Friday, August 29, 2014

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI YA WASANII KATIKA BUNGE LA KATIBA...........











MTANDAO WA MUZIKI WASHIRIKI SAFARI YA KUTEMBELEA BUNGE LA KATIBA DODOMA




Hii ndio PRESS RELEASE  iliyosomwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki siku ya  27 August 2014 kwa waandishi wa habari jijini Dodoma. Ndugu waandishi wa habari, katika mfumo wa sanaa wa nchi yetu wasanii wamegawanyika katika makundi makuu manne, ambayo yanaendeshwa na Mashirikisho ya vyama mbalimbali vya sanaa. Mashirikisho hayo ni;
i.                Shirikisho la Filamu TAFF
ii.              Shirikisho la Sanaa za Maonyesho
iii.             Shirikisho la Sanaa za Ufundi
iv.             Shirikisho la Muziki
 Tuliopo mbele yenu ni viongozi na wasanii kutoka vyama na Mashirikisho ya sanaa yaliyotajwa hapo juu. Kundi hili limekuwepo hapa Dodoma kwa siku mbili kukutana na wajumbe wa Bunge la katiba ili kufuatilia maslahi ya wasanii katika katika mchakato wa  Katiba mpya ya nchi yetu Tanzania.  Hii si mara ya kwanza kwa kundi hili kukutana na Wabunge wa Bunge hili la Katiba, bali hii ni mara ya tatu kundi hili limefika hapa Dodoma. Mchakato uliotufikisha leo hapa ulianza kwa Mashirikisho kukutana na kutengeneza Baraza la katiba ambapo mashirikisho yalitoa mapendekezo kadhaa yaliyofikishwa kwenye Tume ya Katiba. Lakini hakukuweko jambo lolote lililotokana na mawazo hayo ambalo lilichukuliwa na kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba. Mashirikisho yalituma majina 36, (tisa kutoka kila shirikisho)  katika kupendekeza wawakilishi katika Bunge la Katiba. Katika hili mjumbe mmoja, Paulynus Raymond Mtenda aliteuliwa na hivyo kubeba uwakilish wa kundi zima la wasanii Tanzania. Siku ya Ijumaa 14/2/2014 Mashirikisho yote ya sanaa yalikutana BASATA na kumkabidhi rasmi mapendekezo yao Mbunge huyu, ili ahakikishe kundi hili haliachwi katika mchakato wa Katiba.
Muda mfupi baada ya hapo kundi hili lilikuja Dodoma, na kukutana na Wabunge mbalimbali wa Bunge hili la Katiba, tulikutana na Wabunge wa kambi zote na kufanya nao mikutano mingi, ambayo mingine ilifika mpaka saa nane za usiku. Wabunge wa kambi zote walionekana kuunga mkono hoja za wasanii na tulianza mawasiliano mbalimbali na Wabunge yakiwemo ya ana kwa ana, simu na email, Wabunge wakihitaji documentation mbalimbali kuhusiana na mapendekezo yetu katika Katiba mpya.  Katika kipindi hiki tulikuja wakati hata Mwenyekiti wa Bunde la Katiba hajachaguliwa. Ujumbe huu ulikuja tena …. Na hii ni mara ya tatu.
Ujumbe huu toka awali ulikuwa na maombi mawili tu.
i.                Wasanii kutambuliwa kama kundi maalumu kama yalivyotambuliwa makundi ya wakulima wafugaji, wavuvi. Sababu za kutaka kutambuliwa huku, ni kuwa kundi hili ni kubwa kuliko hata makundi mengine yaliyotajwa hapo juu. Takwimu za Baraza la Sanaa la Taifa za mwaka 2006 zinaonyesha kuwa wasanii nchini walikuwa kiasi cha milioni 6. Leo ni mika minane imepita na si siri kuwa kundi hili limekuwa na hivyo kukaribia robo ya Watanzania, si haki kutolitambua.
ii.              Milikibunifu (Intellectual Property) itajwa rasmi kama moja ya aina za mali zinazohitaji kulindwa katika katika Katiba
Tumekuja pia na mapendekezo ya namna ya kuingiza hoja zetu hizi zilizosahauliwa, hatujaja na  Ibara mpya kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyoonekana kutuhumu katika magazeti ya juzi. Mapendekezo yetu ni kuwa katika Ibara ya 30 iongezwe  aya moja tu ya. Na ibara ya 37 inayoongelea Haki ya ulinzi wa mali, itambue kuwa pamoja na mali zinazohamishika na zisizohamishika, pia kuna mali isiyoshikika.
Tumepata faraja kubwa kupokelewa na Bunge hili,  Na kuweza kuzunguka kwenye kamati 9 kwa hizi siku mbili kukumbusha mapendekezo yetu haya, ambayo hayabebi tu wasanii bali pia wavumbuzi wa kiteknolojia, kibailojia, wasomi watafiti, na wananchi wote kwa ujumla. Pendekezo letu la pili ni muhimu katika kulinda na kuendeleza uchumi wa Tanzania. Na sisi kama Watanzania tumeona ni muhimu kutumia nafasi hii adimu kuhakikisha tunatoa mawazo yetu katika Bunge hili kwani tusipotumia nafasi hii tutakuwa hatukujitendea haki wala kuvitendea haki vizazi vijavyo vya Tanzania.


