Tuesday, September 15, 2015
Monday, September 14, 2015
MWANAMUZIKI KUIBURUZA KAMAPUNI YA SIMU MAHAKAMANI
MWANAMUZIKI wa Abuja, nchini
Nigeria Omenuwoma Okson Dovie, aka Baba 2010, ameamua kuipeleka mahakamani
kampuni ya simu ya MTN kwa kukiuka
haki zake za hakimiliki katika nyimbo zake nne, zikiwemo "Gentleman
"Ometena", "Twisted" and "Unity Song."
Dovie anaituhumu kampuni
hiyo kwa kubadili nyimbo hizo kuwa caller tunes/ring tones, na kuziuza bila
ruksa yake kwa miaka mitatu mfululizo. Nyimbo hizo ziko kwenye album yake aliyoitoa
2005 ikiwa na jina
"Twisted”.
Barua ya mwanasheria wake
Rockson Igelige, imeitaka MTN
kumlipa mteja wake naira milioni
500 (Tshs 5,455,000,000), kwa matumizi ambayo hayakuruhusiwa na yenye kupunguza thamani ya nyimbo
zake. Na pia alitoa siku 14 ambazo MTN lazima iwe imekamilisha malipo au kujibu
hoja.
Mshauri wa sheria wa MTN
amekubali kuwa kapokea barua na kuwa kampuni hiyo inaliangalia swala hilo.
Wakati huohuo Igelige amesema wameishauri Kamisheni ya Hakimiliki ya Nigeria
kuwafungulia mashtaka MTN, wakati nao wakifungua mashtaka kwa upande wa
mwanamuziki.
Wednesday, September 2, 2015
WANAMUZIKI WACHANGAMKIA KUPATA BIMA YA AFYA
Hamis Mnyupe wa Msondo akijaza fomu za Bima ya Afya |
Kinuka, mpiga bezi wa kujitegemea na producer akijaza fomu za Bima ya Afya |
Goddy Mkude mpiga gitaa wa B Band akijaza fomu za Bima ya Afya |
Geophrey Kumburu mpiga kinanda na producer akiwa na kadi yake ya Bima aliyoipata karibuni |
Simon Mwamkinga mpiga kinanda na kiongozi wa Rungwe Band akiwa na kadi yake ya Bima ya Afya aliyoipata karibuni |
TAMUNET YAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA BIMA YA AFYA
Mwaka
2004, John Kitime ambaye kwa sasa ndie Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki
Tanzania (Tanzania Musicians Network-TAMUNET) alihudhuria Mkutano Mkuu wa
Shirikisho la Muziki Duniani –International Federation of Musician (FIM).
Katika mkutano huo moja ya maazimio ya mkutano ule ilikuwa kila nchi ihakikishe
inaanzisha utaratibu wa Bima ya Afya kwa wanamuziki wake.
Mara
baada ya kurudi Tanzania, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa TAMUNET, Kitime
alianza kufuatilia uwezekano wa kupata huduma ya Bima hiyo kwa wanamuziki. Kwa
bahati mbaya hakukuwa na njia yenye gharama nafuu ya malipo ya BIma hiyo ambayo
mwanamuziki wa kawaida angeweza kuyamudu. Kulikuweko na kampuni ambayo iliweza
kutoa huduma hiyo kwa gharama ya dola 300 kwa mwaka kwa mwanamuziki mmoja.
Kampuni nyingine za Bima zilizotembelewa hazikuonyesha ushirikiano katika jambo
hilo. TAMUNET iliwasiliana pia na mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa katika kipindi
hico mfuko ulikuwa hauna mamlaka ya kuhudumia watu waliokuwa nje ya ajira ya
serikali na mashirika ya umma. TAMUNET iliwasiliana na Mganga Mkuu wa Serikali,
ambaye alishauri TAMUNET kuwasiliana na NGO moja ambayo ilikuwa na makao yake
makuu Sinza, na kweli NGO hiyo ilikubali kuwa ingeweza kutoa huduma ya Bima ya
Afya kwa wanamuziki kwa gharama ya shilingi 3000/- tu kwa mwezi, lakini huduma
hii ilikuwa ni kwa hospitali kadhaa tu jijini Dar es Salaam. Hilo nalo
lilionekana ni bora kuliko kukosa kabisa, lakini muda mfupi baadae NGO hiyo
ilisema haishughuliki tena na huduma hiyo bali imeelekeza nguvu zake kwa watoto
wa mtaani. Hapo ilifuatia miaka kadhaa ambayo hakukuweko na njia yoyote
iliyowezekana ya kupata huduma hiyo. TAMUNET ilijaribu pia kuwasiliana na
mifuko mingine, lakini kila mara iligonga ukuta aidha kwa ahadi ambazo zilikuwa
zikipigwa kalenda bila kutekelezwa.
