KIONGOZI WA BENDI |
Wednesday, July 31, 2013
MWENYEKITI NA MWEKA HAZINA WA TANZANIA MUSICIANS NETWORK WAKITIA SAINI MAKUBALIANO YA UTAFITI KUHUSU HALI YA MUZIKI TANZANIA
BEST AC imeuwezesha Mtandao wa muziki Tanzania kufanya utafiti wa kina na kisha kuja na majibu ya matatizo ya wanamuziki wa Tanzania hasa katika swala la Hakimiliki. Katika makubaliano hayo Mtandao utapata dola 49,000, zitakazolazimika kupatikana kwa ripoti katika muda wa miezi mitatu ijayo
Hans muwakilishi wa BEST AC |
Mwenyekiti wa Mtandao John Kitime akitia sahihi makubaliano hayo kwa niaba ya Mtandao |
Asha Warsama Salvador Mweka hazina akitia sahihi kwa niaba ya Mtandao |
KIKAO CHA MUHIMU CHA WANAMUZIKI CHAFANYIKA BASATA LEO
Wanamuziki chini ya chombo chao kipya Tanzania Musicians Network (Mtandao wa Wanamuziki Tanzania) leo wamekutana katika ukumbi wa BASATA na kufanya mkutano amba katika mkutano huo wameongelea mambo muhimu yafuatayo;
Mwenyekiti wa Mtandao John Kitime aliwaeleza hali halisi ya Mtandao ambao kwa kipindi hiki umejipanga kufanya kazi kadhaa baada ya kulipa ada zake zote BASATA na hivyo kuwa halali wameweza kuingia katika makubaliano na BEST AC ambapo Mtandao utapewa Dola 49,000 USD, katika awamu tatu, ili kuweza kufanya utafiti wa tatizo linalokabili sekta ya muziki Tanzania hasa katika nyanja ya Hakimiliki. Fedha hizi ni zamradi ambao utachukua miezi mitatu ambapo mtafiti au watafiti watafanya research ya kutafuta nini chanzo cha matatizo ya hakimiliki katika tasnia ya muziki, na pia kifanyike nini, na ripoti ipatikane ya kuuuwezesha Mtandao kuongea na wadau wengine katika muziki , ikiwemo serikali, vyombo vya utangazaji, vyombo vingine kama BASATA, TCRA, COSOTA na kadhalika ili kuwezesha wanamuziki wa Tanzania wanufaike na kazi zao. Pamoja na ripoti hiyo kutakuweko na semina kubwa ya wanamuziki kuboresha ripoti hiyo na hatimae kuweza kuwa na mkutano wa wanamuziki na wadau waliotajwa hapo juu. Pamoja na hayo yote Mtandao utatengeneza vipindi kadhaa vya redio vitakavyoanza kurushwa karibuni ambavyo vitayaweka wazi mazingira yaliyomo katika tasnia hii na namna ya kuyakabiri.
Pamoja na maelezo hayo wanamuziki walitaarifiwa kuwa Mtandao umepata ofisi katika maeneo ya Kinondoni jirani na American Chips katika mtaa yalipo Makao Makuu ya CHADEMA. Kodi ya ofisi imekwisha lipia na baadhi ya samani zimenunuliwa, japo wanamuziki waliombwa kama wana samani yoyote wanayoweza kujitolea itapokelewa kwa mikono miwili.
Wanamuziki walitaarifiwa kuwa kupatikana kwa ofisi kutarahisisha uandikishaji wa wanachama wapya. Malipo ya wanachama yapo kama ifuatavyo.
Fomu za uanachama- 1000/-
Kiingilio - 20,000/-
Ada -5,000/- kwa mwaka, fomu zitaanza kupatikana JUmatatu ijayo katika ofisi mpya ya chama.
Wanachama walitaarifiwa kuwa anwani ya email ya cham ni musicnettz@gmail.com na blog hii ilitambulishwa. Wanamuziki waliombwa kuitumia blog hii kama gazeti lao la kuelezea shughuli zao zote bila kuwa na woga.
