HAKIKA Diamond kiboko yao. TAMUNET inatoa hongera kwa Diamond Platnumz kwa kushinda MTV
European Music Awards (MTVEMA), katika tukio lililofanyika Milan Jumapili hii tarehe 25 October wakati Tanzania ikipiga kura
kutafuta viongozi wake wa miaka mitano ijayo. Tuzo hili hufanyika katika miji mbalimbali ya Ulaya
kila mwaka, na washindi huchaguliwa kwa kura za wapenzi kutoka dunia nzima. Mcheza
filamu kutoka India na ambae pia alikuwa Miss World mwaka 2000 Priyanka Chopra pia alishiriki akiwa kundi
moja na Diamond, katika ‘ category ‘ ya
Worldwide Act : "Africa/ India". Pamoja na uwingi wa watu wa
India , Diamond Platnumz ameweza kupata kura nyingi zaidi na kuongeza sifa wake
mwenyewe binafsi na kwa Taifa. Hongera tena Diamond
Priyanka Chopra |