Prof. Hermas Mwansoko na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Katika hatua nyingine Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amemteua Bwana Ghonche Materego kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
Kabla ya uteuzi huo Materego alikuwa amemaliza muda wake kama Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa.
Wajumbe wa Bodi hiyo walioteuliwa na Waziri Mukangara ni Dkt. Herbert Makoye, Prof. Emanuel Mbogo, Dkt. Lucy Mboma, Prof. Hermas Mwansoko pamoja na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla ya watu 21 kuwa wajumbe wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.
Wajumbe hao ni Dkt. Shani Omari, Prof. Yohana Msangila, Ester Riwa, Dkt. Issa Zidi, Khadija Juma na Dkt. Martha Qorro.
Wengine ni Mmanga Mjawiri, Razia Yahaya, Richard Mbaruku, Selina Lyimo, Keneth Konga, Amour Khamis, John Kiango, na Shani Kitogo.
Wajumbe wengine ni Ally Kasinge, Ahmed Mzee, Rose Lukindo, Shabani Kisu pamoja na Edwin Mgendera.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo la BAKITA atachaguliwa na wajumbe watakapokutana kwenye kikao chao cha kwanza.
Subscribe to:
Posts (Atom)