Mwaka
2015 hatimae ndipo mlango umefunguka, Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa NHIF,
uliitarifu TAMUNET kuwa umeanzishwa mpango wa Bima kwa Kikoa ambao
ungewawezesha wanamuziki nao kupata Bima ya Afya kwa gharama nafuu. TAMUNET
iliuchangamkia mpango huo kwa kuwa imekuwa ajenda ya chama hiki kwa miaka zaidi
ya kumi.
Wanamuziki
wanachama wa TAMUNET tayari wameanza kufaidi huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka
mzima, hii ni baada ya kulipia shilingi 76,800/-. Mpango huu utaondoa aibu ya
wanamuziki kuchangiwa fedha za matibabu kila wanapougua, kwani itakuwa busara
kwa wapenzi na washabiki wa muziki kuchangia mwanamuziki wanaempenda apatiwe
Bima ya Afya kuliko kumchangia fedha za matibabu ya muda mfupi. Baadhi ya
wanamuziki ambao tayari wana bima za afya chini ya mpango huu ni Louiza Nyoni,
Abdul Salvador, Rashid pembe, na wengine wengi wamekwisha anza taratibu za
kupata huduma hii.
Wasanii katika semina kuhusu BIma Ya Afya iliyofanyika BASATA karibuni |
Muwezeshaji Catherine kutoka Mfuko wa Taifa wa BIma ya Afya akitoa maada katika semina ya wasanii kuhusu Bima ya Afya |
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makond aliyekuwa mgeni rasmi katika semina ya Bima ya Afya kwa wasanii |
Mwenyekiti wa TAMUNET akipokea kadi za kwanza za Bima ya Afya za wanamuziki, katika ofisi za Mfuko wa BIma ya Afya wa Taifa. |
John Kitime akiwa na kadi yake ya BIma ya Afya aliyoipata karibuni |
Kadi za Bima ya Afya za wanamuziki mbalimbali |
Louiza Nyoni akionyesha kadi yake mpya ya Bima ya Afya |
Thursday, May 21, 2015
VANESSA MDEE AFIWA NA DADAKE MKUBWA
Anna na Vanessa ni watoto wa marehemu Sammy Mdee, aliyekuwa mwandishi mkongwe aliyewahi kuongoza gazeti la Daily News, Katibu wa Mwalimu Nyerere na pia mkurugenzi wa kituo cha AICC. Mazishi ya Anna yatakuwa Same Jumamosi mchan saa 8.
Mungu Amlaze Pema Anna Mdee
Wednesday, April 29, 2015
MTANDAO WA WANAMUZIKI WAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA HUDUMA YA BIMA YA AFYA
Wanamuziki wanachama wa Tanzania Musicians Network -TAMUNET_ sasa wanaweza kujiunga na mpango nafuu wa Bima ya Afya baada ya chama chao kuingia katika makubaliano na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF.
WAnamuziki walikuwa ni kundi mojawapo ambalo limekuwa na tatizo kubwa la kupata matibabu bora kutokana na kukosa taratibu za bima ya afya, jambo ambalo ni njia ya kisasa na ya uhakika wa kupata matibabu bora kwa kila binadamu.
