Saturday, February 15, 2014
MTANDAO WA MUZIKI TANZANIA WAPATA OFISI MPYA
Baada ya kuwa na ofisi ya muda ambayo ilikuwa katika mazingira magumu kikazi hatimae Mtandao wa Muziki Tanzania umepata ofisi mpya yenye hadhi ya kuitwa ofisi ya wanamuziki. Ofisi hiyo iko katika barabara inayoelekea Mahakama ya Kinondoni, katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa. Ofisi iko ghorofa ya 3 chumba na 148. Wanamuziki mnakaribishwa kuitumia ofisi hiyo
Monday, January 27, 2014
Friday, December 13, 2013
GURUMO 53 - TAMASHA LA KUSTAAFU MUZIKI MUHIDIN MAALI GURUMO
Wanamuziki kadhaa wenye heshima
katika muziki wa dansi watakuweko katika Tamasha la Gurumo 53, ambalo ni
tamasha la kustaafu muziki mwanamuziki mkongwe Muhidin Maalim Gurumo. Kati ya
wanamuziki watakao panda jukwaani ni
Komandoo Hamza Kalala, Mzee Makassy, wanamuziki nyota waliowahi kutamba
na bendi ya DDC Mlimani Park , Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe,
Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa,
Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande. Pia wapulizaji wakongwe Majengo na King
Maluu watakuweko na wote kwa pamoja wataporomosha show kubwa Jumamosi
hii ndani ya TCC Club Chang’ombe. Wakali hao jana Alhamisi walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano
watakazopiga katika tamasha hilo. Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club
ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa
wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo zilizofanyiwa
mazoezi ni pamoja na “Selina”
utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka
kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa). Tamasha
la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka
katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi
kustaafu muziki. Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia,
Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga. Burudani zingine zitakazokuwepo siku
hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga
Pepeta.
Wednesday, November 20, 2013
MWENYEKITI WA MTANDAO ATOA MADA YA UTAFITI WA MALIPO YA MIRABAHA
Katika Jukwaa la Sanaa ambalo huweko kila Jumatatu katika ukumbi wa BASATA , wiki hii Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki John Kitime alichambua utafiti uliokamilika karibuni uliofanywa na mtafiti Martin Cuff kwa niaba ya Mtandao kwa ufadhili wa BEST AC. Utafiti huo ambao umo kwenye kitabu chenye kurasa 84 unachambua hali halisi ya Hakimiliki Tanzania, na mapungufu yake na kisha kutoa mapendekezo ya kuboresha hali hiyo kwa manufaa ya wenye Hakimiliki na tasnia ya muziki kwa ujumla. Kitabu cha utafiti huo kitapatikana baada ya muda si mrefu.
Thursday, November 7, 2013
UBALOZI WA MAREKANI WAKABIDHI VITABU 800 KWA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA
Ubalozi wa marekani nchini Tanzania, leo hii 7/11/2013
umemkabidhi vitabu vya Hakimiliki zaidi ya 800 Mwenyekiti wa Tanzania
Musicians Network, John F Kitime katika hafla iliyofanyika katika maktaba ya
Ubalozi huo uliopo jijini Dar es Salaam. Kitabu hicho chenye lugha mbili
Kiswahili na Kiingereza kimetungwa na Alex Perullo ambaye ni Associate Professor wa Anthropology na African Studieskatika chuo cha
Bryant Marekani. Hiki ni kitabu cha pili cha aina hii kutungwa na Profesa huyu,
cha kwanza alikisambaza kupitia Ubalozi huu huu miaka kumi iliyopita. Kwa vile
kina lugha mbili kitabu hiki kina majina mawili kinaitwa Artistic Rights na
Haki za Kisanii. Ni kitabu cha kurasa 98 ambacho kimejaa maelezo mengi kuhusu
haki za wasanii, wasanii watakao kisoma watafaidika sana.
Mtandao wa Muziki Tanzania, utakisambaza
kitabu hiki katika taasisi mbalimbali muhimu na pia utawapa bure wanachama wake
nakala za kitabu hiki muhimu. Dibaji ya kitabu hiki imeandikwa na John Kitime.
Wednesday, October 30, 2013
WANAMUZIKI WA TANZANIA WAFANYA WARSHA KUBWA
Martin Cuff |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ndie aliyefunga warsha hii kwa kusifu jitihada hii ya wanamuziki kufanya utafiti. Katika kukutana huku na Naibu Katibu mkuu wanamuziki walioingia mkataba na kampuni mojawapoya ringtones walilalamika kuwa waliingia mkataba wa miaka kumi na kampuni hiyo na baada ya hapo kampuni hiyo haikutaka hata kujibu barua zao, Naibu Katibu Mkuu aliwaita wahsanii hao ofisini kwake ili kuona cha kufanya, pia alimtaka Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network John Kitime amuone ili waongelee tatizo la TBC kutokulipa mirabaha na kuatafuta suluhu.
Subscribe to:
Posts (Atom)