SIMON MWAKIFWAMBA-SHIRIKISHOLA FILAMU TANZANIA (TAFF)


JOHN KITIME….MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA (TAMUNET)

Saturday, August 16, 2014

UMUHIMU WA MILIKIBUNIFU KUTAJWA KATIKA KATIBA MPYA

Katika Rasimu ya Katiba kumetajwa ulinzi wa mali, lakini ni wazi mali hizi ni zile zililzozoeleka katika akili za watu mali zinazohamishika na zisizohamishika. Kuna aina ya tatu ya mali ni ile inayotokana na ubunifu, na kwa sasa ndio mali inayolindwa zaidi na mataifa mengi, kwani ndio inayoleta ugunduzi wa madawa, mitambo, teknolojia, sanaa, na maendeleo ya kila aina. Hii huitwa Milikibunifu. Ni muhimu kutajwa kama zilivyofanya nchi nyingine ambazo zimefaidika sana na kulinda milikibunifu za wananchi wake.....
Milikibunifu au Intellectual Property Rights ni haki anazopewa mbunifu ili kulinda hali za mali yake ambayo haishikiki. Mali hii iyokanayo na ubunifu ni muhimu kuilinda kwani matokeo ya mali hii huwa faida kubwa kwa jamii. Milikibunifu ndizo haki ambazo huwalinda wagunduzi wa maendeleo katika teknolojia, madawa ya binadamu mifugo na kilimo, njia mbalimbali za kuongeza ubora na ufanisi wa teknolojia. Milikibunifu imegawanywa katika makundi mbalimbali ya ulinzi;
i.                Patent – (Hataza) hii ni njia ya kulinda na kusajili uvumbuzi mbalimbali wa kiteknolojia. Mfano vifaa vya kuvunia mazao kwa haraka zaidi, au kulima kwa haraka zaidi, vifaa vya uvuvi wa haraka, vifaa vya mawasiliano na vifaa vyovyote ambavyo vitaongeza thamani ya maisha yetu. Katika nchi kama Korea ya Kusini ulinzi wa Milikibunifu uliwekwa katika Katiba kuanzia baada ya vita ya pili ya dunia kwa kufusts mfumo wa  Katiba ya Marekani na ulinzi huo umeifanya wananchi wake ambao ni wabunifu kuweza kuja naubunifu ambao unatikisa dunia vifaa kama Samsung, Daewoo, KIA, LG ni matokeo ya ulinzi wa kikatiba wa wa Milikibunifu
ii.              Trademarks – (Alama za Biashara ) Alama za biashara huweza kufikia hatua ambapo zikawa na thamani kubwa kwani huweza kuaminika. Ili kulinda zisitumiwe hovyo au hata kuibiwa na wenye uwezo zaidi hulindwa na sheria za kulinda alama hizi. Kwa mfano Cocacola, Vodacom, Dell, na hapa kwetu Azam, ni majina ya bidhaa ambazo zina aminika, na hivyo kuwa na dhamani kubwa japo hazishikiki, nazo ni sehemu ya mali  ambazo hazishikiki lakini zina thamani kubwa
iii.             Industrial designs – Hizi ni haki wanazopewa wale wenye ubunifu wa kuweza kufanya usanii wenye kuboresha muonekano wa kitu ambacho tayari kimeshagunduliwa. Kwa mfano kila mtu ana simu ya mkononi lakini muonekano wa simu mbalimbali shape nap engine hali ya kuwa ni ya ku slide au kufungua au kupokea moja kwa moja ni matokeo ya design, pia vitu kama design za nguo, viatu , kiti ulichokalia makochi magari, vyote hivyo ndivyo matokeo ya industrial designs. Kazi za ubunifu huo ni muhimu kulindwa kwani huwa na thamani kubwa sana, kwa mbunifu na kwa mchango wake kwa nchi.  
