Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete usiku wa Ijumaa, Oktoba 23, 2015, amewateua Makatibu Wakuu wanne
wapya wa wizara mbali mbali. Kati Makatibu Wakuu hao Rais amemteua
aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel, kuwa Katibu Mkuu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Sihaba
Nkinga kuhamishiwa Wizara ya Wanawake, Jinsia
na Watoto kutoka Wizara ya Habari. Hakika hii ni habari nzuri kwa wasanii katika kipindi hiki tunapongojea matokeo ya uchaguzi Mkuu. Profesa ni mchapa kazi wa ukweli, ni kati ya mambo mazuri makubwa yaliyotokea katika Wizara hii kwa muda mrefu
No comments:
Post a Comment