KATIKA mkutano uliofanyika leo kwenye makao makuu ya MSONDO, wanamuziki waliweza kupata taarifa ya namna BIMA YA AFYA inavyofanya kazi. Maelezo hayo yaliyotolewa kwao na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki, (TAMUNET) John Kitime. Baada ya mkutano huo wanamuziki hao walikubaliana kuanza kuhakikisha kila mmoja wao ana Bima ya Afya mara moja
Tuesday, October 20, 2015
Sunday, October 11, 2015
DIAMOND AZOA TUZO TATU AFRIMMA AWARDS
- Eddy Kenzo (Uganda)
- Jaguar (Kenya)
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Bebe Cool (Uganda)
- Jackie Gosse (Ethiopia)
- Ali Kiba (Tanzania)
- Dynamq (Sudan)
- Khadija Kopa (Tanzania)
- Aster Aweke (Ethiopia)
- Victoria Kimani (Kenya)
- Vanessa Mdee (Tanzania)
- Juliana Kanyamozi (Uganda)
- STL (Kenya)
- Irene Ntale (Uganda)
Best Newcomer
- Kiss Daniel (Nigeria)
- Pappy Kojo (Ghana)
- Korede Bello (Nigeria)
- Lil Kesh (Nigeria)
- Mz Vee (Ghana)
- Fabregas (Congo)
- Ommy Dimpoz (Tanzania)
- Bebi Philip (Ivory Coast)
- mpata Wapi’ (Tanzania)
- Sauti Sol – ‘Sura Yako’ (Kenya)
- Cassper Nyovest – ‘Doc Shabaleza’ (South Africa)
- Flavour (Nigeria)
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Sarkodie (Ghana)
- Cassper Nyovest (South Africa)
- Davido (Nigeria)
- Fally Ipupa (Congo)
- Eddy Kenzo (Uganda)
- Wizkid (Nigeria)
- Yemi Alade (Nigeria)
- Bucie (South Africa)
- Bracket ft. Diamond & Tiwa Savage – ‘Alive’ (Nigeria & Tanzania)
- Irene Ntale – ‘Woman’ (Uganda)
- Sarkodie ft. Castro – ‘Adonai’ (Ghana)
- Jose Chameleon – ‘Bwerere’ (Uganda)
- Psquare ft. Dave Scott – ‘Bring it On’ (Nigeria)
- Eddy Kenzo – ‘Be Happy’ (Uganda)
Thursday, October 8, 2015
TAMUNET YAFANYA MKUTANO
Wa kwanza kushoto, Abraham Kapinga (Tanzanite Band) Katibu Mkuu wa Mtandao |
Toka kushoto-Innocent Nganyagwa, Ally Jamwaka(Sikinde), Rashid Pembe(Mark Band), Davidi Ng'asi(Mwalimu wa muziki) |
Abdul Salvador |
Ilionekana kuwa kasi ya kujiunga na bima ya afya bado ni ndogo, na moja ya sababu ni ukosefu wa uelewa kuhusu umuhimu wa Bima na namna ya utendaji wa Bima. Mikakati ilipangwa kukabili hali hiyo.
Taaarifa ya Tamasha ilikwisha anza kusambazwa kutumia mitandao ya Facebook, vikundi vya Whatsapp Blog hii na taarifa za mdomo. Tayari wasanii kadhaa walionyesha nia ya kushiriki. Mtandao uangalie namna ya kwezesha wanamuziki hawa kufanikiwa katika ushiriki wa tamasha hili.
Ilikuablika kuwa katika wiki mbili zijazo kufanyike kikao cha kuangalia utekelezaji wa kushiriki katika kuboresha elimu ya muziki. Mwanamuziki na Mwalimu wa Muziki David Ng'asi alipewa jukumu la kuja na andiko la awali la mkakati huo.
Monday, October 5, 2015
Tuesday, September 29, 2015
MWANAMUZIKI WA DOUBLE M SOUND AVAMIWA NA VIBAKA MSUMBIJI
Taarifa
zimetufikia kwenye ofisi ya Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, kutoka kwa Muumin Mwinjuma 'Kocha' zikieleza kuwa mmoja wanamuziki wake
aliokuwa nao katika safari ya Msumbiji amepata mkasa wa kuibiwa na kuumizwa muda mfupi kabla ya onyesho kumalizika rasmi. Kwa kadri ya maelezo ya Muumini, bendi ilipiga katika
kitongoji cha Nanyupu, ambapo show hiyo ilikuwa ni ya pili katika mahala hapo
baada ya bendi kufanya show ya kwanza siku ya Jumapili tarehe 20 Septemba.
Kitongoji hiki ni makazi ya wachimbaji wa madini ya Ruby ambapo wengi wao ni
Watanzania, pia kuna wenyeji ambao ni Wamsumbiji, Wasenegali na Wanaijeria
kadhaa. Kwa kuwa Watanzania ni wengi, mara baada ya show ya kwanza, wakazi walimuomba aliyeipeleka bendi wakapige
show nyingine, nae hakukataa kwani alikuwa katengeneza pesa vizuri, hivyo bendi
ilikwenda kupiga tena siku ya Alhamisi tarehe 24 Septemba, siku ya Idd. Wakati
wa kupiga wimbo wa mwisho, muimbaji Amina hakuwa na kazi hivyo alishauriana na madansa watangulie kwenye gari. Madansa waliondoka kwa pamoja na kuelekea
kwenye gari lakini Amina ambaye pia ni katibu wa bendi alipanda kwanza jukwaani
kumuaga Muumini. Aliposhuka kwenye jukwaa kuelekea kwenye gari kundi la vijana
wakaanza kumsemesha Kiswahili nae akawa anajisikia kama yuko na ndugu zake.