iv.             Geographical Indication – Huu ni utambulisho wa wapi chanzo cha mali husika. Kwa mfano mvinyo kutoka Dodoma, Dodoma Wine ni mzuri na hivyo huitwa Dodoma Wine bila kulinda hili, watu watachukua mvinyo huu na kuupa hata jina jingine ukaitwa South African wine na hivyo kuiba haki wanazostaili kupata wakulima wa Dodoma, kutambuliwa kwa jina hili kutasababisha kutakiwa zaidi kwa wine hii duniani na hivyo kuweza kufanya hata Dodoma kuwa Wine City jambo ambalo linawezekana lakini nchi haijatambua umuhimu huu. Pia kuna mchele wa Kyela, Dagaa wa Kigoma na vitu kama hivi ambavyo havipatikani popote duniani kasoro sehemu iliyotajwa.  Nchi kama Uswiss imejenga jina miaka mingi ya utengenezaji wa saa bora hivyo saa ikiandikwa Swiss made huwa inajulikana ni bora na huwa gharama zaidi, Sigara kutoka Cuba, Cuban Cigars ni bei kubwa kwani hazipatikani popote kasoro Cuba, au mvinyo maarufu kama Champagne, ambao hutoka jimbo la Champagne Ufaransa, umejijengea sifa kubwa duniani na kuwa na bei kubwa sana kiasi cha kwamba si rahisi kwa mtu wa kipato cha kawaida kununua. Harusi zetu hutumia Sparkling Wine na kuiita Shampeni.
v.              Hakimiliki na Hakishiriki – Hizi ni haki zinazolinda kazi za kisayansi na kisanii. Computer Programs, Data, Utunzi wa vitabu, miswaada, hotuba, uchoraji, muziki, kazi za usonara, picha za mnato na filamu, uchongaji na kadhalika. Kazi hizi zimekuwa ni chanzo cha utajiri mkubwa kwa watu binafsi na Mataifa. Katika nchi ya Marekani kazi za Hakimiliki na Hakishiriki ni za pili katika uchangiaji wa pato la Taifa. Ripoti ya WIPO ya 2010 ilionyesha kuwa katika nchi ya Tanzania kazi za hakimiliki na Hakishiriki zilichangia asilimia 4.3 ya pato la taifa, karibu mara mbili ya mchango wa Madini!. Katika mwaka 2009 kazi za hakimiliki zilitengenza aslimia 5.63 ya ajira nchini, ikiwa juu ya mchango wa Afya (4.23), Biashara na mambo ya Fedha Real estate, &Business Service(2.37), Ujenzi (1.38),Usafirishaji na Mawasiliano (0.92), Umeme, Gas na maji (0.91), Madini (0.89)
Pamoja na umuhimu huu, Katiba inataja mali zinazoshikika tu-Zinazohamishika na zisizohamishika, hivyo mali hizi ambazo zimeonyesha kuleta maendeleo makubwa kwa nchi ambazo wakati wa Uhuru tulikuwa sawa kwa mfano Thailand, India, Malasia, Korea kusini ambazo zote zimetuacha mbali ni kwa ajili ya ulinzi wa mali hizi zisizoshikika ambazo ndizo pia zinawezesha mazingira ya kuingiza fedha nyingi za uwekezaji kutoka kwa wenye pesa na kuanzisha viwanda vyenye mali ya asili ya hapa. Nchi zote zinazoendelea ambazo ziliwahi kuona umuhimu wa kuweka kipengele cha miliki bunifu katika Katiba yake mapema, zimeweza kupata maendeleo ya haraka kama nilivyotaja hapo juu.

