Wednesday, March 5, 2014
MTANDAO KUFANYA WARSHA YA VIONGOZI WA BENDI
Kamati ya uongozi ya Mtandao wa wanamuziki(TAMUNET), leo imefanya kikao na katika yaliyopangwa na kufanya warsha ya siku moja ya viongozi wa bendi kujadili changamoto mbalimbali zinazozikuta bendi katika zama za sasa. Tarehe ya warsha hii inategemea makubaliano na BASATA ambao watakuwa kiungo muhimu katika warsha hii. Lakini warsha hii lazima itakuwa mwezi huu March kabla ya mkutano mkubwa wa wanamuziki mara baada ya warsha hiyo.
Wednesday, February 19, 2014
HARAKATI ZA WASANII KUPATA NAFASI KATIKA KATIBA MPYA—3
Kamati ilipata
mapokezi ya heshima kubwa kutoka kwa wabunge wa CHADEMA, ambapo Wabunge sita wa CHADEMA walikaa na kuwasikiliza
wawakilishi hawa wa wasanii wakieleza mapendekezo yao katika Katiba kuhusiana
na wasanii. Wasanii wana ajenda mbili,
1. Kundi la wasanii kutajwa katika
Katiba kuwa ni kundi rasmi kutokana na ukubwa wa kundi hili nchini, kama yalivyotajwa makundi ya wakulima, wafugaji, wavuvi na kadhalika, pia mchango
wake katika ajira ya vijana na ukubwa wa pato linalotokana na kundi hili,
ambalo kutokana na kutokutambuliwa linapotea katika mifuko ya watu na kukosesha
wasanii na Taifa pato kubwa.
2. Wasanii walitaka ubunifu ulindwe kwanza kwa
ulinzi wa Milikibunifu kutajwa rasmi katika katiba na hivyo kuwezesha sheria bora kutungwa na pia
utekelezaji wa ulinzi wa kazi zao uweko kama ilivyo katika mali nyingine za
wananchi wengine. Kikao cha saa moja na nusu kilikuwa cha mafanikio na kuwa na
faida kwa pande zote mbili.
Wasanii hawakulala mapema kwani walimalizia siku na
kuhamia eneo jingine ambapo
walikuwa na kikao na Mheshimiwa Mbunge wa Donge ambae pia ni Mwenyekiti wa
Ummoja wa Vijana wa CCM Taifa Mheshimiwa Sadifa, ambapo kikao hicho kiliisha saa saba
ya usiku.
HARAKATI ZA WASANII KUPATA NAFASI KATIKA KATIBA MPYA—2
Ili kuwezesha kufika Dodoma na kuwakilisha mapendekezo
yaliyokusanywa na Mashirikisho, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET),
waliwezesha idadi ya wasanii 12 kufika na kuishi Dodoma. Wasanii hao wakiwemo
viongozi toka Mashirikisho wameza kufika Dodoma na kuanza kazi mara moja ya
kukutana na Wabunge mbalimbali, na kufanya nao mikutano na mazungumzo ya papo
kwa popa na kwa kweli mapokezi yamekuwa ya hali ya juu yanayoleta tumaini kubwa
kwa wote waliofika huku. Wasanii
waliomo katika msafara huu muhimu kwa tasnia na Taifa ni
1.
Simon Mwakifwamba – Rais, Shirikisho la Filamu
(TAFF)
2.
John Kitime – Mwenyekiti, Tanzania Musicians
Network (TAMUNET)
3.
Bishop Hiluka – Katibu Mkuu, TAFF
4.
Yobnesh ‘Batuli’ Yusuph –Msanii/FilmProducer
5.
Samwel ‘Braton’ Mbwana –Tanzania Urban Music
Association (TUMA)/Music Producer
6.
Paul ‘P Funk’ Matthysse – Mwenyekiti, Tanzania
Producers Association/ Producer
7.