Katika kikao cha viongozi wa chama hicho leo kamati maalumu imeundwa kuratibu mpango huu ambapo kamati hii itakuwa ikiandikisha wanachama wote wanaohitaji kupata huduma hii muhimu. Kamati itakuwepo kila Jumatano kuanzaia saa nne mpaka saa tisa katika ofisi za Mtandao zilizopo katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa jirani na hospitali ya Mvungi katika barabara ya kuelekea mahakama ya Kinondoni, chumba namba 148. Pia unaweza kuwasiliana na Mweka hazina Asha Salvador kupitia simu namba 0687378797 kwa maelezo ya ziada
WAnamuziki walikuwa ni kundi mojawapo ambalo limekuwa na tatizo kubwa la kupata matibabu bora kutokana na kukosa taratibu za bima ya afya, jambo ambalo ni njia ya kisasa na ya uhakika wa kupata matibabu bora kwa kila binadamu.
Katika kikao cha viongozi wa chama hicho leo kamati maalumu imeundwa kuratibu mpango huu ambapo kamati hii itakuwa ikiandikisha wanachama wote wanaohitaji kupata huduma hii muhimu. Kamati itakuwepo kila Jumatano kuanzaia saa nne mpaka saa tisa katika ofisi za Mtandao zilizopo katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa jirani na hospitali ya Mvungi katika barabara ya kuelekea mahakama ya Kinondoni, chumba namba 148. Pia unaweza kuwasiliana na Mweka hazina Asha Salvador kupitia simu namba 0687378797 kwa maelezo ya ziada
Friday, August 29, 2014
MTANDAO WA MUZIKI WASHIRIKI SAFARI YA KUTEMBELEA BUNGE LA KATIBA DODOMA
Hii ndio PRESS RELEASE iliyosomwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa
Wanamuziki siku ya 27 August 2014 kwa waandishi wa habari jijini
Dodoma. Ndugu waandishi wa habari, katika mfumo wa sanaa wa nchi
yetu wasanii wamegawanyika katika makundi makuu manne, ambayo yanaendeshwa na
Mashirikisho ya vyama mbalimbali vya sanaa. Mashirikisho hayo ni;
i.
Shirikisho la Filamu TAFF
ii.
Shirikisho la Sanaa za Maonyesho
iii.
Shirikisho la Sanaa za Ufundi
iv.
Shirikisho la Muziki
Tuliopo mbele
yenu ni viongozi na wasanii kutoka vyama na Mashirikisho ya sanaa yaliyotajwa
hapo juu. Kundi hili limekuwepo hapa Dodoma kwa siku mbili kukutana na wajumbe
wa Bunge la katiba ili kufuatilia maslahi ya wasanii katika katika mchakato wa Katiba mpya ya nchi yetu Tanzania. Hii si mara ya kwanza kwa kundi hili
kukutana na Wabunge wa Bunge hili la Katiba, bali hii ni mara ya tatu kundi
hili limefika hapa Dodoma. Mchakato uliotufikisha leo hapa ulianza kwa
Mashirikisho kukutana na kutengeneza Baraza la katiba ambapo mashirikisho
yalitoa mapendekezo kadhaa yaliyofikishwa kwenye Tume ya Katiba. Lakini
hakukuweko jambo lolote lililotokana na mawazo hayo ambalo lilichukuliwa na
kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba. Mashirikisho yalituma majina 36, (tisa
kutoka kila shirikisho) katika
kupendekeza wawakilishi katika Bunge la Katiba. Katika hili mjumbe mmoja,
Paulynus Raymond Mtenda aliteuliwa na hivyo kubeba uwakilish wa kundi zima la
wasanii Tanzania. Siku ya Ijumaa 14/2/2014 Mashirikisho yote ya sanaa
yalikutana BASATA na kumkabidhi rasmi mapendekezo yao Mbunge huyu, ili
ahakikishe kundi hili haliachwi katika mchakato wa Katiba.
Muda mfupi baada ya hapo kundi hili lilikuja Dodoma, na
kukutana na Wabunge mbalimbali wa Bunge hili la Katiba, tulikutana na Wabunge
wa kambi zote na kufanya nao mikutano mingi, ambayo mingine ilifika mpaka saa
nane za usiku. Wabunge wa kambi zote walionekana kuunga mkono hoja za wasanii
na tulianza mawasiliano mbalimbali na Wabunge yakiwemo ya ana kwa ana, simu na
email, Wabunge wakihitaji documentation mbalimbali kuhusiana na mapendekezo
yetu katika Katiba mpya. Katika
kipindi hiki tulikuja wakati hata Mwenyekiti wa Bunde la Katiba hajachaguliwa.
