Saturday, March 19, 2016

DKT AYUB RIOBA CHACHA MKURUGENZI MKUU MPYA TBC

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AMEMTEUA DKT AYUB RIOBA CHACHA KUWA MKURUGENZI MPYA WA TBC. DKT RIOBA ANACHUKUA NAFASI YA CLEMENT MSHANA ALIYESTAAFU.

WAZIRI NAPE NNAUYE KUKUTANA NA WANAMUZIKI JUMATATU 21 MARCH 2016

12347733_1139421576075747_4085232307530687920_nKATIKA hatua ya kujua mafanikio na changamoto za muziki wa dansi na hatimae kupanga yajayo, Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo atakutana na wanamuziki wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni siku ya Jumatatu kuanzia saa nne asubuhi. Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka mingi kwa Waziri wa Utamaduni kufanya mkutano wa namna hii na wanamuziki.