Kulwa ‘Dude’ Kikumba – Msanii/ Producer
8.
Abdul Salvador –Katibu Mkuu, Shirikisho la
Muziki Tanzania (TMF)
9.
Adrian Nyangamale – Rais, _Shirikisho la Sanaa
za Ufundi Tanzania
10. Mh.
Paulynus Raymond Mtendah – Mbunge Bunge la katiba
11. Yvonne
Cherie ‘Mona Lisa’ –Msanii
12. Seleman
Hamisi- Producer toka Dodoma
13. Ernest
Omalla – Mshauri wa TAFF na TAMUNET
Mara baada ya kufika Dodoma Mbunge wa Bunge la Katiba Mh.
Maria Sarungi aliwezesha kufanyika kikao cha kwanza kati yake na wasanii ambapo
pia Mh. Paul Makonda alikuweko. Mazungumzo yalifanyika ambapo msafara ukaweza
kueleza mapendekezo yake kupitia mshauri mtaalam Ernest Omalla na mwanamuziki
John Kitime. Mkutano huu wa saa mbili ulikuwa wenye matumaini makubwa.
Msafara
ulitoka hapa na kwenda kwenye mkutano mwingine ambapo msafara tena ulitoa
maelekezo yake kwa waheshimia Wabunge watatu, Mh Paul Mtanda, Mh.Livingstone na
Mh Murtaza Mangungu, na tena mkutano huo ulikuwa ni mzuri wenye mafanikio
mazuri sana. Mheshimiwa Mtanda aliahidi atajitahidi kukusanya wajumbe wa kamati
ya Ustawi wa Jamii ili kuweza kupata uelewa wa maombi ya wasanii.
Kamati haikuishia hapo kwani jioni Mheshimiwa Makonda aliiwezesha kundi hili kukutana
na wabunge wengine wakiwemo Mh.
Ahmed Salum, Mh. William Mgeja na Mh. Mpina Mbunge wa Kisesa.
Katika hali ya
kuonyesha kuwajali wasanii wabunge wa Dar es Salaam waliwafuata wasanii katika
Lodge waliofikia na kuwasikiliza lile ambalo walikuwa wakilitaka. Mheshimiwa
Idd Azan na Mh. Abbas Mtemvu waliwakilisha wabunge wa Dar es Salaam na kuwa na
saa nzima ya kuwasikiliza wasanii hawa katika malengo yao
mawili waliyotaka yaingie katika Katiba.
Tuesday, February 18, 2014
HARAKATI ZA WASANII KUPATA NAFASI KATIKA KATIBA MPYA—1
MH. PAULYNUS RAYMOND MTENDA |
Kuna
mashirikisho manne ya sanaa nchini ambayo ni Shirikisho la muziki, Shirikisho
la Filamu, Shirikisho la Sanaa za maonyesho na Shirikisho la Sanaa za Ufundi.
Ulipotolewa wito wa makundi maalumu kutoa mapendekezo yao katika Katiba
Mpya, Mashirikisho yalikaa kama
Kamati za katiba na kuja na mapendekezo kadhaa kwenye katiba, mapendekezo hayo
licha ya kupokelewa na Tume ya Katiba hakuna kilichoingizwa katika Rasimu ya
Katiba.
Baada ya hapa ndipo wito ukatolewa wa kupendekeza majina ya
watu watakaoingia katika Bunge la Katiba, Mashirikisho yote yalipendekeza
majina mbalimbali. Hatimae jina la Paulynus Raymond Mtenda lilirudi kama ndie
mwakilishi aliyeweza kutoka katika kundi la Watu wenye malengo yanayofanana .
Tarehe 14, February 2014 viongozi wa Mashirikisho walikutana
BASATA kumpongeza Mbunge Mteule huyu na kumkabidhi rasmi mapendekezo ambayo
yalipelekwa awali kwenye Tume ya Katiba ili aweze kuyapendekeza katika katiba
mpya.