Vijana wale ghafla wakamvamia na kuanza kumpiga makofi na kumburula na kumpora
mkoba wake uliokuwa na passport yake na ya mpiga drum na fedha za Msumbiji zenye thamani ya 150,000/-. Wenzie walipofika
kumsaidia tayari vibaka wale walikuwa wameshaingia gizani. Na mara moja dansi lilivunjwa ili
kumpeleka mji wa Pemba kwa matibabu.
Bendi
ilifanya maonyesho mengine mawili katika mji wa Pemba na kuona kuna haja ya kurudi kwanza nyumbani ili Amina apone vizuri, wakati wanamuziki wengine wanategemea kurudi nchini wakati wowote, Amina ataendelea kuwa Msumbiji kwa wiki moja zaidi ili apate matibabu zaidi. Pia bendi inakuja kujipanga kwa safari ndefu zaidi
inayotegemewa muda si mrefu.
Amina akiwa na mwanamuziki mwenzie Kupaza |
Monday, September 21, 2015
DOUBLE M YAANZA KUTIKISA MSUMBIJI
KUNDI la Double M chini ya Muumin Mwinyjuma, limealikwa Msumbiji kwa mwezi mzima, na katika wakati huo kundi litashiriki katika sherehe za miaka 51 ya Vita vya Ukombozi wa nchi hiyo. Wanamuziki hawa ambao ni wanachama wa Mtandao wa Wanamuziki walipitisha barua yao ya taarifa ya kwenda huko na hivyo Mtandao ukatoa taarifa Baraza la sanaa La Taifa kama inavyostahili. Waliomo katika msafara huo ni pamoja na kiongozi wa kundi Muumin Mwinyjuma, maarufu kwa jina la KOCHA, na wanamuziki wengine 16.
1.
Mwinjuma Muumin Buguza- Kiongozi wa
Bendi-Muimbaji
2.
Omary Kisila- Kinanda
3.
Hamza S Waninga- Drums
4.
Imma Keffa –Bass Guitar
5.
Emmanuel Namwinga- Rhythm guitar
6.
Amina R Juma –Muimbaji
7.
Veronica D Buzeri –Dansa
8.
Neema Kawambwa-Dansa
9.
Stamili
Hamis –Dansa
10. Greyson
Semsekwa – Rapper
11. Sharey
Aboubakar-Muimbaji
12. Revina
Mzinja -Dansa
13. Salma Shaaban –Dansa
14. Afande
Muhamada-Fundi Mitambo
15. Omary
Maulid –Fundi Mitambo
16. Saleh Kupaza-Muimbaji
17. Dogo Rama-Muimbaji
Habari toka TAMUNET- Mtandano wa Wanamuziki Tanzania
Tuesday, September 15, 2015
Monday, September 14, 2015
MWANAMUZIKI KUIBURUZA KAMAPUNI YA SIMU MAHAKAMANI
MWANAMUZIKI wa Abuja, nchini
Nigeria Omenuwoma Okson Dovie, aka Baba 2010, ameamua kuipeleka mahakamani
kampuni ya simu ya MTN kwa kukiuka
haki zake za hakimiliki katika nyimbo zake nne, zikiwemo "Gentleman
"Ometena", "Twisted" and "Unity Song."
Dovie anaituhumu kampuni
hiyo kwa kubadili nyimbo hizo kuwa caller tunes/ring tones, na kuziuza bila
ruksa yake kwa miaka mitatu mfululizo. Nyimbo hizo ziko kwenye album yake aliyoitoa
2005 ikiwa na jina
"Twisted”.
Barua ya mwanasheria wake
Rockson Igelige, imeitaka MTN
kumlipa mteja wake naira milioni
500 (Tshs 5,455,000,000), kwa matumizi ambayo hayakuruhusiwa na yenye kupunguza thamani ya nyimbo
zake. Na pia alitoa siku 14 ambazo MTN lazima iwe imekamilisha malipo au kujibu
hoja.
Mshauri wa sheria wa MTN
amekubali kuwa kapokea barua na kuwa kampuni hiyo inaliangalia swala hilo.
Wakati huohuo Igelige amesema wameishauri Kamisheni ya Hakimiliki ya Nigeria
kuwafungulia mashtaka MTN, wakati nao wakifungua mashtaka kwa upande wa
mwanamuziki.
Wednesday, September 2, 2015
WANAMUZIKI WACHANGAMKIA KUPATA BIMA YA AFYA
Hamis Mnyupe wa Msondo akijaza fomu za Bima ya Afya |
Kinuka, mpiga bezi wa kujitegemea na producer akijaza fomu za Bima ya Afya |
Goddy Mkude mpiga gitaa wa B Band akijaza fomu za Bima ya Afya |
Geophrey Kumburu mpiga kinanda na producer akiwa na kadi yake ya Bima aliyoipata karibuni |
Simon Mwamkinga mpiga kinanda na kiongozi wa Rungwe Band akiwa na kadi yake ya Bima ya Afya aliyoipata karibuni |
Subscribe to:
Posts (Atom)