Saturday, February 15, 2014

TANZANIA MUSICIANS NETWORK GETS NEW OFFICES

THE NETWORK has shifted to the new offices this week. The shift had long been awaited as the former premisses were not at all conducive to musicians, as the office space was very small and airless most of the time. Musicians and others in the industry are warmly welcome to the new offices



MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA OFISI MPYA

Baada ya kuwa na ofisi ya muda ambayo ilikuwa katika mazingira magumu kikazi hatimae Mtandao wa Muziki Tanzania umepata ofisi mpya yenye hadhi ya kuitwa ofisi ya wanamuziki. Ofisi hiyo iko katika barabara inayoelekea Mahakama ya Kinondoni, katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa. Ofisi iko ghorofa ya 3 chumba na 148. Wanamuziki mnakaribishwa kuitumia ofisi hiyo



Friday, December 13, 2013

GURUMO 53 - TAMASHA LA KUSTAAFU MUZIKI MUHIDIN MAALI GURUMO

Wanamuziki kadhaa wenye heshima katika muziki wa dansi watakuweko katika Tamasha la Gurumo 53, ambalo ni tamasha la kustaafu muziki  mwanamuziki mkongwe Muhidin Maalim Gurumo. Kati ya wanamuziki watakao panda jukwaani ni  Komandoo Hamza Kalala, Mzee Makassy, wanamuziki nyota waliowahi kutamba na bendi ya DDC Mlimani Park , Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe, Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa, Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande. Pia wapulizaji wakongwe Majengo na King Maluu watakuweko na wote kwa pamoja wataporomosha show kubwa Jumamosi hii ndani ya TCC Club Chang’ombe. Wakali hao  jana Alhamisi walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano watakazopiga katika tamasha hilo. Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo zilizofanyiwa mazoezi ni  pamoja na “Selina” utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa). Tamasha la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi kustaafu muziki. Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia, Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga. Burudani zingine zitakazokuwepo siku hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga Pepeta.

Wednesday, November 20, 2013

MWENYEKITI WA MTANDAO ATOA MADA YA UTAFITI WA MALIPO YA MIRABAHA

Katika Jukwaa la Sanaa ambalo huweko kila Jumatatu katika ukumbi wa BASATA , wiki hii Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime alichambua utafiti uliokamilika karibuni uliofanywa na mtafiti Martin Cuff kwa niaba ya Mtandao kwa ufadhili wa BEST AC. Utafiti huo ambao umo kwenye kitabu chenye kurasa 84 unachambua hali halisi ya Hakimiliki Tanzania, na mapungufu yake na kisha kutoa mapendekezo ya kuboresha hali hiyo kwa manufaa ya wenye Hakimiliki na tasnia ya muziki kwa ujumla. Kitabu cha utafiti huo kitapatikana baada ya muda si mrefu.




















Thursday, November 7, 2013

UBALOZI WA MAREKANI WAKABIDHI VITABU 800 KWA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA


Ubalozi wa marekani nchini Tanzania, leo hii 7/11/2013 umemkabidhi  vitabu vya Hakimiliki zaidi ya 800 Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network, John F Kitime katika hafla iliyofanyika katika maktaba ya Ubalozi huo uliopo jijini Dar es Salaam. Kitabu hicho chenye lugha mbili Kiswahili na Kiingereza kimetungwa na  Alex Perullo ambaye ni Associate Professor wa Anthropology na African Studieskatika chuo cha Bryant Marekani. Hiki ni kitabu cha pili cha aina hii kutungwa na Profesa huyu, cha kwanza alikisambaza kupitia Ubalozi huu huu miaka kumi iliyopita. Kwa vile kina lugha mbili kitabu hiki kina majina mawili kinaitwa Artistic Rights na Haki za Kisanii. Ni kitabu cha kurasa 98 ambacho kimejaa maelezo mengi kuhusu haki za wasanii, wasanii watakao kisoma watafaidika sana.
Mtandao wa Muziki Tanzania, utakisambaza kitabu hiki katika taasisi mbalimbali muhimu na pia utawapa bure wanachama wake nakala za kitabu hiki muhimu. Dibaji ya kitabu hiki imeandikwa na John Kitime.




Wednesday, October 30, 2013

WANAMUZIKI WA TANZANIA WAFANYA WARSHA KUBWA







Martin Cuff

 Warsha kubwa ya siku moja ya wanamuziki wa tanzania yafanyika pale Nyumbani Lounge. Wanamuziki kutoka kila aina ya muziki walikuweko. katika warsha hii iliyoomgozwa na mtafiti Martin Cuff ilikuwa ni kutoa report ya utafiti wake kuhusu hali halisi ya utekelezaji wa Ukusanyaji na ugawaji wa Mirabaha. Wanamuziki walipata nafasi ya kuchangia  na kutoa mapendekezo. Ripoti nzima kutoka katika wiki mbili zijazo. Utafiti ulifanywa na Martin Cuff na kuongozwa na Tanzania Musicians Network kwa ufadhili wa BEST AC.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ndie aliyefunga warsha hii kwa kusifu jitihada hii ya wanamuziki kufanya utafiti. Katika kukutana huku na Naibu Katibu mkuu wanamuziki walioingia mkataba na kampuni mojawapoya ringtones walilalamika kuwa waliingia mkataba wa miaka kumi na kampuni hiyo na baada ya hapo kampuni hiyo haikutaka hata kujibu barua zao, Naibu Katibu Mkuu aliwaita wahsanii hao ofisini kwake ili kuona cha kufanya, pia alimtaka Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network John Kitime amuone ili waongelee tatizo la TBC kutokulipa mirabaha na kuatafuta suluhu.