Wanamuziki kadhaa wenye heshima
katika muziki wa dansi watakuweko katika Tamasha la Gurumo 53, ambalo ni
tamasha la kustaafu muziki mwanamuziki mkongwe Muhidin Maalim Gurumo. Kati ya
wanamuziki watakao panda jukwaani ni
Komandoo Hamza Kalala, Mzee Makassy, wanamuziki nyota waliowahi kutamba
na bendi ya DDC Mlimani Park , Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe,
Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa,
Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande. Pia wapulizaji wakongwe Majengo na King
Maluu watakuweko na wote kwa pamoja wataporomosha show kubwa Jumamosi
hii ndani ya TCC Club Chang’ombe. Wakali hao jana Alhamisi walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano
watakazopiga katika tamasha hilo. Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club
ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa
wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo zilizofanyiwa
mazoezi ni pamoja na “Selina”
utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka
kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa). Tamasha
la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka
katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi
kustaafu muziki. Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia,
Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga. Burudani zingine zitakazokuwepo siku
hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga
Pepeta.
Friday, December 13, 2013
Wednesday, November 20, 2013
MWENYEKITI WA MTANDAO ATOA MADA YA UTAFITI WA MALIPO YA MIRABAHA
Katika Jukwaa la Sanaa ambalo huweko kila Jumatatu katika ukumbi wa BASATA , wiki hii Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime alichambua utafiti uliokamilika karibuni uliofanywa na mtafiti Martin Cuff kwa niaba ya Mtandao kwa ufadhili wa BEST AC. Utafiti huo ambao umo kwenye kitabu chenye kurasa 84 unachambua hali halisi ya Hakimiliki Tanzania, na mapungufu yake na kisha kutoa mapendekezo ya kuboresha hali hiyo kwa manufaa ya wenye Hakimiliki na tasnia ya muziki kwa ujumla. Kitabu cha utafiti huo kitapatikana baada ya muda si mrefu.
Thursday, November 7, 2013
UBALOZI WA MAREKANI WAKABIDHI VITABU 800 KWA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA
Ubalozi wa marekani nchini Tanzania, leo hii 7/11/2013
umemkabidhi vitabu vya Hakimiliki zaidi ya 800 Mwenyekiti wa Tanzania
Musicians Network, John F Kitime katika hafla iliyofanyika katika maktaba ya
Ubalozi huo uliopo jijini Dar es Salaam. Kitabu hicho chenye lugha mbili
Kiswahili na Kiingereza kimetungwa na Alex Perullo ambaye ni Associate Professor wa Anthropology na African Studieskatika chuo cha
Bryant Marekani. Hiki ni kitabu cha pili cha aina hii kutungwa na Profesa huyu,
cha kwanza alikisambaza kupitia Ubalozi huu huu miaka kumi iliyopita. Kwa vile
kina lugha mbili kitabu hiki kina majina mawili kinaitwa Artistic Rights na
Haki za Kisanii. Ni kitabu cha kurasa 98 ambacho kimejaa maelezo mengi kuhusu
haki za wasanii, wasanii watakao kisoma watafaidika sana.
Mtandao wa Muziki Tanzania, utakisambaza
kitabu hiki katika taasisi mbalimbali muhimu na pia utawapa bure wanachama wake
nakala za kitabu hiki muhimu. Dibaji ya kitabu hiki imeandikwa na John Kitime.
Wednesday, October 30, 2013
WANAMUZIKI WA TANZANIA WAFANYA WARSHA KUBWA
Martin Cuff |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ndie aliyefunga warsha hii kwa kusifu jitihada hii ya wanamuziki kufanya utafiti. Katika kukutana huku na Naibu Katibu mkuu wanamuziki walioingia mkataba na kampuni mojawapoya ringtones walilalamika kuwa waliingia mkataba wa miaka kumi na kampuni hiyo na baada ya hapo kampuni hiyo haikutaka hata kujibu barua zao, Naibu Katibu Mkuu aliwaita wahsanii hao ofisini kwake ili kuona cha kufanya, pia alimtaka Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network John Kitime amuone ili waongelee tatizo la TBC kutokulipa mirabaha na kuatafuta suluhu.