Ujumbe huu ulikuja tena …. Na hii ni mara ya tatu.
Ujumbe huu toka awali ulikuwa na maombi mawili tu.
i.
Wasanii kutambuliwa kama kundi maalumu kama
yalivyotambuliwa makundi ya wakulima wafugaji, wavuvi. Sababu za kutaka
kutambuliwa huku, ni kuwa kundi hili ni kubwa kuliko hata makundi mengine
yaliyotajwa hapo juu. Takwimu za Baraza la Sanaa la Taifa za mwaka 2006
zinaonyesha kuwa wasanii nchini walikuwa kiasi cha milioni 6. Leo ni mika
minane imepita na si siri kuwa kundi hili limekuwa na hivyo kukaribia robo ya
Watanzania, si haki kutolitambua.
ii.
Milikibunifu (Intellectual Property) itajwa
rasmi kama moja ya aina za mali zinazohitaji kulindwa katika katika Katiba
Tumekuja pia na mapendekezo ya namna ya kuingiza hoja zetu
hizi zilizosahauliwa, hatujaja na Ibara mpya kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyoonekana
kutuhumu katika magazeti ya juzi. Mapendekezo yetu ni kuwa katika Ibara ya 30
iongezwe aya moja tu ya. Na ibara
ya 37 inayoongelea Haki ya ulinzi wa mali, itambue kuwa pamoja na mali
zinazohamishika na zisizohamishika, pia kuna mali isiyoshikika.
Tumepata faraja kubwa kupokelewa na Bunge hili, Na kuweza kuzunguka kwenye kamati 9 kwa
hizi siku mbili kukumbusha mapendekezo yetu haya, ambayo hayabebi tu wasanii
bali pia wavumbuzi wa kiteknolojia, kibailojia, wasomi watafiti, na wananchi
wote kwa ujumla. Pendekezo letu la pili ni muhimu katika kulinda na kuendeleza
uchumi wa Tanzania. Na sisi kama Watanzania tumeona ni muhimu kutumia nafasi
hii adimu kuhakikisha tunatoa mawazo yetu katika Bunge hili kwani tusipotumia
nafasi hii tutakuwa hatukujitendea haki wala kuvitendea haki vizazi vijavyo vya
Tanzania.
SIMON MWAKIFWAMBA-SHIRIKISHOLA FILAMU TANZANIA (TAFF)
JOHN KITIME….MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA (TAMUNET)
Saturday, August 16, 2014
UMUHIMU WA MILIKIBUNIFU KUTAJWA KATIKA KATIBA MPYA
Katika Rasimu ya Katiba kumetajwa ulinzi wa mali, lakini ni wazi mali
hizi ni zile zililzozoeleka katika akili za watu mali zinazohamishika na
zisizohamishika. Kuna aina ya tatu ya mali ni ile inayotokana na
ubunifu, na kwa sasa ndio mali inayolindwa zaidi na mataifa mengi, kwani
ndio inayoleta ugunduzi wa madawa, mitambo, teknolojia, sanaa, na
maendeleo ya kila aina. Hii huitwa Milikibunifu. Ni muhimu kutajwa kama
zilivyofanya nchi nyingine ambazo zimefaidika sana na kulinda
milikibunifu za wananchi wake.....
Milikibunifu au Intellectual Property Rights ni haki
anazopewa mbunifu ili kulinda hali za mali yake ambayo haishikiki. Mali hii
iyokanayo na ubunifu ni muhimu kuilinda kwani matokeo ya mali hii huwa faida
kubwa kwa jamii. Milikibunifu ndizo haki ambazo huwalinda wagunduzi wa
maendeleo katika teknolojia, madawa ya binadamu mifugo na kilimo, njia
mbalimbali za kuongeza ubora na ufanisi wa teknolojia. Milikibunifu imegawanywa
katika makundi mbalimbali ya ulinzi;
i.