KAIMU KATIBU MTENDAJI WA BASATA AKIMKABIDHI MAPENDEKEZO YA MASHIRIKISHO MBUNGE MTEULE |
Pamoja na mapendekezo hayo Shirikisho la Filamu TAFF, na
Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET), pia walikuja na hoja mbili muhimu
nazo ni;
1.
Kutambuliwa kwa wasanii kama ni kundi maalumu katika
Katiba, kama yalivyoweza kutambuliwa makundi ya wakulima, wavuvi na
wafanyakazi. Sababu kubwa za kuja na hoja hii ni kutokana na ukweli
unaopatikana katika tafiti mbalimbali.
Wasanii ni wengi sana, katika ripoti ya BASATA ya mwaka 2006, idadi ya
wasanii nchini wakati huo ilikuwa kiasi cha milioni sita. Kwa kuwa ni miaka
minane sasa imepita toka wakati wa ripoti hiyo kuna kila sababu ya kuamini kuwa
kundi hilo limekuwa kubwa zaidi. Sababu nyingine ni ukweli kuwa wasanii
wanasababisha ajira kwa kundi kubwa la watu, wakiwemo wafanyakazi wa vyombo vya
utangazaji, wafanya kazi katika biashara ya matangazo, wasambazaji, wafanya
biashara ndogondogo, (machinga) na wengine wengi waliomo katika mnyororo wa
biashara hii ikiwemo, maproducer, mameneja, mafundi mitambo, watayarishaji wa
maonyesho na kadhalika. Hivyo sanaa si utamaduni tu bali ni kazi yenye mapato
makubwa. Ripoti ya WIPO ya mwaka 2012 imeonyesha kuwa kazi zitokanazo na
Hakimiliki huingiza fedha nyingi zaidi katika uchumi wa Taifa kuliko MADINI,
jambo ambalo ni wazi wengi wanaosikia kwa mara ya kwanza hushangaa kwa kuwa
kelele za mapato ya Madini ni kubwa sana katika jamii wakati hakuna
anaelalamika kuhusu mapato kutokana na hii raslimali ya nchi inayoitwa sanaa.
Ripoti hiyo ya WIPO pia ilionyesha kuwa sekta ya Hakimiliki inaajiri watu wengi
zaidi kuliko, sekta za Madini, gesi, maji, Ustawi wa Jamii, Afya, Usafirishaji.
Hivyo ni sekta ambayo ina umuhimu sana katika uchumi wa Taifa ikiwa italindwa inavyostahili.
2.
Hoja ya pili ilikuwa kuwekwa rasmi kipengele cha
kutambuliwa kwa Miliki Bunifu na kuhakikishiwa ulinzi na uendelezaji wa
shughuli za Milikibunifu katika Katiba. Wasanii hutegemea maendeleo yao na
uboreshaji wa kazi zao kwa kulindwa kwa Hakimiliki. Lakini ingekuwa ni uchongo
wa mawazo kudai ulinzi wa Hakimiliki peke yake. Hivyo lengo ni kupata ulinzi wa
Miliki Bunifu ambayo itasababisha kulinda haki za wasanii ,wabunifu, wagunduzi,
wanasayansi na wabunifu wa teknolojia mbalimbali. Kuna mifano kila mara hutolewa ambayo
inaonyesha nchi kadhaa ambazo wakati nchi hii inapata uhuru, uchumi wa nchi
hizo ulikuwa sawa na uchumi wetu, kama vile Malasia, Thailand na Korea Kusini ambazo
kutokana na ulinzi na uendelezaji
wenye mipango wa Miliki Bunifu nchi hizo zimewezesha uchumi wao kukua na kuwa katika
uchumi bora duniani.
