Wednesday, April 29, 2015

MTANDAO WA WANAMUZIKI WAWEZESHA WANAMUZIKI KUPATA HUDUMA YA BIMA YA AFYA

Wanamuziki wanachama wa Tanzania Musicians Network -TAMUNET_ sasa wanaweza kujiunga na mpango nafuu wa Bima ya Afya baada ya chama chao kuingia katika makubaliano na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF.
WAnamuziki walikuwa ni kundi mojawapo ambalo limekuwa na tatizo kubwa la kupata matibabu bora kutokana na kukosa taratibu za bima ya afya, jambo ambalo ni njia ya kisasa na ya uhakika wa kupata matibabu bora kwa kila binadamu.
Katika kikao cha viongozi wa chama hicho leo kamati maalumu imeundwa kuratibu mpango huu ambapo kamati hii itakuwa ikiandikisha wanachama wote wanaohitaji kupata huduma hii muhimu. Kamati itakuwepo kila Jumatano kuanzaia saa nne mpaka saa tisa katika ofisi za Mtandao zilizopo katika jengo la ghorofa lililojengwa kwa matofari ya kuchomwa jirani na hospitali ya Mvungi katika barabara ya kuelekea mahakama ya Kinondoni, chumba namba 148. Pia unaweza kuwasiliana na Mweka hazina Asha Salvador kupitia simu namba 0687378797 kwa maelezo ya ziada