Patent – (Hataza) hii ni njia ya kulinda na kusajili
uvumbuzi mbalimbali wa kiteknolojia. Mfano vifaa vya kuvunia mazao kwa haraka
zaidi, au kulima kwa haraka zaidi, vifaa vya uvuvi wa haraka, vifaa vya
mawasiliano na vifaa vyovyote ambavyo vitaongeza thamani ya maisha yetu. Katika
nchi kama Korea ya Kusini ulinzi wa Milikibunifu uliwekwa katika Katiba kuanzia
baada ya vita ya pili ya dunia kwa kufusts mfumo wa Katiba ya Marekani na ulinzi huo umeifanya wananchi wake
ambao ni wabunifu kuweza kuja naubunifu ambao unatikisa dunia vifaa kama
Samsung, Daewoo, KIA, LG ni matokeo ya ulinzi wa kikatiba wa wa Milikibunifu
ii.
Trademarks – (Alama za Biashara ) Alama za
biashara huweza kufikia hatua ambapo zikawa na thamani kubwa kwani huweza
kuaminika. Ili kulinda zisitumiwe hovyo au hata kuibiwa na wenye uwezo zaidi
hulindwa na sheria za kulinda alama hizi. Kwa mfano Cocacola, Vodacom, Dell, na
hapa kwetu Azam, ni majina ya bidhaa ambazo zina aminika, na hivyo kuwa na
dhamani kubwa japo hazishikiki, nazo ni sehemu ya mali ambazo hazishikiki lakini zina thamani
kubwa
iii.
Industrial designs – Hizi ni haki wanazopewa
wale wenye ubunifu wa kuweza kufanya usanii wenye kuboresha muonekano wa kitu
ambacho tayari kimeshagunduliwa. Kwa mfano kila mtu ana simu ya mkononi lakini
muonekano wa simu mbalimbali shape nap engine hali ya kuwa ni ya ku slide au
kufungua au kupokea moja kwa moja ni matokeo ya design, pia vitu kama design za
nguo, viatu , kiti ulichokalia makochi magari, vyote hivyo ndivyo matokeo ya
industrial designs. Kazi za ubunifu huo ni muhimu kulindwa kwani huwa na
thamani kubwa sana, kwa mbunifu na kwa mchango wake kwa nchi.
iv.
Geographical Indication – Huu ni utambulisho wa
wapi chanzo cha mali husika. Kwa mfano mvinyo kutoka Dodoma, Dodoma Wine ni
mzuri na hivyo huitwa Dodoma Wine bila kulinda hili, watu watachukua mvinyo huu
na kuupa hata jina jingine ukaitwa South African wine na hivyo kuiba haki
wanazostaili kupata wakulima wa Dodoma, kutambuliwa kwa jina hili kutasababisha
kutakiwa zaidi kwa wine hii duniani na hivyo kuweza kufanya hata Dodoma kuwa
Wine City jambo ambalo linawezekana lakini nchi haijatambua umuhimu huu. Pia
kuna mchele wa Kyela, Dagaa wa Kigoma na vitu kama hivi ambavyo havipatikani
popote duniani kasoro sehemu iliyotajwa.
Nchi kama Uswiss imejenga jina miaka mingi ya utengenezaji wa saa bora
hivyo saa ikiandikwa Swiss made huwa inajulikana ni bora na huwa gharama zaidi,
Sigara kutoka Cuba, Cuban Cigars ni bei kubwa kwani hazipatikani popote kasoro
Cuba, au mvinyo maarufu kama Champagne, ambao hutoka jimbo la Champagne
Ufaransa, umejijengea sifa kubwa duniani na kuwa na bei kubwa sana kiasi cha
kwamba si rahisi kwa mtu wa kipato cha kawaida kununua. Harusi zetu hutumia
Sparkling Wine na kuiita Shampeni.
v.