Saturday, February 15, 2014
MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA OFISI MPYA
Baada ya kuwa na ofisi ya muda ambayo ilikuwa katika mazingira magumu kikazi hatimae Mtandao wa Muziki Tanzania umepata ofisi mpya yenye hadhi ya kuitwa ofisi ya wanamuziki. Ofisi hiyo iko katika barabara inayoelekea Mahakama ya Kinondoni, katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa. Ofisi iko ghorofa ya 3 chumba na 148. Wanamuziki mnakaribishwa kuitumia ofisi hiyo
Monday, January 27, 2014
Friday, December 13, 2013
GURUMO 53 - TAMASHA LA KUSTAAFU MUZIKI MUHIDIN MAALI GURUMO
Wanamuziki kadhaa wenye heshima
katika muziki wa dansi watakuweko katika Tamasha la Gurumo 53, ambalo ni
tamasha la kustaafu muziki mwanamuziki mkongwe Muhidin Maalim Gurumo. Kati ya
wanamuziki watakao panda jukwaani ni
Komandoo Hamza Kalala, Mzee Makassy, wanamuziki nyota waliowahi kutamba
na bendi ya DDC Mlimani Park , Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe,
Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa,
Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande. Pia wapulizaji wakongwe Majengo na King
Maluu watakuweko na wote kwa pamoja wataporomosha show kubwa Jumamosi
hii ndani ya TCC Club Chang’ombe. Wakali hao jana Alhamisi walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano
watakazopiga katika tamasha hilo. Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club
ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa
wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo zilizofanyiwa
mazoezi ni pamoja na “Selina”
utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka
kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa). Tamasha
la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka
katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi
kustaafu muziki. Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia,
Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga. Burudani zingine zitakazokuwepo siku
hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga
Pepeta.
Wednesday, November 20, 2013
MWENYEKITI WA MTANDAO ATOA MADA YA UTAFITI WA MALIPO YA MIRABAHA
Katika Jukwaa la Sanaa ambalo huweko kila Jumatatu katika ukumbi wa BASATA , wiki hii Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime alichambua utafiti uliokamilika karibuni uliofanywa na mtafiti Martin Cuff kwa niaba ya Mtandao kwa ufadhili wa BEST AC. Utafiti huo ambao umo kwenye kitabu chenye kurasa 84 unachambua hali halisi ya Hakimiliki Tanzania, na mapungufu yake na kisha kutoa mapendekezo ya kuboresha hali hiyo kwa manufaa ya wenye Hakimiliki na tasnia ya muziki kwa ujumla. Kitabu cha utafiti huo kitapatikana baada ya muda si mrefu.
Thursday, November 7, 2013
UBALOZI WA MAREKANI WAKABIDHI VITABU 800 KWA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA
Ubalozi wa marekani nchini Tanzania, leo hii 7/11/2013
umemkabidhi vitabu vya Hakimiliki zaidi ya 800 Mwenyekiti wa Tanzania
Musicians Network, John F Kitime katika hafla iliyofanyika katika maktaba ya
Ubalozi huo uliopo jijini Dar es Salaam. Kitabu hicho chenye lugha mbili
Kiswahili na Kiingereza kimetungwa na Alex Perullo ambaye ni Associate Professor wa Anthropology na African Studieskatika chuo cha
Bryant Marekani. Hiki ni kitabu cha pili cha aina hii kutungwa na Profesa huyu,
cha kwanza alikisambaza kupitia Ubalozi huu huu miaka kumi iliyopita. Kwa vile
kina lugha mbili kitabu hiki kina majina mawili kinaitwa Artistic Rights na
Haki za Kisanii. Ni kitabu cha kurasa 98 ambacho kimejaa maelezo mengi kuhusu
haki za wasanii, wasanii watakao kisoma watafaidika sana.
Mtandao wa Muziki Tanzania, utakisambaza
kitabu hiki katika taasisi mbalimbali muhimu na pia utawapa bure wanachama wake
nakala za kitabu hiki muhimu. Dibaji ya kitabu hiki imeandikwa na John Kitime.
Subscribe to:
Posts (Atom)