Monday, October 28, 2013
MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA WAFANYA WARSHA YA SIKU MOJA
WANAMUZIKI takriban 70 leo wameshinda siku nzima wakijadili ripoti ya utekelezaji wa Hakimiliki katika kipengele cha kukusanya na kugawa mirabaha. Wanamuziki wakiongozwa na mtafiti kutoka Afrika ya Kusin martin Cuff leo walifanya warsha hiyo katika ukumbi wa Nyumbani Lounge. Warsha ilifungwa na Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya habari, Utamaduni na Michezo aliyesifu jitihada za wanamuziki kuweza kufanya kikao kama hiki.
Sunday, October 20, 2013
PRODUCERS WAHUDHURIA SEMINA YA HAKIMILIKI
Pamoja na kuwa leo ni siku ya Jumapili, watu wengi huwa wanapumzika, maproducer kadhaa wamejikusanya na kuhudhuria semina ya Hakimiliki iliyoendeshwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime. Semina hiyo iliyofanyika katika jengo la Sayansi na Teknolojia iliwawezesha Producers kufahamu nini maana ya Hakimiliki na vilevile kupata elimu ya awali kuhusu yaliyomo katika sheria ya Hakimiliki ya hapa nchini
JULIUS NYAISANGAH.... UNCLE J.,,.SUPER TALL HATUNAE TENA
MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA UNATOA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KWA NDUGU , RAFIKI, NA WANAMUZIKI WALIOWAHI KUFANYA KAZI NA MTANGAZAJI MKONGWE JULIUS NYAISANGA, ALIYEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO 20 OKTOBA, 2013 KATIKA HOSPITALI YA MAZIMBU MOROGORO.
MUNGU AMLAZE PEMA JULIUS, KAZI YAKO ULIOIFANYA KATIKA TASNIA YA MUZIKI HAITAFUTIKA
MUNGU AMLAZE PEMA JULIUS, KAZI YAKO ULIOIFANYA KATIKA TASNIA YA MUZIKI HAITAFUTIKA
Wednesday, October 16, 2013
Je unapenda muziki wa Mashujaa Band?
Bendi ya Mashujaa imetengeneza ukurasa wao ambapo unaweza sasa kusikiliza nyimbo zao nyingi kutoka hapo. Je wewe au bendi yako mnanyimbo katika mtandao wa intanet, basi tutumie anwani au wimbo kupitia musicnettz@gmail.com ili tuuweke katika blog yetu.
Kwa kusikiliza nyimbo za Mashujaa ingia HAPA upate nyimbo zao
Kwa kusikiliza nyimbo za Mashujaa ingia HAPA upate nyimbo zao
Thursday, October 3, 2013
KIPINDI CHA MIKIKI MIKIKI YA MUZIKI KUANZA KURUKA JUMAMOSI HII SAA 12:30 JIONI TBC RADIO YA TAIFA
BAADA ya kupata ufadhili wa BEST AC kwa kupitia Tanzania Heritage Project, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TMN), utaanza kurusha vipindi vya radio kupitia Radio TBC Taifa. Vipindi hivyo ambavyo vitaendeshwa na mwanamuziki na mwenyekiti wa Mtandao John Kitime. Kipindi cha kwanza kitaanza na kuangalia biashara ya muziki kwa kutegemea viingilio ilivyo na kama kweli inalipa na kitashirikisha kwa kukusanya maoni kutoka kwa wasikilizaji. Kipindi hiki ni mwanzo wa vipindi vingi vya redio vitakavyohusu muziki kama utamaduni, taaluma na kama biashara. Karibuni tusikilize na tutoe maoni kupitia blog hii na ukurasa wa facebook https://www.facebook.com/wanamuzikiwa.tanzania Wanamuziki wa Tanzania tuna uwezo kama wanamuziki wengine duniani lakini tuna matatizo makubwa ya mpangilio katika tasnia yetu
Monday, September 30, 2013
WANAMUZIKI WAWILI WA TEMEKE WAFARIKI LEO
Msanii wa kundi la WATEULE, Malik Ahmed Moa maarufu kwa jina la Mack2B amefariki dunia leo. Msiba utakuwa Yombo kwa wazazi wake Mack 2B alikuwa producer na msanii wa raga, amefariki kutokana na ugonjwa wa figo uliokuwa unamsumbua muda mrefu
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMIN
**********************************************************
Mwanamuziki mpiga bezi wa siku nyingi Joseph Watuguru
amefariki mchana huu katika hospitali ya Amana. Watuguru amewahi kupigia bendi nyingi zikiwemo Bantu Group ya Hamza Kalala, Magoma Moto Sound, African Stars ile ya mwanzo kabisa Mchinga Sound, na katika siku zake za mwisho alikuwa bendi ya WK Sound ya Temeke. Watuguru aliwahi kushiriki katika bendi iliyotengenezwa na Producer kutoka Norway Sigbjorn Nedland iliyoitwa Mradi Group akiwa na akina Bob Rudala, Keppy Kiombile, John Saggati, Bizimana Ntavyu, Anania Ngoliga na wengine. Alikuwa mpiga bezi mzuri na pia fundi mitambo wa kutegemewa
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMIN
**********************************************************
Joseph akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wakati akiwa African Stars |
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA
Tuesday, September 17, 2013
MTANDAO KUANDAA SEMINA YA WANAMUZIKI KUHUSU UKUSANYAJI NA UGAWAJI WA MIRABAHA KATIKA KAZI ZA MUZIKI
Kamati ya kuratibu mradi unaoendelea wawa Utafiti wa hali halisi ya ukusanyaji na ulipaji wa mirabaha leo imekaa na kupanga kufanya semina ya awali kwa baadhi ya wanamuziki ili kuanza kuelimisha taratibu za ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Semina hiyo itafanyika katika muda wa wiki mbili. Semina itahusisha wanamuziki wa aina tofauti za muziki, dansi, taarab, bongoflava, hiphop, gospel muziki asili nakadhalika
Sunday, September 15, 2013
MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA UFADHILI WA BEST AC
MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA umepata ufadhili kutoka
Business Environment Strengthening of Tanzania (BEST – AC) ili kuweza kufanya
utafiti wa kina kupata ukweli wa hali halisi ya ukusanyaji na ugawaji wa
mirabaha ya muziki unaofanywa na COSOTA, na baada ya hapo kutoa ushauri wa nini
kifanyike ili kuboresha hali iliyopo. Madhumuni ya mradi huu ni kuwezesha
kufanya mabadiliko katika tasnia ya muziki ambayo yatatengeneza nafasi za ajira
zenye tija ili kuwezesha tasnia kutoa mchango wake katika pato la Taifa, na
kukuza sifa ya nchi kutokana na wasanii wengi wenye sifa waliomo hapa nchini.
Mradi utaangalia sheria zilizopo zinazohusu ugawaji wa
mirabaha ya wanamuziki na mambo mengine yote yanayohusiana na shughuli ya
ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha na kupendekeza taratibu za kuboresha hali.
Kamati za fedha na utawala zitaanza kazi wiki hii ili
kuweza kufanikisha zoezi hili ambalo linatakiwa likamilike katika muda wa mwezi
mmoja. Wanamuziki watashirikishwa katika semina ambayo itafanyika katika wiki chache zijazo. Mtafiti kutoka Afrika ya Kusini amekwisha ingia mkataba na Mtandao ili
kufanya kazi hiyo.
TANZANIA MUSICIANS NETWORK SECURES A GRANT FROM BEST AC
TMN has secured a grant from Business Environment
Strengthening of Tanzania (BEST – AC) to conduct a study to assess the existing
arrangement under COSOTA in collection of music royalties and use the findings
to provide clear and precise recommendations for appropriate interventions to advocate
for change in collection system for the music industry growth of Tanzania.
The objective of the project is to
initiate appropriate interventions that will support the Tanzania music
industry to create the much needed jobs, subsequently taxes flowing back to
government and enhancing the image of country built up from the talented
artistes from institutionalized support for the industry.
The Project will specifically carry
out a study to assess the legal framework regulating the distribution of
royalties to musicians and other owners of copyright in works and all matters
connected thereto and provide a report with recommendations. The report will be used to engage with
government to address the inefficiencies established with a purpose to strengthen
the musicians' bargaining power in controlling the usage of their copyright.
The project is aims to examine the music industry landscape
and the struggle on copyright protection, combating piracy, legislative
instruments to implement copyright and managing music rights; mandate,
transparency, fairness in collection and timely payment of royalties to
artists. The purpose is to seek
government’s support to have clear distinguished roles of the Copyright Society
of Tanzania (COSOTA) as a Government copyright office from that of collecting
organization. The project should identify the important stake holders in the
industry such as Publishers, Distributors, Manufacturers of musical works,
lyrists, arrangers, producers, executive producers and such others and their
roles in the Royalties payment chain.
Sunday, September 8, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)