Tuesday, July 30, 2013
MKUTANO WA WANAMUZIKI WOTE BASATA
Mkutano wa wanamuziki kuweko Jumatano tarehe 31 July 2013, BASATA, kuanzia saa nne hadi saa sita. Katika mkutano huo ajenda kubwa itakuwa kutambulisha Mtandao upya kwa wanamuziki na kupeabna taarifa za hali halisi, na kisha kupeana majukumu, wanamuziki wa kila aina aina ya muziki tunakaribishwa.
Thursday, July 25, 2013
MWANAMUZIKI WA ZIMBABWE CHIWONISO MARAILE AFARIKI DUNIA
Mwanamuziki Chiwoniso Maraile wa Zimbabwe amefariki dunia baada ya kuugua kwa matatizo ya mapafu. Chiwoniso ambaye amewahi kuja Tanzania na kurekodi katika studio za Marimba Studio akifanya kazi na wanamuziki wa hapa nchini kama Karola Kinasha, Norma Bikaka, Bob Rudala, alikuwa mahiri sana kwa chombo chake cha Mbira na kuimba pia.
Mungu amlaze pema mwenzetu
Mungu amlaze pema mwenzetu
Tuesday, May 28, 2013
SOMA GAZETI LA INTERNATIONAL FEDERATION OF MUSICIANS HAPA
INGIA HAPA KUSOMA GAZETI LA INTERNATIONAL FEDERATION OF MUSICIAN BONYEZA
Tanzania Musicians Network chaanza upya kwa kishindo
-->
Tanzania Musicians Network au Mtandao wa Wanamuziki Tanzania ni chombo
kilichosajiliwa BASATA 2004,
kilianza kwa nguvu mwaka 2006 na kufikia kuwa na wanachama 400, lakini kilipata pigo mwaka 2007 kwa jengo
ambalo lilikuwa ofisi ya chama hiki kuvunjwa na kulibadilishwa matumizi na
mwenye mali, cham kikadorora.
Kutokana na umuhimu wa chombo hiki na kutokana na pengo la
chombo chenye kukusanya wanamuziki wote na washiriki wengine kwenye muziki,
wakiwemo, wanamuziki, wachezaji( stage show), sound engineers wa studio na wa
muziki ‘live’, producers, managers na wadau wengine wa aina hiyo, imelazimika kukifufua tena chombo hiki muhimu. Lengo kuu la
mtandao huu ni kuwa chama cha wafanyakazi wanamuziki (Musicians Union). Chombo chenye kulea na kukuza
shughuli hii kuwa yenye taratibu zinazompasa mfanya kazi wa kazi hizi, kama inavyokuwa katika ulimwengu sehemu nyingine.Chombo hiki ni mwanachama hai wa Shirikisho la Wanamuziki Duniani (FIM).
Kwa sasa ajenda iliyo mbele ni bima ya afya ya wanamuziki. Si siri kuwa
tatizo la matunzo na huduma za wanamuziki na wafanyakazi wengine wa tasnia hii
ni gumu pale afya zao zinapokuwa na matatizo, hivyo tayari viongozi wameshakuwa
na mazungumzo ya awali na moja ya vyombo vya bima ya afya na kinachosubiriwa ni
wanamuziki kujiunga na chombo hiki ili kuweza kuanzisha taratibu hizi.
Pamoja na malengo haya Mtandao huu utaendesha semina na
warsha kwa ajili ya wanamuziki wanachama katika Nyanja mbalimbali za mambo ya
muziki. Katika kipindi hiki hiki tayari mtandao umewezesha wafadhili kufadhili
utafiti kuhusu matatizo yaliyomo katika biashara ya muziki jambo ambalo
litawezesha wafadhili kufadhili miradi itakayobuniwa katika kurekibisha hali
hiyo ngumu.
Tunakaribisha maombi ya uwanachama, unaweza kuonyesha nia
kwa kutuma jina na anwani yako katika inbox ya ukurasa facebook Wanamuziki wa Tanzania au kupitia
anwani ya musicnettz@yahoo.com na utaweza kuwapewa maelezo ya ziada. Tuma jina lao, jinsia,
mahala uliko, namba ya simu, anwani ya email na taaluma unayoshiriki, …. UMOJA
NI NGUVU
Subscribe to:
Posts (Atom)