 Mifano ya nchi nyingine….
Marikani ni nchi moja wapo ambapo ulinzi wa Milikibunifu umewezesha maendeleo makubwa katika sanaa na teknolojia,
·      U.S. Constitution. Article I, Section 8 provides: "The Congress shall have Power … To promote the Progress of Science and useful Arts, by securing for limited Times to Authors and Inventors the exclusive Right to their respective Writings and Discoveries."
·      The Constitution of Malaysia, which is the supreme law of Malaysia, was adopted on 31 August 1957. Since then, the Constitution has been amended many times, most recently in 2009.
The Constitution contains provisions on intellectual property.
In the Legislative Lists (List I-Federal List) of the Ninth Schedule, the Constitution gives the federal government the power to enact laws relating to patents, designs, inventions, trade marks and mercantile marks, copyrights (Section 8 (e)).
·      Article 22 ya Katiba ya South Korea inasema (1) All citizens shall enjoy freedom of learning and the arts. (2) The rights of authors, inventors, scientists, engineers, and artists shall be protected by Act

Thursday, July 10, 2014

MWENYEKITI WA MTANDAO WA WANAMUZIKI TANZANIA, AFUNDISHA WAALIMU WA NURSERY MUZIKI

Ili kupata kizazi kitakachoweza kupenda muziki na kutumia vifaa vya muziki ni vizuri kuhakikisha unapata waalimu bora wa muziki. Na ni vizuri kuanza kufundisha watoto wakati wakiwa bado wadogo. Kufanikisha hili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania-John Kitime, akishirikiana na Chuo cha Montesori cha Waalimu wa Shule za Nursery, wameanza mpango wa kuwawezesha waalimu kujifunza japo chombo kimoja cha muziki, na pia njia rahisi za kutunga nyimbo za watoto. Waalimu wanafunzi watarekodi nyimbo walizotayarisha na kuondoka nazo baada ya kumaliza masomo ili waweze kuzitumia kufundishia wanafunzi kwenye vituo vyao.










Thursday, June 19, 2014

COSOTA KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA


Rob Hooijer
CHAMA cha Hakimiliki cha Tanzania kimekuwa katika wiki moja na nusu ya warsha, na mikutano ya kukiboresha ambayo inaendeshwa na mtaalamu Robert Hooijer kutoka Afrika ya Kusini. Kazi kubwa iliyokuwa inafanyika ni kuiwezesha COSOTA kufanya kazi katika mifumo ya kisasa ya ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha. Mr Hooijer ni mtu mwenye uzoefu wa miaka mingi katika shughuli za Hakimiliki, aliwahi kuwa CEO wa CISAC, ambacho ndicho muungano wa vyama vyote vya ukusanyaji mirabaha duniani na pia alikuwa CEO wa South African Musicians Rights Organisation (SAMRO) ambayo ndicho chama kikubwa kuliko vyote cha ukusanyaji wa mirabaha Afrika. Kwa kipindi hiki amekuwa Kenya akisaidia shughuli kama hii na mafanikio makubwa yamewezekana huko.









WASANII WAKUTANA NA KUTOA MCHANGO KATIKA UTAYARISHAJI WA SERA YA MILIKIBUNIFU YA TANZANIA



Wasanii kadhaa wakiwemo viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa yote yaliyopo,wiki iliyopita walikutana katika ukumbi wa Chichi Hotel Kinondoni kutoa mchango wao katika utengenezaji wa Sera ya Taifa ya Milikibunifu (National Intellectual Property Policy). Katika mradi huu wa pamoja wa Tanzania Musicians Network (TAMUNET) na Tanzania Film Federation (TAFF), ambao umefadhiliwa na BEST AC, wasanii hawa walipata nafasi kuchangia mambo mbalimbali kuhusu kipengele cha Hakimiliki katika sera ya Milikibunifu. Washiriki wakiongozwa na mtaalamu Ernest Omalla na John Kitime , Mwenyekiti wa TAMUNET na wataalamu kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, mambo mengi yalipendekezwa yawemo katika sera hiyo.Bado zinatafutwa taratibu za kuweza kuwapata wadau wengine wa Hakimiliki ili waweze kuongeza ubora wa sera hii.












ARTISTS HOLD A STAKEHOLDERS MEET ON PROPOSED INTELLECTUAL PROPERTY POLICY

The Ministry of Industry and Trade is in the last phase of preparing the National Intellectual Property Policy. The Policy has been in preparation since 2012. A few days ago artists brought together by Tanzania Musicians Network and Tanzania Film Federation with the help of a grant from Best AC, gathered at the Chichi Hotel in Kinondoni and  spent hours coming up with suggestions for the Copyright section of the Policy. Present at the meeting were leaders and members of all the four Federations of Artists and the Tanzania Musicians Network (TAMUNET), also present were officials from the Ministry  of Industry and Trade. Tanzania Musicians Network will work with Tanzania Film Federation in collecting all the suggestions of the artists together with other Copyright stakeholders and together come up with a workable Copyright policy for presentation to the Government.