Hakimiliki na Hakishiriki – Hizi ni haki
zinazolinda kazi za kisayansi na kisanii. Computer Programs, Data, Utunzi wa
vitabu, miswaada, hotuba, uchoraji, muziki, kazi za usonara, picha za mnato na
filamu, uchongaji na kadhalika. Kazi hizi zimekuwa ni chanzo cha utajiri mkubwa
kwa watu binafsi na Mataifa. Katika nchi ya Marekani kazi za Hakimiliki na
Hakishiriki ni za pili katika uchangiaji wa pato la Taifa. Ripoti ya WIPO ya
2010 ilionyesha kuwa katika nchi ya Tanzania kazi za hakimiliki na Hakishiriki
zilichangia asilimia 4.3 ya pato la taifa, karibu mara mbili ya mchango wa
Madini!. Katika mwaka 2009 kazi za hakimiliki zilitengenza aslimia 5.63 ya
ajira nchini, ikiwa juu ya mchango wa Afya (4.23), Biashara na mambo ya Fedha
Real estate, &Business Service(2.37), Ujenzi (1.38),Usafirishaji na
Mawasiliano (0.92), Umeme, Gas na maji (0.91), Madini (0.89)
Pamoja na umuhimu huu, Katiba
inataja mali zinazoshikika tu-Zinazohamishika na zisizohamishika, hivyo mali
hizi ambazo zimeonyesha kuleta maendeleo makubwa kwa nchi ambazo wakati wa
Uhuru tulikuwa sawa kwa mfano Thailand, India, Malasia, Korea kusini ambazo
zote zimetuacha mbali ni kwa ajili ya ulinzi wa mali hizi zisizoshikika ambazo
ndizo pia zinawezesha mazingira ya kuingiza fedha nyingi za uwekezaji kutoka
kwa wenye pesa na kuanzisha viwanda vyenye mali ya asili ya hapa. Nchi zote
zinazoendelea ambazo ziliwahi kuona umuhimu wa kuweka kipengele cha miliki
bunifu katika Katiba yake mapema, zimeweza kupata maendeleo ya haraka kama
nilivyotaja hapo juu.
Mifano ya nchi nyingine….
Marikani ni nchi moja wapo ambapo ulinzi wa Milikibunifu
umewezesha maendeleo makubwa katika sanaa na teknolojia,
·
U.S. Constitution. Article I, Section 8
provides: "The Congress shall have Power … To promote the Progress of
Science and useful Arts, by securing for limited Times to Authors and Inventors
the exclusive Right to their respective Writings and Discoveries."
·
The Constitution of Malaysia, which is the
supreme law of Malaysia, was adopted on 31 August 1957. Since then, the
Constitution has been amended many times, most recently in 2009.
The Constitution contains provisions on intellectual property.
In the Legislative Lists (List I-Federal List) of the Ninth Schedule, the Constitution gives the federal government the power to enact laws relating to patents, designs, inventions, trade marks and mercantile marks, copyrights (Section 8 (e)).
The Constitution contains provisions on intellectual property.
In the Legislative Lists (List I-Federal List) of the Ninth Schedule, the Constitution gives the federal government the power to enact laws relating to patents, designs, inventions, trade marks and mercantile marks, copyrights (Section 8 (e)).
·
Article 22 ya Katiba ya South Korea inasema (1)
All citizens shall enjoy freedom of learning and the arts. (2) The rights of
authors, inventors, scientists, engineers, and artists shall be protected by
Act
Thursday, July 10, 2014
MWENYEKITI WA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA, AFUNDISHA WAALIMU WA NURSERY MUZIKI
Ili kupata kizazi kitakachoweza kupenda muziki na kutumia vifaa vya muziki ni vizuri kuhakikisha unapata waalimu bora wa muziki. Na ni vizuri kuanza kufundisha watoto wakati wakiwa bado wadogo. Kufanikisha hili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania-John Kitime, akishirikiana na Chuo cha Montesori cha Waalimu wa Shule za Nursery, wameanza mpango wa kuwawezesha waalimu kujifunza japo chombo kimoja cha muziki, na pia njia rahisi za kutunga nyimbo za watoto. Waalimu wanafunzi watarekodi nyimbo walizotayarisha na kuondoka nazo baada ya kumaliza masomo ili waweze kuzitumia kufundishia wanafunzi kwenye vituo vyao.
Subscribe to:
Posts (Atom)